Mwanasheria Mkuu Zanzibar Aapishwa Rasmi

1 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein akimuapisha Bwana Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Unguja..
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Bwana Said Hassan Said, kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
2Wageni waliohudhuria kwenye hafla hiyo ya kuapishwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyeikiti wa Baraza la Mapinduzi alimteua Bw. Said Hassan jana kushika wadhifa huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 55 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Hafla ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu huyo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
3
Miongoni mwao ni Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman Makungu, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis.
Wengine ni Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa Wadi, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib,Washauri wa Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali

Comments

Popular posts from this blog