RAIS DKT. JAKAYA KIKWETE AFANYA MABADILIKO MAKATIBU WAKUU



NA MAGRETH   KINABO NA ELEUTERI MANGI – MAELEZO
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya uongozi katika ngazi za juu za utendaji wa Serikalini kwenye nafasi za makatibu wakuu na naibu makatibu wakuu katika wizara mbalimbali, ambapo  wapo waliohamishwa, wataopangiwa kazi nyingine na yumo anayestaafu.
 Kauli hiyo ilitolewa leo jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
“Rais amefanya mbadiliko haya kwa lengo kuu la kuimarisha utendaji wa kazi za Serikali  katika ngazi hizo za juu,”alisema Balozi Sefue.
 Mabadiliko yaliyofanywa kwa upande wa makatibu wa wakuu ni kama ifuatavyo; Dk. Florens Turuka amekuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Joyce Mapunjo Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki(awali alikuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda,Biashara na Masoko, Jumanne Sagini amekuwa Katibu  Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) awali alikuwa Naibu Katibu  Ofisi wa Waziri Mkuu – TAMISEMI.
Wengine ni Dk.  Servacius Likwalile amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Fedha,awali alikuwa Naibu Katibu Wizara ya Fedha,  Dk. Patrick Makungu amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, awali alikuwa  Naibu Katibu Mkuu katika wizara hiyo, Alphayo Kitanda amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, awali alikuwa Naibu Katibu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI.
Dk. Shaaban Mwinjaka amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi,awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko, Dk.Uledi Mussa  amekuwa Katibu Mkuu Wizara  ya Viwanda, Biashara na Masoko, awali alikuwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Profesa Sifuni Mchome amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya  Elimu na Mafunzo ya Ufundi, awali  alikuwa  Katibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania.
Wanaofuata ni Charles Pallangyo amekuwa Katibu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri,  Anna Maembe amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wizara hiyo, Sihaba  Nkinga amekuwa Katibu  Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo na  Sophia Kaduma amekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo.
 Balozi Sefue aliongeza kwamba Katibu Mkuu aliyepewa uhamisho ni  Peniel  Lyimo  ambaye anahamia Ofisi ya Rais – Ikulu  kwenye  ‘Presidential‘s Delivery Bureau’ kama Naibu Mtendaji Mkuu mwenye jukumu la kuanzisha na kuongoza Idara ya Mageuzi ya Kilimo mwanzoni alikuwa  Katibu Mkuu   Ofisi ya Waziri Mkuu.
Makatibu wakuu watakaopangiwa kazi nyingine ni  Sethi Kamuhanda aliyekuwa Katibu  Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Kijakazi Mtengwa aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto na  Injia Omari  Chambo  aliyekuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi.
 Kwa upande wa Makatibu wanaostaafu ni Patrick Rutabanzibwa ambaye alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi amestaafu kwa hiari.
Aidha Balozi Sefue alisema Rais Kikwete pia amefanya uteuzi wa naibu makatibu wakuu wapya na kuwapa uhamisho baadhi yao. 
 Alisema naibu makatibu wakuu wapya walioteuliwa ni  Angelina  Madete  Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais  Mazingira, Regina Kikuli  Naibu  Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Zuberi Sumataba Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI- anayeshughulikia  suala la elimu katika ngazi za Serikali za Mitaa , Edwin  Kiliba Naibu Katibu Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu -  TAMISEMI.
Wengine Deodatus Mtasiwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI ambaye atashughulikia  saula la afya  upande wa  Serikali za Mitaa, Dk. Yamungu Kayandabila amekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Adolf Mkenda Naibu Katibu Mkuu ya Fedha anayeshughulikia sera, Dorothy  Mwanyika Naibu Katibu Mkuu Wizara ya  Fedha anayeshughulikia Fedha za Nje na Madeni.
Rose Shelukindo Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Selassie  Mayunga Naibu Katibu Mkuu  Wizara ya Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Monica Mwamunyange Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Consolata Mgimba  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya  Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
 Naibu makatibu wakuu wengine ni Profesa Elisante ole Gabriel Laizer amekuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Armantius Msole Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
 Balozi Sefue aliwataja naibu makatibu wakuu waliopewa uhamisho kuwa ni John Mngondo ambaye amehamishiwa Wizara ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ametoka Wizara ya Uchukuzi katika nafasi hiyo, Selestine Gesimba  amehamishiwa  Wizara ya Maliasili na Utalii anatoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Injinia Ngosi Mwihava anahamia Wizara ya Nishati na Madini kutokea Ofisi ya Makamu wa Rais.
Wanaofuatia ni Maria Bilia amehamia Wizara ya Viwanda na Biashara kutoka Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi na Nuru  Milao anahamia  Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii.

Comments

Popular posts from this blog