Posts

Labda ulikua huyajui haya kuhusu hizi picha za Wema Sepetu na Ommy Dimpoz

Image
Zile picha za mahaba zilizosambaa kwenye mitandao zikimuonyesha Staa wa Bongo Fleva,Ommy Dimpoz na Wema Sepetu wakiwa kitandani zimezidi kuzua utata baada ya Ommy kusema hakujua alipigwa saa ngapi kwani hakuwa na fahamu bali aulizwe Wema.Ommy amezungumza na Uheard na Soudy Brown alisema kuwa hana maelezo zaidi ya kuzungumza zaidi ya kusema kuwa hajui ni muda upi zilipigwa picha hizo.Wiki hii picha hizo zilisambaa mitandaoni na kuzua hizo zilisambaa mitandaoni na kuzua maswali kuwa Ommy Dimpoz ameamua kujiweka kwa Wema baada ya kuachana na aliyekuwa mpenzi wake Diamond Platinum,lakini Aunty Ezekiel ambaye rafiki wa Wema alisema kuwa rafiki yake huyo alikwenda nchini Afrika Kusini kufanya video mpya ya ngoma ya Ommy. Hata hivyo picha nyingine zilisambaa Wema akiwa na aliyekuwa mume wa Zari wakiponda raha nchini humo na kuzua sintofahamu.

Mchumi wa Wizara ya Ardhi Afikishwa Mahakamani akituhumiwa Kumshika Matiti Mwanamke bila Ridhaa Yake

Image
MCHUMI wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Brown Kajange (42) amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo kujibu mashitaka mawili, likiwamo la shambulio la aibu kwa kumshika matiti mwanamke bila ridhaa yake. Karani wa Mahakama hiyo, Blanka Shao alidai mahakamani hapo mbele ya Hakimu Matrona Luanda kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Februari 16, mwaka huu katika eneo la kuuzia samaki la Feri Kivukoni wilaya ya Ilala. Shao alidai siku ya tukio saa 6 mchana katika eneo hilo, mshtakiwa alimshika matiti Queensia Fusi bila ridhaa yake huku akijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria. Alidai kuwa shtaka la pili, mshtakiwa alimpiga ngumi mlalamikaji katika jicho la kushoto na kusababisha maumivu makali katika sehemu hiyo. Mshtakiwa alikana mashtaka na Hakimu Luanda aliahirisha kesi hiyo hadi Machi 3, mwaka huu itakapotajwa. Mshtakiwa yupo nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ya kuwa na mdhamini mmoja mwenye barua kutoka serikali ya

CHADEMA YAWAPIGA "STOP" WANAOTAKA KUWANG'OA LEMA NA NASSARI

Image
Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe akiwa pamoja na Mbunge Joshua Nassari (kushoto) na Godbless Lema (kulia) katika moja ya mikutano ya chama hicho. Picha ya Maktaba  Chama cha Demokrasia na Maendeleo(chadema), mkoa wa Arusha “kimewapiga stop” wanachama wake, kutangaza nia ya kugombea ubunge katika majimbo matatu, yanayoshikiliwa na wabunge wa chama hicho,hadi hapo Bunge litakapovunjwa rasmi julai 2 mwaka huu. Majimbo hayo ni jimbo la Arusha mjini, mbunge wake, Godbless Lema, Jimbo la Arumeru Mashariki, mbunge Joshua Nassari na Jimbo la Karatu mbunge, Mchungaji Israel Natse ambapo tayari kuna    wanachama wa chama hicho, wameanza kutangaza nia   za kuwang’oa wabunge hao. Akizungumza na mwananchi leo, Katibu wa Chadema mkoa wa Arusha, Calist Lazaro alisema, maagizo anayoyatoa ni kutekeleza utaratibu ambao umetolewa na Kamati Kuu ya chama hicho,kuhusiana na uchaguzi mkuu ujao. “Naomba hapa ieleweke kuwa hatuzuwii mtu kugombea lakini tunataka

TEAM WEMA WAMKANA OMMY DIMPOZ, WEMA ANAYE MPENZI WAKE HANDSOME BOY

Image
Kubwa la Maadui Dougiemasta wa Instagram Ambaye kwa sasa ni Kiongozi wa Team Wema Sepetu amefunguka Kuhusu wale wanaotaka kujua kama wema ana mpenzi ama la kwa sasa baada ya kuachana na Mwanamuziki Diamond Platnumz...Haya ndio aliyoyasema: 'Kabari habari zenyu wananchi.kwa watu jana wameni uliza kwanini wema ajamuonesha mpenzi wake na wala ajaonesha wapi walikwenda kwenye valentine day banange kwani ukipiga picha halafu umepozi kama uko kwenye mahaba kwaiyo hapo inamaanisha kuwa mnapenda sana ? just picha aina maana yoyote. Valentine day sio lazima utoke out na mpenzi na vitu fulani una weza kukaa home na unayempenda basi maisha yanakwenda. Haya mapenzi ya mitandao yasiwasumbue akili zenu watu wanatumia pesa nyingi kuonesha wapizani wao kuwa wao wanapenda Nakumbukeni kuwa wema alisema mwaka huu anataka kujifunza yale makosa yako yote ,wema yupo bussy sana na mambo ya kikazi na biashara kuweni wavumilivu mtaona vitu vyake mwaka huu.Wema Sepetu anaye mupenzi wak

Ndesamburo njiapanda

Image
Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo    Ashikwa kigugumizi kugombea tena ubunge, CCM yatamba kumweka mgombea anayekubalika Moshi Mjini. Moshi. Mbunge wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo ana siku 72 za kuamua kugombea tena kiti hicho au la, ili kupisha wanachama wengine watangaze nia. Ndesamburo anaonekana yuko njiapanda kutoa uamuzi, huku taarifa zilizozagaa zinadai kwamba hagombei tena. Mbunge huyo ni miongoni mwa wabunge wakongwe wa upinzani, tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa mwaka 1991. Ndesamburo ambaye amekuwa mbunge kwa vipindi vitatu vya kuanzia mwaka 2000 hadi 2015, alipotafutwa jana kuzungumzia tetesi hizo alisema: “Wakati ukifika nitasema kama nagombea au sigombei.” Kutokana na kuzagaa kwa taarifa hizo, Chama cha Mapinduzi (CCM) kinadaiwa kusubiri kwa hamu tamko la Ndesamburo, ambaye amekisumbua chama hicho kwa miaka 15 mfululizo. Katibu wa Chadema, Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema alikiri kuwapo k

Mama aliyeporwa mtoto albino afanyiwa upasuaji wa kichwa

Image
Ester Jonas (30) ambaye ni mama mzazi wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi, Yohana Bahati akiwa amelazwa kwenye chumba cha uangalizi maalumu katika Hospitali ya Rufaa Bugando (BMC). Picha na Aidan Mhando Wabunge walia na Serikali kushindwa kulifanyia kazi tatizo la utekaji na mauaji yanayoendelea Geita/Dar. Mama wa mtoto mwenye ulemavu wa ngozi ambaye alitekwa juzi na watu wasiofahamika mkoani Geita, amefanyiwa upasuaji wa kichwa na jopo la madaktari wa Hospitali ya Rufaa ya Bugando (BMC) mjini Mwanza. Mama huyo aliyefahamika kwa jina la Ester Jonas (30), alilazimika kufanyiwa upasuaji huo baada ya kushambuliwa kwa kukatwa mapanga na watu hao ambao walimteka mtoto wake juzi akiwa amembeba mgongoni nyumbani kwake. Mkuu wa Kitengo cha dharura cha Hospitali ya Bugando, Dk Darick David alisema mama huyo alifikishwa hapo jana akiwa na hali mbaya kutokana na kuvuja damu nyingi. “Namkumbuka mwanangu Yohana Bahati,” hayo ni maneno aliyoyasema mama mzazi wa mtoto huyo a

Bunduki Waliyoporwa Polisi na 'Magaidi wa Tanga' Yapatikana ikiwa na Risasi 20......Ilikuwa Imefichwa ndani ya Mapango ya Amboni

Image
Polisi  mkoani Tanga imesema imefanikiwa kupata bunduki aina ya SMG, ikiwa na risasi 20 ndani ya mapango ya Majimoto katika eneo la Amboni, inayodaiwa ilikuwa ikitumiwa na wahalifu waliorushiana risasi na askari mwishoni mwa wiki.   Aidha, imesema inashikilia watu kadhaa akiwemo aliyesababisha kupatikana kwa bunduki hiyo. Baadhi ya watu wanaendelea kuhojiwa, kupata taarifa kwa lengo la kukamata waliopora silaha kwa askari na kurushiana risasi kwenye mapango hayo.   Kupatikana kwa silaha hiyo, kunafuatia msako maalumu uliodumu kwa siku nne sasa, uliolenga kusaka silaha na wahalifu wanaodaiwa kujificha ndani ya mapango ya mawe yaliyopo Amboni, nje kidogo ya mji wa Tanga.   Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja alitoa taarifa hiyo jana kwa waandishi wa habari mjini hapa.   Alisema mafanikio hayo, yametokana na subira ya wakazi wa Tanga na ushirikiano mkubwa wanaoendelea kuuonesha kwa Polisi inayoshirikiana na vikosi vin

Gadner alitongoza na kuwashika makalio wanawake mbele yangu – Lady Jaydee

Image
Wiki hii Lady Jaydee amewapa nafasi mashabiki wake kumuuliza maswali naye kuyajibu kupitia akaunti yake ya Instagram. Ameulizwa maswali mengi, na miongoni mwa maswali hayo ni la kuhusu ndoa yake na mtangazaji wa Radio E-FM Gadner G. Habash. Haya ni maswali na majibu kama alivyopost Instagram. Tunasikia umeachana na mume ni kweli au uzushi? JIBU : Hatuja achana niliamua kumuacha   Kwanini umeachana/umemuacha mume? JIBU : Nimemuacha kutokana na kuwa Ndoa inatakiwa iwe na maelewano, furaha, amani na upendo. .. ila kwa bahati mbaya vyote hivyo havikuwepo , sikuwa tayari kuendelea kuishi kwa maumivu huku niki pretend ili kuiridhisha jamii.    Huoni kama umejishushia heshma kuachana na mume? JIBU : Sioni hivyo, ila naona nilikuwa najishushia heshma zaidi kuishi na mume asie na heshma, anaeweza kutongoza na kushika wanawake makalio wakati mi niko jukwaani naimba. Kuwapa mademu magari yangu waendeshe na kuyagonga wakati niko safarini . Ukiachilia

'Magaidi wa Tanga' Watiwa Mbaroni.....Mwili wa Mwanajeshi wa JWTZ Aliyeuawa katika Mapigano hayo Waagwa

Image
Serikali imetoa taarifa rasmi kuhusu uhalifu uliotikisa mkoani Tanga, ikisema hali ni shwari na umma wa Watanzania upuuze taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zikitia hofu. Aidha, imesema  watu kadhaa wanashikiliwa wakihusishwa na uhalifu huo.   “Tunawashikilia ila mpaka sasa siwezi kukueleza idadi yao na kwamba ni wa kikundi cha ugaidi au la. Hao watu tunafanya nao mahojiano ili kuweza kuelewa kama wanahusika kwenye tukio hilo,”  alisema Kaimu Kamanda wa Polisi  wa Mkoa wa Tanga, Juma Ndaki.   Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari, Ndaki alisema hali katika kitongoji cha Majimoto, Amboni na mkoa wa Tanga kwa ujumla iko shwari. “Tunaendelea kufanya uchunguzi kubaini hao wahalifu pamoja na silaha zilizoibwa,” alisema.   “Tunaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano wao hasa wanapoona watu wenye majeraha au wanaowahisi kwamba ni wahalifu ili nasi tuweze kuwachunguza kama wanahusika kwenye tukio hili”, alisema.   Ingawa Kamanda hak

YAMOTO BAND LIVE KWA MARA YA KWANZA KWENYE JIJI LA LONDON

Image
  YAMOTO BAND   COMFIRMED  will performing all their major hits including NITAJUTA, NISEME, WAMBEA, NITAKUPWELEPWETA and many more @ The Royal Regency Banquet Hall, Sat 21 Feb 2015 From 8pm to 3:30am, there are limited VIP Tables available book yours now for ultimate VIP treatment or individual place your booking early to avoid disappointment. Table bookings please call 07405824696/ WhatsApp +447557304940 info@bongodeejays.com or jestinageorge@gmail.com Ukumbi wa Royal Regency ndio sehemu pekee ambayo utawaona YAMOTO BAND kwenye jiji la LONDON usiku wa 21. Feb 2015 Usiku wa tarehe 21 February 2015 The Royal Regency patakuwa hapatoshi. Kwa kuondosha usumbufu wahi ticket yako mapema  Kiingilio ni: £25 kwa Ticket ya kawaida £35 kwa VIP ticket Kama Unahitaji VIP table for 10 people piga simu  07405824696  kwa maelezo zaidi au tuma email kwenda: info@bongodeejays.com or jestinageorge@gmail.com YAMOTO BAND  will be  alongside supported artist such as Sultan King,

MUUZA MISHIKIKA AKAMATWA NA NYAMA YA PAKA NA KISHA KUSULUBIWA NA WATEJA WAKE

Image
Muuuza mishikaki maarufu Temeke stand ya mabasi anayejulikana kwa jina maarufu la Said mishikaki amekamatwa na nyama ya paka na kisha kusulubiwa na binadamu wenye hasira. Hivi mtu huruhusiwi kuwa na nyama ya paka

Masikini..Kijana Aingizwa Mochwari Akinizaniwa Amekufa

Image
Kijana mmoja, Omary Ramadhani, 28, (pichani) mkazi wa Sinza Madukani, Dar amenusurika kifo baada ya kupata ajali ya kugongwa na ‘Break Down’ alipokuwa akiendesha Bajaj katika makutano ya Barabara ya Sam Nujoma na Ali Hassan Mwinyi, Mwenge, jijini Dar es Salaam. Akizungumza kwa masikitiko, Omary alisema kuwa alipogongwa na gari hilo hakuweza kujitambua kwani hata wasamaria wema walivyomchukua na kumkimbiza katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, walijua alifariki dunia hivyo wakamuingiza moja kwa moja mochwari, lakini kwa bahati nzuri alitokea nesi mmoja aliyeshauri asiwekwe kwanza kwenye friji mpaka apimwe. Akiendelea kuzungumza kwa tabu kutokana na maumivu ambayo anayo, Omary alisema baada ya nesi huyo kumpima aligundua alikuwa akipumua kwa shida. Alisema hata ndugu zake walijua ameshafariki dunia kutokana na alivyokuwa, kwani alivunjika mgongo mara sita na mfupa wa mkono ulitoka nje na kupasuka kichwani jambo lililosababisha kuvuja damu nyingi. Al

ANGALIA KINACHOENDELEA TANGA

Image

Necessary Job Interview Preparations

Image
In the event when you are invited on a job interview, your thoughts become focused on preparing an outstanding presentation. Much like exams during your student days, job interviews are likely to toss you into a stressful state, but if you remain level-headed, chances for achieving success significantly improve. A word of advice, do not strain your mind too much if things go south, since a lot of people get jobs due to their connections, not their qualifications, in other words, you should not allow failure bring you down too much, just find out who got the job, and things may appear much clearer to you. Here are some good suggestions on how to get ready for an upcoming job interview, I am pretty convinced you will find them useful. Think about the Possible Scenario If this is your first job interview , you will find the following paragraph very useful. When you are on the job interview, here are some of the questions your potential employer might ask:      

AJINYONGA BAADA YA MATOKEO YAKE YA FORM 4 KUWA MABAYA.. MUANGALIE HAPA

Image
Imekuwa kawaida kila mwaka pale ambapo matokeo yanapotoka watu wengenge utalajia mambo mazuri ata yulealiye kuwa kilaza dalasani naye anaamini atafaulu tu ila matokeo yake mambo yanakuja kutokana na kile ulicho panda kama ulipanda mawe basin ni mawe unatakiwa kuvuna Kinachosikitisha Zaidi ni pale wanapo chukua hatua kama huyu Kijana mmoja ajulikanaye kwa jina John Maduhu wa KIjiji cha Pandagichiza, Wilaya ya Shinyanga vijijini kaamua kujinyonga baada ya matokeo ya kidato cha nne yaliyotoka jana kumjia vibaya, akiongea na mwandishi, kaka wa marehemu alisema kuwa baada ya matokeo kutoka, JOhn alitoweka nyumbani Mungu atusaidie na atusamehe kwa dhambi hizi. NINI MAONI YAKO NDUGU MSOMAJI NA MDAU WETU.?

GADNER G HABASH AWAULIZA MASHABIKI WAKE KUHUSU KUJIBU TUHUMA ZA MALAIKA

Image
Baada ya Mwanamuziki Lady Jay Dee Ambae alikuwa mke wa Gadner G Habash Kufunguka kisa cha kumuacha Habash  Hatimaye Gadner na Yeye amekuja na Hili Hapa Chini: Hivi ndivyo alivyoandika kwenye ukurasa wake wa Instagram: Valentine hii naishi kwa hisani ya Mungu Muumba, napendeza kwa hisani ya @robbyonefashion, nakula kwa hisani ya kazi @efm_93.7 Efm, natamba kwa hisani ya @majizzo, nna amani kwa hisani ya washkaji wangu @abdallah_gunda na @edbyamps na lavi davi kwa hisani ya #VJM. Ndugu zangu na jamaa zangu nawauliza nimjibu au nisimjibu huyo anayedhani yeye malaika anayekosewa yeye tu??

TASWIRA YA MSIBA WA BABA 'AKE DULLY SYKES HUKO KAWE BEACH JIJINI DAR!

Image
Mwanamuziki Dully Sykes akihojiwa na wanahabari (hawapo pichani) huko msibani Kawe Beach jijini Dar. Dully akilia kwa simanzi wakati akipewa pole na waombolezaji waliofika msibani Mbezi Beach, Dar leo mchana. Dully akipewa pole na baadhi ya waombolezaji waliofika msibani leo. Ebby Sykes enzi za uhai wake.  MAZISHI ya mwanamuziki mkongwe nchini ambaye ni baba mzazi wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Dully Sykes, Ebby Sykes yatafanyika leo saa 10 jioni katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam.  Mzee Sykes alifariki dunia jana mchana akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa vidonda miguuni vilivyopelekea kueneza sumu katika mwili wake na kumsababishia mauti.  Kwa mujibu wa Dully, Mzee Sykes alikuwa akisumbuliwa na vidonda hivyo vilivyoshindwa kupona kutokana na kuvuta sigara. Lakini mbali na hilo hakuwa na tatizo lingine lolote.  Mzee Sykes amefariki akiwa na umri wa miaka 62 al

ANGALIA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE

Image
Posted by RAHA ZA WALIMWENGU On Monday, February 16, 2015 0 comments    MATOKEO KIDATO CHA NNE 2014  BOFYA  HAPA MATOKEO QT 2014 BOFYA HAPA

CHEK DIAMOND NA ZARI WALIVYO KULA BATA SIKU YA VALENTINE HUKO ZANZIBAR

Image
Photos showing the hot couple in town Diamond Platnumz and Zari in Zanzibar, "She had never been to Zanzibar so i had to take her there to experience the beauty of Tanzania" said Diamond