Ridhiwani Kikwete alaani siasa za Chuki n Ukanda zilizowatoa madarakani Zitto Kabwe na Dr. Kitila Mkumbo.


Baadhi  ya watu maarufu  nchini akiwemo  mtoto wa Rais Kikwete, Ridhiwan wamezipokea taarifa za kuvuliwa wadhifa 

wa unaibu Katibu Mkuu wa CHADEMA kwa Zitto Kabwe kwa mitazamo tofauti.
Zitto alivuliwa uongozi wa Naibu Katibu Mkuu Taifa na Naibu Kiongozi 

wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho.

Haya  ni maoni  ya  Ridhiwani  Kikwete  aliyoiweka  katika ukurasa  wake  wa  facebook na  twitter kuhusiana  na  sakata  hilo:

Naendelea kujifunza matunda ya Siasa za Chuki na Ukanda zinavyoumiza 

siasa za Tanzania. Mungu anatuasa kupitia vitabu vitakatifu kuwa ” ili 
kuepusha balaa dogo kutokea, basi liwe balaa kubwa zaidi ya hilo.”. 
Imani kuwa aliloandika limetimia…




  
Zitto Kabwe pamoja na Dk Kitila Mkumbo watakutana na wahariri na waandishi wa habari  LEO Jumapili  kuzungumzia hatua hiyo.


Comments

Popular posts from this blog