KATIKA HALI ISIYO YA KAWAIDA MTOTO AMFUMANIA MAMA YAKE AKIJIUZA JIJINI DAR...! PICHA ZA TUKIO HIZI HAPA



Na Issa Mnally na Richard Bukosi
SHABAASH!
Kijana aliyefahamika kwa jina moja la Hamis mkazi wa Tandale jijini Dar, hivi karibuni alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kumfuma mama yake mdogo akijiuza usiku.
Tukio hilo la kufedhehesha lilitokea usiku wa kuamkia juzi (Jumatano) maeneo ya Sinza Mapambano ambapo mapaparazi wetu walikuwa katika operesheni ya kuwasaka wanawake wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.

Wakiwa maeneo hayo, waandishi wetu walimuona kijana mmoja akiwa amejiinamia baada ya kumfuata na kumhoji kilichompata, alidai kuwa alipewa taarifa juu ya mzazi wake huyo aliyemtaja kwa jina la mama Husna kujiuza na siku hiyo alimuona akiwa kwenye mawindo.
“Jamani niacheni maana nilichoshuhudia kimeniumiza sana…mama yangu anafikia hatua ya kuja kijiuza huku?...amekosa nini…au ni huu ugumu wa maisha dah…?” Alisikika kijana huyo aliyekuwa akilia.
Katika kuthibitisha kile anachokizungumza, Hamis aliwaonesha waandishi wetu kundi la wanawake waliokuwa ‘sokoni’ na kuelekeza kuwa, aliyekuwa amevaa nguo ya mauamaua ndiye mama yake mdogo (angalia picha ukurasa wa 16).
Katika kupata utamu wa stori hiyo, mapaparazi wetu waliwavaa wanawake hao na kuwafotoa picha ambapo walitawanyika huku kila mmoja akishika njia yake.
Aidha, maelezo yaliyopatikana kutoka kwa shuhuda mmoja aliyedai kumfahamu vizuri mama Husna, alisema amekuwa akifika eneo hilo akiwa ameongozana na wapangaji wenzake ambao ni maarufu kwa biashara hiyo ya kujiuza.
Mbali na tukio hilo la aibu, waandishi wetu walitembelea mitaa ya Kinondoni, Posta maeneo ya Las Vegas, Ohio, Jolly Club na kwingineko jijini Dar na kushuhudia idadi kubwa ya wanawake wakijiuza.
Uchunguzi umebaini kuwa, biashara hiyo imekuwa akishamiri kadiri siku zinavyokwenda licha ya operesheni zinazofanywa na polisi huku ugumu wa maisha ukitajwa kuwa ndiyo chanzo.
Gazeti hili linawaomba wanawake wanaojihusisha na biashara hii haramu kuacha mara moja kwani ni hatari kwa maisha yao.

Comments

Popular posts from this blog