ZARI AFUNGUKA KUHUSU UVUMI KUWA HANA MAELEWANO NA BABA WA WATOTO WAKE

Zarinah “The Boss Lady” Tlale a.k.a mama kijacho au kama anavyofahamika kwa kifupi Zari, amekanusha uvumi ulioenea kuwa yeye na mme wake wa zamani ambaye ni baba wa watoto wake watatu, Ivan Ssemwanga kwa sasa hawazungumzi kutokana na kuwa kwenye mtafaruku mkubwa.
“Nina watoto watatu wa kiume wa kwanza ana miaka 12 wa pili 10 na mwingine ana miaka 8 wako poa na nina jivunia kuwa mama.” Alisema Zari kupitia E-Newz ya EATV.
(Kuhusu baba wa wanaye watatu) “Hatuko pamoja lakini tuko poa kwasababu kuna vitu vingine vinaendelea kati yetu wakiwemo watoto na mambo mengine mengi kwahiyo tuko poa. Unajua jinsi watu na vyombo vya habari wanavyochukulia ni kama tuna ugomvi na hatuzungumzi lakini sisi tuko poa kabisa.”
Zari pia amezungumzia kuhusu uhusiano wake na Diamond kwa kusema kuwa mapenzi yao ni ya wao wawili na sio ya watu wengine hivyo hawapendani ili kuwafurahisha wengine.
“Tuko poa, tunapendana lakini hakuna info zaidi. Sitaki kutoa taarifa zaidi ambayo tunaita ‘T.M.I’ (Too Much Info) Lazima huwa kuna kuwa na mitazamo hasi na mitazamo chanya, watu wengine watasema poa wengine watasema sio poa, lakini mwisho wa siku sio kile watu wanachofikiria na sio kile watu wanachotaka lakini ni nini sisi tunataka, nini kinachotupa furaha, je tunafuraha kuwa pamoja tunataka kuwa pamoja, ndo hivyo. Hatudate kwaajili ya watu, au kwasababu wao wanataka tuwe pamoja.”

Comments

Popular posts from this blog