MADENTI MSINGI WAJIUZA SH.2000 HUKO MOROGORO!

UKISTAAJABU ya Musa utayaona ya Farao! Kumekuwa na madai ya baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi mjini hapa kujiuza kwa waendesha bodaboda kwa gharama ya shilingi elfu mbili tu. Mwanafunzi anayedaiwa kujiuza kwa waendesha Bodaboda. Kufuatia madai hayo, mwandishi wa kikosi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ mjini hapa alifanyia kazi madai hayo na kufanikiwa kumnasa Ally Shabani (34) ambaye ni dereva wa bodaboda akiwa na mwanafunzi wa darasa la nne, Shule ya Msingi ya Kiwanja cha Ndege mkoani hapa (jina tunalo).Tukio hilo la kushangaza na kusikitisha pia, lilijiri Jumamosi iliyopita saa 7 mchana katikati ya mashamba ya mkonge yaliyopo Kihonda Kwachambo ambayo yanamilikiwa na Jeshi la Magereza jirani kabisa la Gereza la Kihonda

MAMA MZAZI AISAKA OFM
Awali, mama mzazi wa denti huyo, Mariam Jongo alimtafuta Kamanda wa OFM Mkoa wa Morogoro na kumweleza kuhusu tabia ya bodaboda huyo na mwanaye, alisema:
”Naomba msaada wako baba, kuna dereva wa bodaboda nimempa tenda ya kumpeleka mwanangu shule.
“Lakini cha ajabu nasikia anamshawishi mwanangu mwenye umri wa miaka 9 ambaye hata maziwa hayajaanza kutoka kifuani ili afanye naye mapenzi akitumia chambo cha shilingi elfu mbili, hivyo naomba msaada wako kama kamanda wa kufichua maovu.”

Waliponaswa kichakani. OFM YATOA MBINU
Kamanda wa OFM alimpa maelekezo mama huyo ya kutafuta vijana wa polisi jamii wa kata ambapo baada ya kupatikana mwandishi wetu alimpa maelekezo denti huyo na baadaye kwa kushirikiana na polisi jamii na OFM walitega mtego.
DENTI AMPIGIA BODABODA
OFM alimuita denti huyo na kumpa simu ili ampigie bodaboda huyo ambapo alimtaka aende kijiweni kwake Kihonda kwa Chombo, Mwisho wa Hiace. Denti alilazimishwa na mama yake afike kwenye kijiwe hicho akiwa anafuatwa kwa karibu na OFM na polisi jamii.
BODABODA AMPANDISHA DENTI KWENYE BODABODA
Bila kujua kuwa yupo kwenye mtego, bodaboda huyo alimpakia denti ambaye alionywa kutosema kuhusu mtego na kuondoka naye huku akiendelea kufuatiliwa kwa nyuma na kikosi kazi hicho.
Alipofika jirani na Barabara ya Mazimbo, alisimama, akataka kuingia naye gesti lakini akajishtukia kwa vile ilikuwa mchana na jua kali.


Dereva bodaboda Ally Shabani aliyedaiwa kukutwa na mwanafunzi akiwa mikononi mwa wananchi.
AAMUA KWENDA MKONGENI
Bodaboda huyo alipoona ilikuwa vigumu ‘kujitoma’ gesti na mtoto wa watu, alielekea kwenye shamba la mkonge lililoko kando ya Barabara ya Dodoma na kuzama ndani.
Njemba huyo alijiongeza kwa kusimamisha bodaboda katikati ya shamba na kukaa chini na mtoto huyo ambapo walianza ‘love story’ kwanza.
OFM HIYO!
Ndani ya dakika 10 tu, OFM na kundi lake waliwavamia kwa nyuma na kumkamata bodaboda huyo na kumuuliza kisa cha kuangukia kwa mtoto kama huyo ambaye ni sawa na mwanaye wa kumzaa akiwa ameshamkatia shilingi elfu mbiliUTETEZI WAKE
Katika utetezi wake, bodaboda huyo huku akiangua kilio alimtupia lawama shetani na kuomba msamaha akisema yeye ni mume wa mtu na mkewe analea!
”Shetani kanipitia jamani, mke wangu analea mtoto wetu wa mwisho ana mwaka mmoja kasoro, naombeni msamaha yaishe hapahapa, mnifichie aibu hii,” alisema bodaboda huyo.
WATU KIBAO
Baada ya muda habari za bodaboda huyo kufumwa zilisambaa kwa kasi ya upepo na watu kibao walifurika kwenye shamba hilo huku baadhi ya bodaboda wenzake kwa hasira walimshushia kichapo mwenzao huku baadhi wakitaka kumuua.


Binti huyo akiwasili kijiweni. POLISI WAITWA
Baada ya kuona jamaa anaweza kuuawa, OFM waliita polisi wa pikipiki ambapo kwa mshangao, mmoja wa polisi hao alisema:
”Sisi tuna bifu na bodaboda baada ya mwenzetu kupigwa kule Mindu. Kama unaweza mpakie kwenye pikipiki yako mlete kituoni.”
Ilibidi OFM iite askari magereza ambao walimchukua bodaboda, denti na mzazi wake na kwenda ofisi zao zilipo jirani na shamba hilo.
Baadhi ya watu, hasa wanawake waliokuwepo eneo hilo walisikika wakisema huenda bodaboda huyo alikuwa na lengo la kishirikina.
”Hii siyo bure hiki kitoto kinajua nini katika mapenzi. Huyu huenda ametumwa na mganga wa kienyeji. Sisi wamama tuko hatuna waume ameshindwa nini kuja... kwetu?” alihoji mwanamke mmoja.


...Wakiondoka. MADAI YA KUJIUZA
Kwa mjini Morogoro, baadhi ya bodaboda wanadaiwa kutumia nafasi ya kuwa na chombo hicho cha usafiri kuwalaghai wanafunzi wa shule za msingi kwamba, wakilala nao watakuwa wanawapakiza kwenda shule na pia kutumia shiling elfu mbili kama chambo kikubwa.
“Kwa sasa mjini Morogoro madenti wa shule za msingi kujiuza ndiyo fasheni, wanarubuniwa na shiling elfu mbili na lifti. Jamani, watoto wetu watasoma kweli?” alihoji mwanamke mwingine.

Comments

Popular posts from this blog