SNURA :CHURA IMENIONGEZEA UMAARUFU


STAA wa Muziki wa Kizazi Kipya, Snura Mushi amefunguka kuwa licha ya changamoto ya kutakiwa kutengeneza video mpya yenye maadili ya wimbo wake wa Chura, umaarufu wake umeongezeka kwani jina lake limekuwa gumzo kila kona nje na ndani ya nchi.  Akipiga stori na gazeti hili, Snura alisema tangu aanze muziki hajawahi kufanya mahojiano na watu wengi kama kipindi hiki, kwani japokuwa alitakiwa na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kurekebisha wimbo huo, amepata faida kubwa kimuziki na kiakili.
“Ukiachana na changamoto nimefarijika sana kwani jina langu limekuwa gumzo kila kona, nimepata elimu ambayo sikuwa nayo ambapo wizara imenipa ubalozi wa kuwafundisha wenzangu wasitoe nyimbo zisizokuwa na maadili, hivyo kila ninapokutana na wasanii wenzangu nawafundisha,” alisema

Comments

Popular posts from this blog