HAKIMU IRINGA AFUMANIWA AKIVUNJA AMRI YA SITA NA MKE WA MTU NDANI YA GARI


KASHFA  kubwa  idara ya mahakama  Iringa ni  baada ya  hakimu mmoja  wa mahakama mjini hapa  kufumaniwa ndani ya gari ya mwanamke ambae ni mke wa mpiga  picha mmoja maarufu mjini hapa akivunja amri ya  sita ndani ya gari  nje ya ofisi ya mahakama  ya Mwanzo  bomani na jirani na ofisi ya mkuu wa  wilaya ya Iringa.
Tukio  hilo  la aibu  limetokea usiku wa jana ambapo hakimu  huyo ambae anadaiwa  kuongoza kwa  michepuko na wake  za  watu  alifumwa na njemba  lenye mke akiendelea  kufungua kurasa za mama huyo ambae pia ni mwalimu wa  shule moja za kimataifa katika barabara ya Iringa-Dodoma
Mwandishi wetu alielezwa  kuwa mpiga picha  huyo maarufu mjini hapa kwa muda amekuwa na mgogoro wa ndoa na mkewe  huyo kutokana na mwanamke  kuendekeza  michepuko na wanaume  tofauti  tofauti akiwemo hata  paroko .
Kutokana na hali  hiyo jembe hilo liliamua kufikisha  suala hilo mbele ya  pirato kwa kutoka ndoa  hiyo ivunjjike na mahakama  hiyo ya mwanzo inadaiwa kuhukumu kimagumashi na hivyo jemba hilo kuamua  kusonga  mbele  zaidi na kesi hiyo kuwa mikononi mwa hakimu  huyo aliyefumwa akivunja amri ya sita ndani ya gari.
Hakimu  huyo ambae jina lake  linaanzia na herufi A baada ya  kufumaniwa alilazimika  kuendesha gari hilo kwa mwendo kasi kukwepa kichapo huku wakiwa hawajajisitili vema kutokana na nguo  zao kuvua ,kabla ya jemba lenye mke kufukuza kwa  boda boda na kuungwa mkono na waendesha  boda boda ambao  walifanikiwa  kumkamata  hakimu  huyo na mama mke wa mtu na kuwapa kichapo kiasi  cha hakimu huyo.
Hata  hivyo  mbali ya  kukutwa na mke wa mtu  hakimu  huyo alikimbilia  polisi  kufungua kesi ya kimagumashi  kuwa  eti ameibiwa pesa  shilingili laki  mbili .Wake  za watu ni  sumu ACHA MICHEPUKO BAKI NJIA KUU OGOPA  UKIMWI.
CHANZO:FANCIS GODWIN

Comments

Popular posts from this blog