ACHENI RUSHWA TUISAIDIE NCHI IPATE MAENDELEO, MAGUFULI.

Waziri wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli akizungumza katika ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi wa wizara Ujenzi katika Hoteli ya Peacock jijini Dar es Salaam leo.
 Mhandisi Mussa Lyombe akizungumza leo jijini Dar es Salaam,katika ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya ujenzi.

 Baraza la wafanyakazi wa wizara ya ujenzi waliohudhuria katika ufunguzi wa baraza hizo leo jijini Dar es Salaam.

 Picha ya pamoja ya waziri wa Ujenzi pamoja na Baraza la wafanyakazi wa wizara ya ujenzi. Picha zote na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii WAZIRI wa Ujenzi Dk.John Pombe Magufuli amewataka wafanyakazi katika wizara hiyo kuacha rushwa na badala yake wafanye kazi kwa weledi katika kusaidia nchi kuendelea katika ujenzi wa barabara.
Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akifungua Baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo,amesema wizara hiyo imekuwa na mafanikio kutukana na wafanyakazi kujituma katika miradi mbalimbali.
Amesema madaraja na barabara yaliyokuwa yakisumbua tangu nchi ipate uhuru yamekamilika katika kipindi cha miaka mitano ya Rais Jakaya Kikwete na miradi mingine inaendelea ambayo Tanzania itakuwa nchi ya kuigwa katika kwa kuwa madaraja ya juu.
Aidha amesema Wizara ya ujenzi imevuka hata ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kutokana na kutekeleza miradi kwa asilimia 91.
Magufuli amesema katika sekta ya usafirisha kwa njia ya barabara ndio inabeba uchumi kutokana na kutegemea kwa asilimia 99.7 huku usafiri wa Reli,Maji na Anga ikiwa na asiliamia 0.7.
Magufuli amewataka wafanyakazi kuacha kulalamika kwani wanaweza kulalamika hata kama vitu vinavyofanywa ni vizuri na hiyo ndio umekuwa utamaduni wa watanzania.
Amesema kwa vivuko vilikuwa 15 lakini sasa viko 30 hali ambayo imerahisisha usafiri kwa wakazi wanaotumia vivuko na kufanya maeneo hayo kukua kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog