PRODYUZA AMTUPIA KOMBORA WEMA

BAADA  ya kudaiwa kufanya ngono katika magari ya Kampuni ya Endless Fame inayoongozwa na Wema Issac Sepetu, Prodyuza, Rashid Mohammed ‘Chid Classic’ amefunguka na kusema chanzo cha yote ni mshahara  na ukuwadi ndani ya kampuni hiyo wala siyo uzinzi, Amani linakujuza.

Prodyuza Rashid Mohammed ‘Chid Classic’.
Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili, Chid amesema hajafukuzwa katika kampuni hiyo kama alivyodai mratibu wa kampuni hiyo, Petit Man bali ameondoka baada ya kuchoka  kufanya kazi bila ya kulipwa mshahara.
“Ni uongo kusema kwamba nimenaswa nikifanya uzinzi Coco Beach nikiwa ndani ya magari ya Wema, sijawahi hata siku moja kufanya hivyo kwani nina kwangu ambako nina uwezo wa kumwingiza mwanamke wakati wowote,” alisema.
Wema Isaac Sepetu.
“Tangu kampuni ianzishwe haijawahi kulipa mishahara unadhani nitakuwa na moyo wa kufanya kazi, sikwenda pale kufanya ukuwadi kama wengine, tena nawaomba wasiendelee kusema uongo kwani nina mengi nayajua ya Endless Fame,” aliongeza Chid.
Baada ya kusikia maelezo hayo, Amani lilimtafuta Wema bila ya mafanikio ndipo likaongea na meneja wake, Martin Kadinda.
“Nina wasiwasi na kauli za Chid kwanza tatizo siyo mshahara na hayo masuala ya ukuwadi ni uongo na uzushi, kama ni kweli kwa nini asiongee siku zote hadi lilipoibuka hili la kunaswa akifanya uzinzi kwenye gari?” alihoji Kadinda.
GPL

Comments

Popular posts from this blog