RC Makonda Azindua Chama Cha Waendesha Bodaboda Na Bajaj Mkoa Wa Dar es Saalam

makondaMkuu wa mkoa Paul Makonda akihutubia.makonda-32Sehemu ya umati ya waendesha bodaboda waliojitokeza.makonda-1-001Mmoja wa madereva aliyeshiriki zoezi hilo akiwa kwenye muonekano mpya.makonda-7Mkuu wa Mkoa akiongozana na baadhi ya viongozi wa chama hicho.makonda-12Sehemu ya umati waliohudhuria zoezi hilo.makonda-13Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akivaa koti kama ishara kwa madereva wote ambao watapaswa kuvaa wawapo safarini.makonda-17Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akijianda kuvaa Helmet.makonda-18Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiwa tayari kuvaa kofia nguvu ‘Helmet.’makonda-22Mkuu wa Mkoa Paul Makonda akiwa katika muonekano mpya wa madereva wa bodaboda.makonda-24Mkuu wa Mkoa akiongoza maandamano ya waendesha bodaboda yaliyoanzia viwanja vya Biafra na kuishia viwanja wa Leaders, Kinondoni. makonda-28 Kopro Rioba akieleza jambo kwenye uzinduzi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam mheshimiwa Paul Makonda, mapema leo amezindua Chama cha Waendesha Bodaboda na Bajaj kwa Mkoa wa Dar es Salaam. Pia ameongoza maandamano ya waendesha bodaboda kuanzia viwanja vya Biafra hadi viwanja vya Leaders vyote vipo wilaya ya Kinondoni ikiwa kama ishara ya uzinduzi huo.
Uzinduzi huo umeambatana na mpango wa muonekano mpya wa madereva kwa kuwa na kofia nguvu ‘Helment’ za kisasa na vizibao ambapo awali wengi wao walikuwa hawana kutokana na kutomudu gharama za manunuzi.
Mkuu wa mkoa ametumia nafasi hiyo kuwaomba madereva kuwa mabalozi kwa wenzao wanaovunja sheria za Barabarani kwa kupakiza abiria zaidi ya mmoja ‘Mshikaki’.
Amewaomba bodaboda kuacha kutumia vilevi wakati wanafanya kazi zao za usafirishaji.
“Tumeongeza vituo vya Bodaboda na Bajaj kushirikiana na SUMATRA ili kurahisisha usafiri katika Jiji la Dar es Salaam.” Amesisitiza mkuu huyo wa mkoa.

Comments

Popular posts from this blog