Miss Tanzania ataka namba ya Samatta

MaureencropnewMshiriki wa Miss Tanzania 2005 ambaye pia ni mcheza fi lamu, Maureen Gislary.
Imelda Mtema,Dar es Salaam
MSHIRIKI wa Miss Tanzania 2005 ambaye pia ni mcheza fi lamu, Maureen Gislary ameibuka na kutaka namba ya simu ya mchezaji wa timu ya Taifa Stars na Klabu ya TP Mazembe ya DR Congo, Mbwana Samatta kwa gharama yoyote.
Samatta-Waziri-Mkuu-15Mbwana Samatta.
Akizungumza na Amani Sports, Maureen aliyekuwa kumi bora katika kinyang’anyiro hicho cha Miss Tanzania kilichoshuhudiwa kwa Nancy Sumari kuibuka mshindi alisema kuwa, nia ya kuhitaji namba hiyo nikuhakikisha anamuweka Samatta ‘kibindoni’ kabla hajatimkia nje ya nchi.
“Kwanza nimefurahishwa sana na ushindi wake wa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika kwa Wachezaji wa Ndani mwaka 2015, mwenye namba yake tafadhalini naiomba kwa gharama yoyote nitatoa,” alisema Maureen.

Comments

Popular posts from this blog