Hatimaye video ya Diamond yaanza kurushwa kwenye channel za kimataifa


d8
Lilikuwa swali kwamba inakuaje video iliyotumia ya gharama kubwa zaidi ya msanii wa bongoflava haipati airtime kwenye vituo vya kimataifa wakati video nyingine za wasanii wa muziki huu huu wanafanikiwa kupata airtime.
Jibu la swali hilo hatimaye limepatikana baada ya video ya My number one kuanza kuchezwa kwenye vituo maarufu duniani.
Diamond kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii aliwajulisha mashabiki wake kwamba wanaweza pia kuiona video ya My number one kwenye channel ya Trace na Sound City.
Kupitia Trace video hiyo imetambulishwa kama video mpya na kwenye Sound city imerushwa kwenye trending video request na hizi ni picha kutoka kwenye screen wakati video hiyo ikipata airtime kwa mara ya kwanza kwenye vituo hivi.d1
d2
d3
d6
d7
d4
d5

Comments

Popular posts from this blog