Waziri Mkuu aongoza Swala ya Eid El Fitr jijini Dar

1.Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa akihutubia umati wa waislamu katika viowanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa akitoa mawaidha  mbele ya waumini wa kiislamu katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. 2.Waziri Majaliwa akisoma hotuba yake.Waziri Mkuu Majaliwa akiendelea kutoa mawaidha yake kwa waumini hao ambao hawapo pichani. 3.Mufti Mkuu wa Tanzania, Shekh Abubakar Zuber akisoma mawaidha yake mbele ya waumini wa kiislamu.           Mufti Mkuu wa Tanzania, Shekh Abubakar Zubery akitoa mawaidha yake mbele ya waumini wa kiislamu.
4.She Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa akiongea na waumini wa dini ya kiislamu katika kuwatakia sikukuu njema waislamu kote duniani.Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa akiongea na waumini wa dini hiyo na kuwatakia sikukuu njema waislamu wote nchini.
5.Kutoka kushoto mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi, Rais Mstaafu, Ally Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa.Kutoka kushoto mbele ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi, Rais Mstaafu, Ally Hassan Mwinyi na Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa.
6. Waumini wakiomba dua.Waumini wakiomba dua.
7.Alhadi Mussa akihutubia waumini wa dini ya kiislamu katika viwanja vya Mnazi Mmoja.Alhadi Mussa akihutubia waumini wa dini ya kiislamu katika Viwanja vya Mnazi Mmoja.
8.Taswira ya viwanja mnazi Mmoja palivyoonekana.Taswira ya  baadhi ya waumini waliojitokeza katika Viwanja vya Mnazi Mmoja inavyoonekana.
9Sehemu ya waumini akinamama walijitokeza katika swala hiyo kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja.
10
11
12
13
14
WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Majaliwa Kassim Majaliwa mapema leo Jumatano, ameongoza waumini wa dini ya kiislamu  katika swala ya Eid El Fitr  iliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na waumini mara baada ya swala hiyo, Waziri Mkuu Majaliwa aliwataka waislamu  wote nchini kusherehekea sikukuu hiyo kwa kufanya matendo mema ya kumpendeza Mwenyezi Mungu.
Amewataka waumini wote kuwaombea dua maalum watu waliopoteza maisha katika ajali  ya gari iliyopoteza maisha ya abiria 30 iliyotokea juzi Jumatatu mkoani Singida.
Naye Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakary Zubery amewaomba waumini wa dini hiyo na wakristo kukaa pamoja na kula pamoja, kusherehekea sikukuu hiyo ikiwemo kutoa sadaka kwa wagonjwa na wasiojiweza.
Aidha Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salum naye alitoa nasaha zake kwa waumini wote wa kiislamu kwa kufikisha siku ya leo ya mfungo wa  mwezi mtukufu wa Ramadhani na kuwataka wanaoendelea kwa  kufunga sita wawe na mfungo mwema.
NA DENIS MTIMA/GPL

Comments

Popular posts from this blog