NIMEKUFA NIMEOZA KWA BABA MWENYE NYUMBA WANGU

..NIMEJIPITISHA NA KUJIBALAGUZA LAKINI WAPI.. Ndugu  zangu, naombeni  nisieleke  vibaya.. Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 26. Nina mwaka wa kwanza tangu nianze kujitegemea mara baada ya kumaliza shule. Nimepanga kwenye nyumba moja iliyoko  maeneo ya  Mbezi.


Tatizo langu ni kwamba nimetokea kumpenda  sana  baba mwenye nyumba wangu ambaye ana watoto na familia. Kila nikijibaraguza siwezi. 

Nimefanya  kila  mbinu  kuzificha  hisia  zangu  lakini  nimeshindwa.Kimsingi simpendi mwanamume mwingine zaidi yake.


Nisaidie kuniepusha na mtihani huu  mgumu.Asanteni
Anna 
TUPE MAONI YAKO

Comments

Popular posts from this blog