KINANA,NAPE WAZURU KABURI LA BABA WA TAIFA HAYATI JULIUS NYERERE

721_e8e65.jpg

Katibu Mkuu wa CChama Cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati akiweka shada la maua kwenye kaburi la Hayati. Mwalimu Julius K. Nyerere huku Nape Nnauye Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi akishuhudia tukio hilo.IMG_7745_ab5c6.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katikati akiwa katika picha ya pamoja na Andrew Nyerere Mtoto wa Kwanza wa Baba wa taifa Mwalimu Julius K. Nyerere wakati alipozuru kaburi la Mwaasisi huyo wa taifa la Tanzania Mwitongo, Butiama Nyumbani kwa mwalimu Mkoani Mara jana, Kinana alifanyakazi na Andrew Nyerere wakati wakilitumikia Jeshi la Ulinzi la wananchi la Tanzania (JWTZ), Katibu Mkuu huyo jana aliendelea na ziara yake katika wilaya ya Butiama katika kuimarisha chama na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, Kinana ataendelea na ziara yake katika Wilaya ya Serengeti leo. Kushoto ni Nape Nnayue Katibu wa (NEC) Itikadi Siasa na Uenezi.PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-BUTIAMA MARA
IMG_7746_457c1.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na Andrew Nyerere mara baada ya kuzuru Kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere Mwitongo Butiama jana
430_0a75e.jpg
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa tatu kutoka kulia akiongozwa na ndgu wa Mwalimu Mzee Jack Nyamwaga wakati akielekea kuweka shada la maua katika kaburi la Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius K. Nyerere jana mjini Butiama, Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mama Mabula
1015_e5c12.jpg
Wana habari nao wakishiriki kuweka mashada ya maua katika Kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere jana kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangwe Bw. John Bukuku, Said Mwishehe kutoka Jambo Leo Oktavian kutoka CCM Gerson Msigwa wa TBC, Ufo Saro wa ITV na Prosper Dereva wa CCM.

Comments

Popular posts from this blog