HATARI...!! MREMBO HUYU KAAMBUKIZA UKIMWI WATU 324 NA BADO ANAENDELEA....!!! SOMA HAPA UJUE USIJE UKANASA

  
 Jamani tubaki njia kuu!!! demu mmoja nchini kenya ameripotiwa kutembea na wanaume zaidi ya 300 wakati anajua kabisa ni muathirika wa ukimwi.
 Demu huyo aliamua kuchukua uamuzi huo mgumu kama njia ya kulipiza kisasi kwa wanaume baada ya yeye kufanya mapenzi yasiyo salama na mwanaume yaliyopelekea kuambukizwa ukimwi.
 
Mwanafunzi huyu kutoka Karabak University katika jiji la Nakuru  aliamua kufunguka kupitia facebook na kusema “nimesikia watu mkisambaza kashfa. Mimi nina kashfa kubwa zaidi nataka kuisema.” gazeti la daily post nchini kenya liliripoti.
Mwanafunzi huyu aliliambia gazeti la daily post la kenya kwamba ana miaka 19 tu kwasasa, na alikua ni bikira mpaka siku alipoenda club usiku na watu wa miaka ya juu hapo chuoni kwake. Alipoamka aligundua mmoja wa watu hao alifanya nae mapenzi bila ya yeye kujua sababu alikua amelewa kupita kiasi.


“tarehe 22 september ni siku ambayo sitakuja kuisahahu” demu huyu alisema. Alisema walipotoka club na kwenda kusherekea nyumbani kijana anayeitwa Javan alifanya nae mapenzi bila yeye kujua.

 
“nilimuuliza kama alitumia kondom, akasema ndio , sema nilivyoenda kuoga niliona shahawa zake ndipo nilipogundua ulikua ni uongo. nilitamani kujiu kwa kuhofia mimba na ukimwi juu”
Alipogundua ameathirika binti huyu alimueleza Javan japokuwa jamaa mwenyewe alimwambia kwamba hupo safi na hajaathirika.

 
“Nilikua nina mawazo mengi sana. Nikanywa pombe kupitiliza , nilifikia hatua nikanunua sumu, uchungu ulikua mkubwa sana.Nitaiambia nini jamii inayonizunguka ? Nimewaangusha wazazi wangu, nikakata tamaa ya kuishi duniani na kutamani kukatisha maisha yangu. Future yangu imeshaharibiwa.nikasema kunanjia mtu inabidi alipe machungu haya.” alilielezea dada huyu.


Baada ya ushauri kutoka kwa watu mbalimbali basi msichana huyu alinyanyuka na kuanza maisha mapya . “nilikubaliana na hali niliyokua nayo na kujiwekea nadhiri ya kuwatesa  wanaume watakaojileta mbele yangu ”


“Najua mimi ni mtu ninayevutia na wanaume kibao wananifukuzia kushoto , kulia. Nikazika upande wangu mzuri ndipo hapo nilipogeukia upande mbaya. Kusudio langu lilikua kuambukiza ukimwi wanaume wengi kadiri inavyowezekana”


Mwanafunzi huyu amesema kwamba ameweka list ya wanaume aliowaambukiza ukimwi na ataitoa siku atakayozikwa. “Najua sina cha kufanya tena hapa duniani zaidi ya kusubiri kifo changu lakini kabla sijaenda kaburini wanaume wengi watanielewa”
Dada huyu amesema amewaambukiza ukimwi wanaume 324, 156 wakiwa ni wanafunzi wa Kabarak University alipokua anasoma.Waliobaki ni wanaume walioolewa, ma-lectures , ma-lawyers , watu maarufu na wanasiasa.  Amesema Kusudio lake ni kuambukiza wanaume 2000 katika nchi za Afrika Mashariki. Gazeti la Kenyan Daily Post liliripoti.
“siku haipiti bila kufanya mapenzi. Wakiwa wengi ni watu wanne kwa siku. ” mrembo huyu aliendelea kufunguka.

 
“Hakuna kitu kitakachonizuia mimi kutimiza malengo yangu kwa kuendelea kulala na wanaume.Huwezi kujua inawezekana umeshalala na mimi, au kama sio wewe ni kaka yako , au mme wako , au rafiki yako, au baba yako tayari ameshalala na mimi”
“siku yako itafika. wewe mwanaume umeharibu maisha yangu sasa ni wakati na mimi niharibu maisha yako” alimalizia mrembo huyu.

 
Gazeti la Kenyan Daily Post lilisema halitataja jina la msichana huyu japokua waliweka picha zake kutoka kwenye ukurasa wake wa facebook.

Comments

Popular posts from this blog