Kiwanda Bubu Cha Kutengeneza Pafyumu Feki Chakamatwa Dar es Salaam



Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) wamekamata kiwanda bubu kinachotengeneza pafyumu bandia kilichopo eneo  Tuangoma, mtaa wa Goroka Wilala ya Temeke.

Kukamatwa kwa kiwanda hicho kinachotengeneza pafyumu aina ya SAME,  kunatokana na TFDA kupata taarifa kutoka kwa wananchi kuwa  kuna shehena kubwa  ya pafumu hizo katika duka moja la vipodozi lililopo Sinza kwa Remmy wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari  leo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Hiiti Sillo alisema TFDA kanda ya mashariki baada ya kupata taarifa za kuwepo kwa kiwanda hicho kutoka kwa wasamaria wema, walifanya ukaguzi katika duka hilo la vipodozi na kukamata  chupa 5,350 za pafyumu aina ya  SAME zenye thamani ya Sh 107 milioni.

“Februari 23,mwaka huu tulifanya ukaguzi katika duka hilo lililopo Sinza kwa Remmy na kukuta pafyumu  5,350 ambazo zinauzwa Sh 20,000 kwa chupa moja ya pafyumu na pia tuligundua kuwa duka na pafyumu hizo zilikuwa hazijasajiliwa wala hazina kibali kutoka TFDA”Alisema Sillo.

Alisema, awali  maelezo aliyowasilisha na  mmiliki wa duka hilo katika ofisi za TFDA kanda ya mashariki  yalionyesha kuwa shehena hiyo ya pafyume  iliingizwa nchini Desemba 27, mwaka jana kutoka nchi ya Uturuki kupitia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, lakini tulivyofanya uchunguzi  tulibaini kuwa zinatengeneza hapa nchini.

“Kufuatia kukamatwa kwa shehena hii ya pafyumu ambayo ni sawa na katoni 83, tuliendelea kufanya uchunguzi  ambapo tuliambiwa kuwa zinatengenezwa hapa nchini na sio Uturuki”aliongeza.

Alisema kufuatia taarifa hizo, Februari 29,mwaka huu TFDA wakishirikiana na Jeshi la Polisi walifanya ukaguzi na kupekua katika nyumba ya Mwanaidi iliyopo eneo la Tuangoma mtaa wa Goro Wilaya ya  Temeke na  kubaini kuwepo kwa kiwanda  kinachozalisha pafyumu hizo

Comments

Popular posts from this blog