LIGI KUU TANZANIA BARA :SIMBA YANGA ZACHAPWA

Yanga yafa Mkwakwani, Azam yanusa ubingwa

Yanga
Azam
KLABU Ya Azam imejiweka katika mazingira mazuri ya kutwaa taji la Ligi Kuu Tanzania Bara kwa mara ya kwanza baada ya jioni hii kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Simba, huku Yanga ikifa Mkwakwani.
Yanga ilikumbana na kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Mgambo JKT na kutoa nafasi kubwa kwa Azam kunyakua taji hilo kama itashinda mechi mbili kati ya tatu ilizosalia katika ligi kabla ya msimu kuisha.
Mabao ya Mcha Khamis 'Vialli' na John Bocco 'Adebayor' kwa kila kipindi yalitosha kuiwezesha Azam kuendeleza rekodi ya kutopoteza mechi kwa msimu huu na kufikisha pointi 53.
Bao la Simba lililokuwa la kusawazisha lilifungwa kwa kichwa na beki wake wa kati, Joseph Owino dakika chache kabla ya mapumziko.
Nako jijini Tanga bao la mapema la mshambuliaji mkali, Fully Maganga na jingine la mkwaju wa penati wa Malimi Basungu lililotosha kuizamisha Yanga kwenye uwanja wa Mkwakwani, bila kutarajiwa.
Yanga waliokuwa na matumaini makubwa kuibuka na ushindi dhidi ya 'vibonde' hao, walishindwa kuamini walipojikuta wakitafuta bao la kusawazisha licha ya Mgambo kucheza pungufu uwanjani.
Bao la Yanga la kufutia machozi lililokuwa la kusawazisha lilifungwa kwa mkwaju wa penati na Nadir Haroub 'Cannavaro'.

Comments

Popular posts from this blog