ACHANWA NA NYEMBE NA KUTEMBEZWA UMBALI WA MITA 300 BILA NGUO UKO KIHONDA- MOROGORO

Aliyekatwa nyembe.
MWANAMKE mmoja,  Rehema Juma (21) ambaye ni mke wa mtu, mkazi wa Mtaa wa Msamvu B, Kata ya Kihonda Maghorofani mkoani Morogoro amechanwa na nyembe mwilini na baadaye kutembezwa bila nguo mtaani mchana kweupe akituhumiwa kufumwa na mume wa mtu.Tukio hilo la aina yake  ambalo lilivuta umati mkubwa, lilitokea Julai 5, mwaka huu saa 10 jioni katika Mtaa wa Msamvu B.Mashuhuda wa tukio hilo walipohojiwa na paparazi walidai kuwa kwa muda mrefu, Zaitun Ally (30) ambaye pia anaishi kwenye mtaa huo alikuwa akimshutumu Rehema akidai anatembea na mumewe, hivyo akaamua kutega mtego bila mafanikio.“Zaituni baada ya kushindwa kuwanasa leo aliamua kumuita Rehema nyumbani kwake na kudai amewafuma na mumewe hivyo kumchana nyembe baadaye kumvua nguo na kumtembeza bila nguo mtaani hadi nyumbani kwake umbali wa mita 300 mchana kweupe,” alisema mmoja wa mashuhuda hao aliyejitambulisha kwa jina la Ashura Ally.
Rehema Juma akiwa na mama yake.
Paparazi alifika nyumbani kwa Rehema na kumkuta akiwa amefungwa bendeji sehemu za mwili wake na alipoulizwa alifafanua:

“Ni kweli tukio hilo limetokea lakini siwezi kuzunguma peke yangu, twende kwa mama mkwe Mtaa wa Ngerengere.”
paparazi na Rehema walipofika kwa mkwe wa mtuhumiwa, Lilian Julius Sechonge ambaye ni mjumbe wa serikali za mtaa wa Ngerengere na kutakiwa kuzungumzia tukio hilo alikuwa na haya ya kusema:
Mtuhumiwa wa tukio hilo.
“Ni kweli Rehema ni mkwe wangu kwa mwanangu aitwaye Godfrey Sechonge anayeishi naye hadi sasa, Julai 5, mwaka huu mwanangu huyo alikuja na akaniambia mkewe anatembezwa bila nguo.

“Nilifika eneo la tukio na kumkuta mkwe wangu yuko uchi huku akivuja damu mwili mzima.
“Aliniambia amecharangwa viwembe na Zaituni akimshutumu kutembea na mumewe, nilimchukua mwanangu na kumkimbiza polisi ambapo tulipewa PF3 na kufunguliwa jalada namba MOR/RB/4009/2014.”

Naye Rehema alipozungumzia kisa hicho alisema siku ya tukio saa 4 asubuhi, Zaituni alimtuma mwanaye nyumbani kwake na kumuomba aende kwake (Zaituni).
“Nilipofika kwake aliniingiza ndani na kuniwekea kisu shingoni huku mwanaye akinirekodi na simu yake, akaniuliza nimetembea mara ngapi na mumewe!

“Alitaka kujua pia amenihonga shilingi ngapi, kwa hofu ya kuchinjwa nilikubali kwamba nilitembea naye mara moja na alinipa shilingi elfu tano. “Baada ya kusema hivyo akaniachia, nikarudi nyumbani.
Saa kumi aliniita tena, nilipofika nikamkuta yuko na mumewe na watoto wao, akaniuliza unamjua huyu? Nikamwambia simjui, akatoa simu na kufungua mahojiano, mumewe alipojaribu kumpora, akamchanja na wembe.
Mtuhumiwa akihojiwa.
“Ghafla akahamia kwangu na kuanza kunichanja kwa wembe huku nikipiga kelele na akanivua nguo kisha akanitoa nje na kunipeleka kwangu nikiwa na nguo ya ndani tu,” alisema Rehama.              

Akizungumza na paparazi diwani wa kata hiyo, Lydia Mbihaji alisema tangu aanze kuongoza watu hajawahi kukutana na tukio kama hilo ambalo aliliita ni la kinyama.
Tayari Rehema amelifikisha sakata hilo polisi na Zaituni alikamatwa na kuwekewa dhamana na mumewe akisubiri kuburuzwa mahakamani wakati wowote.
Baada ya kudhaminiwa, paparazi aliwashuhudia Zaituni na mumewe wakizungumza na Rehema ambapo inadaiwa wanataka ipatikane suluhu kabla kesi haijaanza kuunguruma mahakamani.

Comments

Popular posts from this blog