SOLLY MAHLANGU ‘OBRIGADO’ KUOMBELEZA KIFO CHA MANDELA UWANJA WA TAIFA

solly2Na Makuburi Ally
WAKATI siku za Tamasha la Krismasi zikikaribia, Muimbaji mahiri  anayeshika kasi katika anga la muziki wa Injili barani Afrika, Solly Mahlangu anatarajia kuombeleza   kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Nelson Mandela  anayetarajia kuzikwa keshokutwa kijijini Qunu nchini humo. 
Baadhi ya waumini watajiuliza maswali mengi kwamba baada ya kifo cha Mandela labda muimbaji huyo hatoweza kushiriki katika Tamasha hilo la kumtukuza na kumuimbia Mungu, lakini ukweli ni kwamba wamtarajie muimbaji huyo ambaye ataimba baadhi ya nyimbo zake kwa lugha ya Kiswahili.  
Kwa mujibu wa Mkurugenzi  wa Kampuni ya Msama Promotions ambao ni waandaaji wa Tamasha hilo, Alex Msama, muimbaji huyo  ni mmoja wa waimbaji kutoka nje ya Tanzania ambao watashiriki, hivyo waumini watarajie kumuona jukwaani akifikisha neno la Mungu kwa njia ya nyimbo.   
“Ni muimbaji ambaye anashika kasi katika anga ya muziki wa injili barani Afrika ambaye pia anamudu kuimba Kiswahili kizuri kwa  baadhi ya nyimbo zake, hivyo  anafaa zaidi kwenye tamasha la kumtukuza Mungu,” alisema Msama.
Msama anatoa wito kwa waumini kujiandaa na Tamasha hilo ambalo litakuwa na viingilio vya shilingi 2000 kwa watoto, 5000 kwa viti vya kawaida, VIP B shilingi 10,000 na VIP A shilingi 20,000.
Msama anasema kwa mikoani viingilio vitakuwa ni shilingi  5000  kwa  wakubwa  na watoto shilingi 2000.
Alizaliwa miaka 40 iliyopita na aliingia kwenye muziki wa kulipwa miaka minne iliyopita ambaye ameutangaza vilivyo muziki wa injili na kuuweka katika ramani ya muziki wa kumtukuza Mungu nchini Afrika Kusini.
Mbali ya kuwa maarufu katika nyimbo za injili nchini humo ni Mchungaji  ambaye ana uwezo wa kufanikisha muziki wa injili na kanisa lake ambalo ni Word Praise Christian Centre Intenational lililoko Tembisa.
Muimbaji huyo mwenye utajiri wa tuzo mwaka  2009 alipata tuzo ya albam bora ya SABC Gospel Crown, albamu hiyo iliyokuwa kwenye mfumo wa DVD  aliuza kopi 15,000 na CD zaidi ya 20,0000.
Mahlangu kabla ya kuja Tanzania kwenye Tamasha la Krismas hivi karibuni ametokea Harare Zimbabwe ambako alipeleka wimbo wake wa Kiswahili wa ‘Mwamba Mwamba’  ambapo kwenye tamasha hilo aliimba na muimbaji nguli Afrika Oliver Mutukudzi.
Mahlangu  alikuwa  na waimbaji wake wanne ambao wanalitawala vilivyo jukwaa ambao ni Sebastian Magacha, Mathias Mhere, the Charambas na Shiloh.
Mahlangu  amefanikiwa kupata tuzo  nne Afrika Kusini  na moja  Uingereza ambapo tuzo hizo alizipata mwaka 2012.
Mahlangu Obrigado anakuja Tanzania na msafara wa watu 14 ambaye atatoa zawadi ya Krismas kwa watanzania kwa kuimbva nyimbo 14 mfululizo, zikiwemo nyimbo za Kiswahili kama Mwamba mwamba na Eee Baba  ambazo zitafikisha ujumbe wa neno la Mungu kupitia uimbaji katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Krismas litakalofanyika hapa nchini katika mikoa mitano, litawakutanisha waimbaji kutoka nje ya Tanzania ambao ni pamoja na Liliane Kabaganza (Rwanda), Solomon Mukubwa (Kenya), Ephraim Sekeleti (Zambia) na Solly Mahlangu (Afrika Kusini).
Tamasha hilo ambalo litaanzia uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam (Desemba 25), Morogoro ( Desemba 26), Tanga ( Desemba 28), Arusha (Desemba 29) na Dodoma ( Januari 1 mwaka 2014).
 Waimbaji waliothibitisha kushiriki katika tamasha hilo ni pamoja na Obrogado, Liliane Kabaganza (Rwanda), Solomon Mukubwa (Kenya) na Eiphraim Sekeleti (Zambia) huku kwa waimbaji wa Tanzania ni pamoja na Rose Muhando, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Edson Mwasabwite, John Lissu na New Life Band. 
ya Mbarali ilitumiwa fedha kuliko kiwango kilichoidhinishwa na Bunge na kwamba
suala la halmashauri mbili za Tanga kupewa zaidi ya Sh2 bilioni haikuwa sahihi bali yalikuwa ni makosa ya Mkaguzi Mkuu wa Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).
Kuhusu ufisadi wa zaidi ya Sh600 milioni zilizotolewa na wafadhili kwa ajili ya mpango wa maboresho ya Serikali za Mitaa, alisema haamini kama maneno yaliyonukuliwa na vyombo vya habari kuhusu fedha hizo yalisemwa na wafadhili.
Wafadhili wa mradi huo walinukuliwa wakilalamikia ufisadi huo na kudai kwa sasa hawana la kufanya na wanamwachia Rais, huku wakieleza kushangazwa na Rais kuteua watu dhaifu kuendesha wizara nyeti kama Tamisemi.
Kuhusu hilo, Ghasia alisema hadhani maneno hayo ni ya wafadhili akisema ni majungu, ni maneno ya waandishi kwa sababu huwa wanatafuta mambo yanayogusa jambo fulani ili kuuza magazeti.Hata hivyo, Ghasia alikiri kwamba ulifanyika ukaguzi na yalibainika matumizi ambayo hayakufuata taratibu na kusisitiza kuwa fedha zilizotumika bila kufuata taratibu zilikuwa Sh444.8 milioni na siyo Sh600 milioni.
Alisema kuwa tuhuma kwamba anawalinda watuhumiwa wa ufisadi na kuwahamisha wale wanaotuhumiwa si za kweli kwani wizara imekuwa ikichukua hatua za kinidhamu dhidi ya watumishi hao na hata kuwafikisha kortini.
Alitolea mfano wa Halmashauri ya Kishapu ambayo watumishi 14 wamesimamishwa kazi na masuala yao hivi sasa yanashughulikiwa na ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na Ofisi ya Takukuru.
Pamoja na maelezo ya Waziri Ghasia, bado Mwenyekiti wa Kamati alisisitiza kuwapo matatizo makubwa
Tamisemi na ndipo alipowataka Ghasia na Manaibu wake kujipima wenyewe kama bado wanafaa kuongoza wizara hiyo nyeti.
Mwenyekiti huyo alisema si kweli kama alivyosema Waziri Ghasia kuwa hakuna mtandao wa ufisadi na
kusisitiza kuwa fedha zilizopelekwa jijini Tanga hazikurudishwa Hazina na badala yake zilitumiwa na Halmashauri hiyo.
Alisema kinachoonekana ni kwamba ulikuwapo mpango wa kuzipeleka fedha kwenye baadhi ya Halmashauri nje ya fedha zilizoidhinishwa lakini baadaye fedha hurudishwa kwa wanamtandao huo baada ya kutakatishwa.
Mwenyekiti huyo alisema Halmashauri zinazopelekewa fedha hizo zilizo nje ya bajeti, hupelekewa fedha hizo kwa malengo ya kuzitakatisha kisha kuzirejesha Hazina ambapo wahusika hunufaika nazo.
Ijumaa wakati akiwasilisha taarifa ya kamati, kamati hiyo iliilipua Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) ikiituhumu kuwa sehemu ya mtandao wa ufisadi serikalini.
Alisema bado kuna ubadhirifu, ufisadi na utovu wa nidhamu wa hali ya juu wa matumizi ya fedha za umma kutokana na Tamisemi kutosimamia au yenyewe kuhusika moja kwa moja na ufisadi huo.
Mfano wa mwaka 2011/2012 ambapo Sh1.6 bilioni zilitumika nje ya bajeti iliyoidhinishwa katika halmashauri 38 na Sh2.6 bilioni zilihamishwa kutoka akaunti moja kwenda nyingine bila kurudishwa.Kamati hiyo imebaini kwamba upo mtindo wa Serikali kutuma kwa Halmashauri kiasi kikubwa cha fedha kuliko kiasi cha fedha kilichoidhinishwa na Bunge katika fungu husika wakati wa upitishaji wa bajeti.
Kamati hiyo imetolea mfano wa Sh2 bilioni zilizotumwa Halmashauri ya Jiji la Tanga na Sh500 milioni zilizotumwa Halmashauri ya Mji wa Korogwe zikiwa zaidi ya kiasi kilichokuwa kimeidhinishwa na Bunge.
"Kitendo hiki ambacho kinafanyika kwa ushirikiano wa hali ya juu wa Hazina,Tamisemi na Halmashauri kinaashiria kuwapo mtandao wa kutisha wa kifisadi baina ya mamlaka hizo," alisema.
Kamati hiyo imeituhumu pia Tamisemi inayoongozwa na Waziri Hawa Ghasia, kuwahamisha haraka watumishi wanaotuhumiwa kufanya ubadhirifu kutoka halmashauri moja kwenda nyingine.
"Kamati imebaini kwamba Tamisemi imekuwa ikitumia mtindo huu kuwalinda watumishi mafisadi ndani ya halmashauri na kuifanya kamati iamini Tamisemi ni sehemu ya mtandao huu," imesema.
Mwenyekiti wa kamati hiyo alisema kwa makusudi mazima, Tamisemi imekuwa ikieneza saratani hiyo ya ufisadi kwenye halmashauri nyingi iwezekanavyo na kuitaka Serikali kuachana na mtindo huo.
Ubadhirifu Wakurugenzi 70
Itakumbukwa Agosti 19 mwaka huu, Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ilitoa taarifa yake baada ya kubaini kuwepo kwa mtandao wa ufisadi unaoshirikisha Wakurugenzi 70 wa Halmashauri mbalimbali hapa nchini ambao wanashirikiana na baadhi ya Watendaji wa Ofisi ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na Kitengo cha Hazina.
Baadhi ya halmashauri hizo ni pamoja na Wilaya ya Monduli, Arusha, Mwanza, Mbeya na Ilala.
Ilielezwa kuwa Tanzania Bara ina halmashauri 134, kwa hiyo ina maana zaidi ya nusu ya wakurugenzi wanajihusisha na mambo hayo.
"Baadhi ya wakurugenzi hao walihamishwa kwenye vituo vyao vya kazi kutokana na kashfa ya matumizi mabaya
ya fedha za Serikali, lakini bado wanajihusisha na mambo haya," alisema Mbarouk alipokuwa akiwasilisha taarifa yake kwa waandishi wa habari."Kuna zaidi ya Wakurugenzi 70 wako kwenye mtandao wa ufisadi kwa kushirikiana na watendaji wa Hazina na Tamisemi, jambo ambalo limesababisha halmashauri zao kupata hati chafu kwa miaka mitano mfululizo," alisema Mbarouk.
Aliongeza wakurugenzi hao wamekuwa wakishirikiana na wahasibu wao katika kutumia vibaya fedha za Serikali zinazotolewa kwa ajili ya kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika halmashauri zao.

Comments

Popular posts from this blog