Posts

Afya ya Lema Mbaya Baada ya Kususia Chakula Mahabusu

Image
Godbless Lema. Afya ya Mbunge wa Arusha Mjini kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Godbless Lema imeripotiwa kuwa mbaya baada kususia kula chakula akiwa mahabusu tangu alipokamatwa juzi asubuhi. Lema alikamatwa na polisi akiwa nyumbani kwake juzi alfajiri na taarifa za kukamatwa kwake zilithibitishwa na Meya wa Jiji la Arusha, Calist Lazaro ambaye hata hivyo hakutaja sababu za kukamatwa kwa mbunge huyo. Imeelezwa kuwa mbunge huyo tangu akamatwe na polisi amegoma kula chakula hali iliyopelekea afya yake kuwa mbaya  na amefanya hivyo kwa sababu anaamini anaonewa na hata kukamatwa kwake kulikuwa ni kwa kumdhalilisha. Bwana Calist Lazaro amesema Lema amekataa kula hadi hapo atakapopelekwa mahakamani na kuliomba Jeshi la Polisi kumuachia kwani akipata madhara matatizo mapya yanaweza kuzuka.

TAZAMA HAFLA NZIMA YA RAIS DKT MAGUFULI KUHUDHURIA MISA YA JUBILEI YA DHAHABU (MIAKA 50) YA NDOA YA RAIS MSTAAFU BENJAMIN MKAPA NA ANNA MKAPA

Image
 Rais Dkt John Pombe Magufuli akilakiwa na  Paroko wa  Parokia ya Mtakatifu  Petro  Fr.  Stephano  Kaombwe  wakati akiwasili kuhudhuria   Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa ya Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016  "Maharusi"   Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakiingia kanisani  tayari kwa   Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016  "Maharusi"   Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakiingia kanisani  tayari kwa   Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agosti 27, 2016   Rais Mstaafu Mhe Benjamin Mkapa na Mama Anna Mkapa  wakiwa ta yari kwa   Misa ya Jubilei ya Dhahabu (miaka 50) ya ndoa yao katika kanisa la Mt. Petro jijini Dar es salaam leo Jumamosi Agos