Breaking Newzzz…..Mwingine adakwa kwa kumkashifu Rais Magufuli kwenye mtandao wa “Whats App”

Sheria ya Makosa ya Kimtandao inaendelea kushika kasi, mwingine tena aingia matatani baada ya kubainika kutumia Lugha mbaya dhidi ya Rais kwenye mtandao wa WhatsApp.
Hapa cha muhimu ni kujuwa sheria hii inafanya kazi, inakamata, inahukumu na kufunga wananchi. Tutumie lugha ya staha, vijana hamko salama kwenye fb, twitter na WhatsApp…sheria ya mitandao ipo na inazunguka kama Simba aungurumae akitafuta mawindo.
=========
Leonard Mulokozi Kyaruzi amefunguliwa mashtaka kwa kumkashifu Rais John Pombe Magufuli kupitia mtandao wa WhatsApp tarehe 2 Juni 2016. Kyaruzi anatuhumiwa kutenda kosa hilo akiwa jengo la Tanzanite jijini Dar es Salaam ambapo aliandika “Hivi huyu Pombe ni kwamba hana washauri? Hashauriki? Au ni zuzu? Bwege sana huyu jamaa, he doesn’t consider the law in place before opening his mouth!. Au na yeye anaumwa ugonjwa wa Mnyika?” Ilisema sehemu ya hati ya mashtaka.

Comments

Popular posts from this blog