LOWASSA AFUNGUKA KUHUSU MAISHA YAKE KISISASA


Leo ninasherehekea siku yangu ya kuzaliwa na kwa namna ya pekee ninamshukuru Mungu kwa kuendelea kunibariki, kunishika mkono na kuniongoza. Maisha yangu ni mfano wa baraka za Mungu. Kuna nyakati nilianguka lakini  kwa upendo wake akaninyanyua na mpaka sasa ameendelea kunionyesha baraka zake. Kwa namna ya pekee ninapenda kuishukuru familia yangu na watanzania wenzangu kiujumla kwa upendo na imani yao juu yangu hata pale nilipopitia vipindi vigumu katika maisha yangu. Nina furaha zaidi leo kwa kuwa ninasherehekea siku yangu ya kuzaliwa nikiwa katika kilele cha mapambano ya kusaidia wananchi wenzangu

Comments

Popular posts from this blog