BREAKING NEWS : TUHUMA ZA RUSHWA KAMATI ZA BUNGE: Mbunge Zitto amejiuzulu

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, ameishtumu Kamati ya Huduma za Jamii anayohudumu kuwa kuna baadhi ya Wajumbe hupokea rushwa.
Kutokana na shtuma hizo ameamua kumuandikia spika kumtaka achunguze na kuchukua hatua.
Kauli yake ianapatikana hapa chini;
"Kuna tuhuma za rushwa dhidi ya Kamati mbalimbali za Bunge ikiwemo kamati ninayohudumu. Nimemwandikia Spika Kuomba Uchunguzi juu Ya tuhuma hizo na kwamba achukue hatua kali dhidi ya yeyote atakayekutwa kuhusika na vitendo vya rushwa. Nimejiuzulu Ujumbe wa Kamati ili Kutoa Nafasi Ya Uchunguzi Husika.

Comments

Popular posts from this blog