WATOTO WAWILI WALIOKUWA WAMEPELEKWA "JANDONI" WAMEFARIKI WA AJALI YA MOTO HUKO LINDI


 Lindi- Watoto wawili wamekufa na mmoja wao kunusurika mauti, baada ya kuungua kwa moto uliosababishwa na kibatari kilichounguza nyasi za kijumba walichokuwemo.

Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga amesema ajali hiyo ilitokea mwishoni mwa wiki jana katika


mtaa wa Mitwero, katika kata ya Rasbura ya Manispaa ya Lindi na kuwataja waliokufa kuwa ni Maliki Kasimu (7) na na Selemani Fadhili (5) wakati aliyenusurika ni Juma Abdallah.

Mzinga amesema watoto hao watatu waliofika kwa mzee mmoja wa jadi, walikuwa wakijenga nyumba kwenye michezo yao wakati wakiwasubiri wenzao wafike siku za usoni, tayari kwa shughuli ya jando.

Siku ya tukio, moto huo ulishika nyasi zilizokuwa ndani ya shimo na kuwaka na kuwachoma Maliki na Selemani ambapo mwenzao, Juma alifanikiwa kukimbia na kujiokoa.

Wanakijiji wanasema mwangalizi wa jando hilo alikuwa mbali na eneo la tukio na hivyo kushindwa kuwaokoa

Comments

Popular posts from this blog