HAWEZI KUKUFANYIA KILA KITU MPENZI WAKO, RIDHIKA!!

HAPA kwenye Love & Life ni mahali sahihi kabisa pa kupanuana mawazo kuhusu maisha na mapenzi. .


Si rahisi akakupa kila kitu, ridhika naye kwa kuwa moyoni umewekeza upendo wako. Vipengele vifuatavyo, vinafafanua zaidi.


HAKUNA RUFAA
Kwanza kabisa unatakiwa kufahamu kwamba, hakuna rufaa katika ndoa. Ukishaingia umeingia. Ni vizuri kuwa mtulivu na kuangalia zaidi mambo ya msingi.


Achana na fikra mbaya kwa mwenzako, wekeza upendo wako kwake. Mwamini na ishi naye kwa akili huku ukijaribu kumshauri mambo mbalimbali ya maisha yenu.


FURAHA YA NDOA
Yapo mambo mengi ya muhimu kwenye ndoa, lakini jambo kubwa na la msingi zaidi ni pamoja na tendo la ndoa. Lazima wanandoa wawe na uhakika wa kupata tendo la ndoa.

Tendo lenyewe linatakiwa kufanyika vizuri na kwa usahihi. Siyo harakaharaka bila ubunifu. Kufanya hivyo ni kuacha mianya ya mmoja wenu kufikiria kutoka nje ya ndoa.


FAMILIA
Majukumu ya familia ni kati ya mambo yanayozidisha furaha ya ndoa. Kama wanandoa wanakuwa makini kuhakikisha familia inakuwa yenye furaha ni jambo zuri.


Lazima watoto wapatiwe elimu bora, uhakika wa lishe, malazi na mambo mengine kama hayo bila kusahau malezi mazuri ya kiimani.


MIPANGO YA BAADAYE
Maisha ni mipango, hamuwezi kufikiria sterehe tena kama ilivyokuwa kwenye uchumba. Kwenye muunganiko wa ndoa kuna suala la maendeleo na mipango ya baadaye.

Hapo mnatakiwa kuwaweka watoto wenu mbele, maana lazima wawe na akiba yao ambayo mtawaachia. Lazima mfikirie kuhusu rasilimali kwa ajili yao.


KUJALIANA
Kila mmoja anaweza kukutana na changamoto kwa wakati wake. Kuna suala la matatizo kazini au msongo wa mawazo. Majukumu ya familia ya upande mmoja au ndugu wa mwenzako.

Mambo kama hayo mkishirikiana kuyatatua huongeza mapenzi ya dhati. Kwa mfano, mmoja wenu anaweza kuugua. Ni jambo zuri sasa kuwa karibu naye na kumpa furaha ili ajione yupo na chaguo lililo kamili.

Maisha ni zaidi ya starehe za kawaida. Majukumu ya familia ni muhimu zaidi kuliko yale mahaba ya mwanzo. Huu ni ukweli ambao wanandoa wengi (hasa wanawake) wanaukimbia.

Comments

Popular posts from this blog