Jamal Malinzi ashinda urais wa TFF

HONGERA


Habari tulizozipata ni kwamba Jamal emil Malinzi amefanikiwa kushinda uchaguzi wa TFF kwa nafasi ya urais aliyokuwa anagombea dhidi ya Makamu wa zamani wa Rais wa TFF Athumani Nyamlani.

Uchaguzi huo, uliotawaliwa na kashkashi za hapa na pale, ulifanyika katika ukumbi wa NSSF WATER FRONT, Dar es salaam

Jamal Malinzi ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha soka cha mkoa wa Kagera ameshinda uchaguzi huo ikiwa ni mara yake ya pili kugombea baada ya kushindwa na Rais wa zamani wa TFF Leodgar Chillah tenga mwaka 2008.
 
TUPE MAONI YAKO MWANASPOT WETU, NA USISAHAU KULIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK/TWITTER


Comments

Popular posts from this blog