KIJANA ALIKUFA AIBUKA AWA MSUKULE POLISI WAPIGWA BUTWAA

Kijana Kenedy Onyango Augustine aliyedaiwa kupotea kimiujiza amerudi nyumbani akiwa hai baada ya kudaiwa kuwa alikuwa amechukuliwa msukule.

KIJANA Kenedy Onyango Augustine (22),  mkazi wa Kitongoji cha Nyambogo Shuleni, Kata ya Kitembe wilayani Rorya mkoani Mara aliyepotea kimiujiza amerudi nyumbani akiwa hai baada ya kudaiwa kuwa alikuwa amechukuliwa msukule.Baba mzazi wa kijana huyo, Augustine Oyoo alisema kuwa kijana wake alipotea katika mazingira ya kutatanisha wakati alipokuwa anakwenda kulala nyumbani kwa baba yake mdogo, Raubeni Oyoo kijijini hapo.‘’Kijana wangu aliondoka saa tatu usiku Juni 3, mwaka huu baada ya kula chakula cha usiku na kwenda kulala kwa baba yake mdogo alikokuwa akilala.“Ajabu hakufika, asubuhi tulianza kumsaka bila mafanikio ndipo tulipochukua hatua za kumtafuta kwa majirani lakini jitihada hizo hazikuzaa matunda ambapo walituambia kuwa hawakumuona,’’ alisema Augustine.  Aliongeza kuwa, baada ya kushindwa kumpata walitoa taarifa ofisi ya serikali ya kijiji na msako ulifanywa lakini kijana wake hakupatikana.

“Juni 6, mwaka huu usiku wa manane, tulimkuta kijana wangu akiwa amesimama nje ya nyumba yetu huku kapakwa matope mwili mzima.
“Tulimsemesha akawa haongei jambo ambalo lilitushitua sana tukaamua kwenda kwa Mwenyekiti wa Kitongoji, Michael Owino kutoa taarifa,” alisema mzazi huyo.
Alisema anaamini mtoto wake alifanywa msukule na jitihada zinafanywa na wazee wa kimila kuhakikisha watuhumiwa wanapatikana na ikishindikana atachanjiwa dawa mwilini mwake kurudisha fahamu pamoja na kujitambua ili aweze kuongea.
Michael Owino ambaye ni mwenyekiti wa kitongoji alikiri kupokea taarifa ya tukio hilo na kuongeza kuwa alimshauri baba wa mtoto kupiga yowe ili wananchi wakusanyike kwa msaada zaidi ambapo alifanya hivyo na kijiji kikazizima kutokana na tukio hilo.
Diwani wa kata hiyo, Thomas Patrick Lisa alisema kuwa tukio hilo tangu aingie madarakani ni la nane ambapo watu wengine walipatikana wakiwa wamechinjwa, hivyo kuhusishwa na ushirikina.

Comments

Popular posts from this blog