KIJANA ATIWA MBARONI KWA KUFANYA MAPENZI NA NG'OMBE HUKO KILIMANJARO..... ANADAI KILA AKITONGOZA HUKATALIWA


JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro linamshikilia kijana mwenye umri wa miaka 15 mwanafunzi wa kidato cha pili katika shule ya sekondari Kelamfua iliyopo wilayani Rombo baada ya kukutwa akimwingilia ndama wa ng’ombe.


Akithibitisha, Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema tukio hilo lilitokea Agosti 3 mwaka huu saa 5:10 usiku nyumbani kwao Kelamfua.

Boaz alisema kuwa baba wa kijana huyo ndiyo aliyemfumania kwa kuwa alikuwa akimfuatilia kwa muda mrefu na ndipo alipomkamata.
 
Alisema kuwa kabla ya tukio hilo kijana huyo aliwahi kukutwa akifanya mapenzi na kuku na kuanzia hapo mzazi wake huyo akaanza kumfuatilia na hivyo kumkamata akifanya mapenzi na ng’ombe ambaye ni ndama.
 
Kamanda alisema kuwa baada ya kukamatwa kijana huyo alifikishwa kituo cha polisi na kuhojiwa ambapo alikiri kufanya kitendo hicho na kueleza kuwa amekuwa akitafuta wasichana bila mafanikio.


Aidha aliongeza kuwa kila msichana anayemtakia neno la mapenzi amekuwa akitaka fedha nyingi wakati yeye ni mwanafunzi hana uwezo wa kupata fedha.
 
Boaz alisema kuwa baba wa kijana huyo alishapata taarifa siku za nyuma kuhusiana na tabia ya kijana wake huyo na ndipo akaanza kumfuatilia na kwa sasa anashikiliwa na polisi uchunguzi zaidi ukiendelea.

Comments

Popular posts from this blog