Tido afiwa na mama yake mzazi

tido 3a9c5
Mama mzazi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), Tido Mhando, Jessie (85), amefariki dunia  Chang'ombe jijini Dar es Salaam kwa ugonjwa wa moyo.
Akizungumza jana jioni, Tido alisema mama yake ( alifariki baada ya hali kubadilika ghafla).
"Alikuwa na matatizo ya moyo kwa siku nyingi, lakini hali ilibadilika ghafla, akafariki akiwa nyumbani," alisema.
Tido alisema taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwa marehemu Chang'ombe, karibu na Klabu ya Sigara. "Tunafanya maandalizi, taratibu zinasubiri watoto wa marehemu waliopo Uingereza, Marekani na Australia, mwili utasafirishwa Tanga kwa maziko."
Ameacha watoto wanane, enzi ya uhai wake alifundisha Shule za Msingi Mgulani, Kibasila za Dar es Salaam. Nyingine ni katika mikoa ya Tanga, Dodoma, Morogoro, Iringa, Arusha na Mwanza.CHANZO MWANANCHI
phars blog tunapenda toa pole kwa familia nzima, Bwana ametoa na bwana ametwahaa,jina la bwa lihimidiwe

Comments

Popular posts from this blog