Posts

MAMA WA MAPACHA BI. K' LYNE AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA REGINALD MENGI.

Image
Kumekuwepo na Minong'ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili.  Hongera Mmiliki  wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali  Jackline Ntuyabaliwe(K'lyne)  .... Hiyo ndo Tweet ya K'lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI

MAMA WA MAPACHAK' LYNE AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA REGINALD MENGI.

Image
Kumekuwepo na Minong'ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili.  Hongera Mmiliki  wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali  Jackline Ntuyabaliwe(K'lyne)  .... Hiyo ndo Tweet ya K'lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI
Image
K' LYNE AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA REGINALD MENGI Kumekuwepo na Minong'ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili.  Hongera Mmiliki  wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali  Jackline Ntuyabaliwe(K'lyne)  .... Hiyo ndo Tweet ya K'lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI

MABINTI WATOANA MANUNDU WAKIGOMBEA MWANAUME

Image
Warembo wawili, wakazi wa Sinza, Dar es Salaam ambao majina yao hayakupatikana, wamenaswa wakizichapa laivu wakidaiwa kugombea bwana. Tukio hilo la kujidhalilisha lilijiri katika baa maarufu ya Corner iliyopo Sinza-Afrikasana, Dar, majira ya asubuhi wakati watu wakiwa kwenye mishemishe za kuwahi kazini.   Katika tukio hilo, mmoja wa warembo hao alikuwa akilalamika kuwa kuna mwanaume walikubaliana kwenda kuvunja amri ya sita fastafasta ili awahi kazini lakini akazidiwa ujanja na shosti wake hivyo akataka kukomboa chake na ndipo alipotolewa manundu. Habari kutoka eneo la tukio zilieleza kuwa warembo hao walijikuta wakizichapa kavukavu wakimgombea mwanaume huyo aliyedaiwa kuwa ni mume wa mtu, mwenye ndoa changa.   Katika timbwili hilo lililojaza kadamnasi, wanaume walishuhudia sinema ya bure baada ya mmoja wa warembo hao kula kipigo kizito na kuvuliwa nguo ambapo alibaki wazi sehemu za makalio.

P- FUNK AWACHANA TENA CLOUDS FM....

Image
AELEZA JINSI MAREHEMU NGWEA ALIVYOGEUZWA NG'OMBE WA MAZIWA Kwa mara nyingine  tena P-Funk amezungumzia sababu anazodhani zilipelekea marehemu Ngwea kujiingiza kwenye madawa.  Producer huyo ameichana CloudsFM kwa kile anachokiona kama unyanyasaji kwa wasanii, na kwamba dhuluma za Clouds Fm ni moja wapo ya vitu vilivyosababisha maisha ya Ngwear yawe na muelekeo mbaya.   “Ngwair alikua kama ng’ombe wenu; mnamkamua tu maziwa.”  P funk Akizungumzia kuhusu kuikataza Clouds FM kupiga nyimbo za Bongo Records  zikiwemo wa Ngwea, P-Funk amesema: “Niko kwenye harakati za kuandaa barua ili nistopishe nyimbo zangu zote za Bongo Records, zisipigwe Clouds Fm.  Sababu kubwa ni uonevu wa haki miliki. Eti mnajiita  number one radio station??. Mnajidaganya .Kisaikolojia wasanii wote mmewateka.  Wote wanaona “bila kupeleka nyimbo zao Clouds hawatafanikiwa.” Mimi cha kwanza nataka kuonyesha mfumo mwingie kwamba bila nyinyi tutaweza. Cha pili mnaingi

MATOKEO MAPYA YA KIDATO CHA NNE, UFAULU WAPANDA KWA ASILIMIA 23....YAANGALIE HAPA.

Image
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa. Baraza la mitihani Tanzania NECTA limetangaza rasmi matokeo ya Kidato cha Nne 2012. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu.  Matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57.  Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.   Kwa matokeo hayo, watahiniwa wa mwaka 2012 watakuwa wamefanya vizuri kuliko wa mwaka 2011, ambao watahiniwa 225,126 sawa na asilimia 53.37 ya 349,390 waliofanya mtihani huo walifaulu. Matokeo ya awali yaliyotangazwa na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Uf

KIFO CHA NGWEA: LADY JAYDEE NAYE ASITISHA SHOW YAKE

Image
Mwanamuziki nguli wa muziki wa kizazi kipya nchini, mwanadada Judith Wambura Maarufu kama Lady Jaydee ametangaza kuahirisha shughuli ya maadhimisho ya miaka 13 tangu aanze muziki iliyokuwa imapangwa kufanyika Ijumaa hii ya Mei 31, 2013 katika mgahawa wake wa Nyumbani Lounge kupisha msiba wa kifo cha msanii Albert Robert Mangweha aliyeripotiwa kufariki nchini Afrika Kusini jana. Judith amesema hayo muda mfupi uliopita (saa 3:52 asubuhi) wakati akihojiwa katika kipindi cha Super Mix ya East Africa Radio na mtangazaji Zembwela.    Jaydee ameeeleza uamuzi wake wa kutitisha show hiyo kuwa unalenga kutoa nafasi kwa wafiwa wote na wadau wa tansnia ya muziki na wapenzi wa Mangwea kumaliza taratibu za kumsitiri kipenzi chao na kueleza kwamba tarehe nyingine ya shughuli hiyo itatangazwa baadae.   Tangu amekaribishwa studio, Judith Wambura alionekana kuwa na majonzi sana kiasi cha kushindwa kuongea mara kwa mara na kukatisha mazungumzo yake kutokana na kukabwa na ki

MWAKILISHI WA BIG BROTHER TANZANIA BI. FEZA AZIDI KUCHANJA MBUGA

Image
Kwa mujibu wa ripoti kutoka kwenye   mitandao  mbalimbali nchini Tanzania, mrembo huyu, mwanamuziki Feza Kessy, ndiye atakayeiwakilisha Tanzania katika Big Brother Africa 2013 (BBA “The Chase.” Well, hizi ni baadhi ya picha zake. Tunaenda vizuri, bahati inaonekana kutuangukia watanzania kwani mshiriki Feza jana ameukwaa ukuu wa kaya ama kwa lugha ya ki-big brother ‘Head of House’. Ilikuwaje? Baba mwenye nyumba, biggie, alitoa task ambayo washiriki walitakiwa kuelekea bustanini na kuchagua box, ambaye angechukua box la ushindi ndo huyo angekuwa mkuu wa kaya. Kama zali, bahati hiyo ilimuangika mrembo Feza. Washiriki wenzie akiwemo mtanzania Nando, walimkumbatia kwa furaha kama ishara ya kumpongeza. Iko hivi, ukichaguliwa kuwa mkuu wa kaya, unauwezo wa kumuokoa mtu ambaye anakuwa amependekezwa atoke katika wiki hiyo. Usipofanya hivyo basi wewe mwenyewe unawekwa kikaangoni. Feza alitumia nafasi hiyo kumuokoa Elikem ambaye ni mshiriki kutoka Ghana na

CHANZO CHA KIFO CHA MSANII ALBERT MANGWEA AKIWA UKO MADIBA....................

Image
Ngwea akiwa na msanii Mwenzake M to the P jana south africa. Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo.  Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear  na   M to the P  ambaye walikuwa room moja  wamekutwa wamezima   baada  ya  kuzidhisha  madawa  ya  kulevya... Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini. Akiongea na mwandishi wetu  muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka. Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka na  kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka n

R.I.P ALBERT MANGWEA

Image
Habari  zilizotufikia  ni  kwamba  msanii  Albert Mangwair  amefariki  dunia akiwa  Afrika  kusini Chanzo  cha  kifo  hicho  bado  hakijafahamika  lakini  taarifa  za  awali  zinadai  kuwa  msanii  huyo  hakuamka  tangu  alipolala . Kwa habari zaidi tutawajulisha kadri ya uwezo.   BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE  

MADAM RITHA WA BSS AELEZA JINSI ALIVYOPATA AJALI

Image
Kilichompata Madam Rita kinasikitisha! Ndivyo unavyoweza kusema ukibahatika kumuona the big boss wa Benchmark Production inayoratibu Shindano la Bongo Star Search , Rita Poulsen ‘Madam’ anayetembelea magongo baada ya kupata ajali mbaya ya gari. Akizungumza na mwandishi wetu baada ya kuwa kimya muda mrefu ikielezwa kuwa alipata ajali hiyo kitambo, Madam Rita alisema kuwa kwanza kabisa anamshukuru Mungu kwani anaamini kila kitu kinachotokea chini ya jua kina sababu yake na hata alipopata ajali hiyo alimshukuru kwa kutoka salama.  Kabla ya ajali Madam Rita aliendelea kueleza kuwa ajali hiyo aliipata katikati ya Jiji la Dar  na kusababisha kuvunjika kwa kifundo ‘enka’ cha mguu wa kulia hivyo kumsababishia kutembelea magongo baada ya hospitali kumuwekea ‘hogo’. “Namshukuru Mungu kwanza kwa kunitoa salama katika ile ajali japokuwa sijapona vizuri,” alisema Madam Rita. Mkurugenzi huyo aliendelea kueleza kuwa alipopata ajali hiyo alikimbizwa katika Hospita

BINTI ALIYETOROKEA UINGEREZA AKIMKWEPA MFALME MSWATI

Image
HUYU NDO BINTI ALIYETOROKEA UINGEREZA AKIKWEPA KUTOMASWA NA MFALME MSWATI Msichana mdogo ameomba hifadhi ya ukimbizi nchini Uingereza baada ya kukataa kwa dharau harakati za ndoa za wake wengi za Mfalme Mswati III wa Swaziland na kugoma kujiunga kwenye nyumba harimu ya wake 13. Tintswalo Ngobeni, mwenye umri wa miaka 22, alitimkia Uingereza kutoka taifa hilo la kusini mwa Afrika akiwa na umri wa chini ya miaka 18 baada ya kuvuta hisia za mfalme huyo milionea, mtawala maarufu mkandamizaji kwa maisha yake ya anasa. Ikiwa ni sehemu ya mila za Swazi, Mfalme Mswati III, mwenye umri wa miaka 45, anaruhusiwa kuchagua mke mpya kila mwaka.   Tintswalo, ambaye sasa anaishi mjini Birmingham, alikuwa na umri wa miaka 15 tu wakati Mfalme huyo alipofanya harakati zake baada kumuona kwenye jumba la kifalme la mke wake wa nne, LaNgangaza. Binti huyo alisema 'alitishika' pale alipogundua dhamira zake za ndoa. Aliongeza: "Alianza kunipigia simu k
Image
MSANII ELIZABETH 'LULU' MICHAEL KURUDI SHULE...!!! Elizabeth 'Lulu' Michael BAADA ya kupata dhamana msanii wa filamu Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu ajipanga kujiendeleza na masomo ili aweza kupambana na changamoto za maisha. Akizungumza na Maisha msanii wa filamu ambaye pia amekuwa ni mtu wa karibu  familia ya Lulu Mahfudh Hussein 'Dkt. Cheni' amebainisha kuwa Lulu yupo kwenye mchakato wa kurudi shule ili aweze kuendelea na masomo yake Alisema kuwa ingawa familia ina mikakati hiyo suala kubwa linalokwamisha kwa sasa ni kipato kwani familia yake haina uwezo wa kumlipia msanii huyo na badala yake anatakiwa Lulu kuanza kufanya kazi ili aweze kujikwamua kwa hilo Dkt. Cheni aliweka wazi kuwa kutokana na kipato cha familia ya msanii huyo hivyo anatakiwa kwa sasa aweze kufanya kazi ya filamu ili aweze kujimudu kama ilivyokuwa mwanzo na maisha yaendele "Hapo awali alikuwa na uwezo wa kuihudumia familia yake kwa njia ya

SIMBA YASEMA KUONDOKA KWA NGASA HASUMBUI

Image
Simba:Ngasa hatusumbui kichwa Share bookmark Print Email Rating   Na Jessca Nangawe  ( email the author ) Posted  Jumatano,Mei22  2013  saa 9:27 AM Kwa ufupi Mwanzoni mwa wiki hii, Ngassa alisaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga, klabu aliyoichezea kabla ya kujiunga na Azam FC na kisha kutua Simba alikocheza msimu mmoja uliomalizika wiki iliyopita  Baada ya siku mbili tu kupita tangu winga wa Simba, Mrisho Ngasa ajiunge Yanga, Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Aden Rage amesema kuondoka kwa mchezaji huyo hakuwasumbui hata kidogo. Mwanzoni mwa wiki hii, Ngassa alisaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Yanga, klabu aliyoichezea kabla ya kujiunga na Azam FC na kisha kutua Simba alikocheza msimu mmoja uliomalizika wiki iliyopita. Simba wanadai Ngassa alikuwa tayari amesaini mkataba wa miaka miwili kwao, kabla ya kusaidi wa Yanga jambo linalizua utata kwenye klabu hizo mbili

NDOA YA DIAMOND PLATINUM NA PENNY YANUKIA

Image
NDOA YA DIAMOND PLATNUMZ NA PENNY YANUKIA. Maharusi watarajiwa Dimaond Platnumz & VJ Penny Esma Abdul ambae ni dada yake mwimbaji staa wa Tanzania, Diamond Platnums, amesema wamejiandaa vizuri kwa ajili ya harusi ya Diamond ambae anatarajiwa kumuoa mtangazaji wa TV aitwae Penny. Esma ambae anaishi nyumba moja na kaka yake amesema, "Tumemkubali sana wifi yetu na tunampenda kwa sababu mtu yeyote mimi nitakaetambulishwa siwezi nikamkataa, manake nikimuingilia kwenye mapenzi yake na yeye ataniingilia kwenye mapenzi yangu." Huu ni mwezi wa tano toka Esma amjue wifi yake ambae ni Penny, anasema nyumbani amekubalika na mipango ya harusi inaandaliwa japo hajui ni lini itafanyika, manake hiyo ni siri kwa sasa. Dada yake Diamond aka wifi yake Penny Zaidi ya wiki tano zilizopita, Diamond aliongea na kusema ndoa yake imekaribia kufungwa na huyo mkewe mtarajiwa ambae ni mjamzito lakini pia akathibitisha kumnunulia gari la kutembelea aliloliagiza nch

MWILI WA HAYATI CHINUA ACHEBE ULIVYOWASILI NCHINI NIGERIA

Image
HIVI NDIVYO MWILI WA HAYATI CHINUA ACHEBE, ULIVYOWASILI NIGERIA In the early hours of Tuesday May 21st, 2013, the corpse of late Prof. Chinua Achebe arrives the Federal Capital Terrorist ( Abuja ) ahead of his burial on Thursday. See more photos of the late Chinua Achebe’s casket below.

MATUKIO YA VURUGU MTWARA

Image
NYUMBA YA MWANDISHI WA HABARI WA TBC YACHOMWA MOTO HUKU MABOMU YAKIRINDIMA HUKO MTWARA Hali imezidi kuwa mbaya katika Mji wa Mtwara na hivi punde watu wanaendelea kufanya uharibifu katika maeneo mbalimbali ya mji huo. Jengo moja ambalo linadaiwa kumilikuwa na CCM limechomwa moto katika eneo la Majengo na daraja linalounganisha Lindi na Mtwara limevunjwa. Mbali na hayo pia nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC)imechomwa moto. Katika Mji wa Mtwara milio ya mabomu na risasi ndio inayosikika kila kona. Jeshi la Polisi linajaribu kuwadhibiti vijana  na watu wengine ambao wanafanya vurugu hizo.   VURUGU ZA MTWARA ZASABABISHA BUNGE LIAHIRISHWE.... Spika wa bunge , Anne Makinda ameahirisha Bunge kutokana na hali ya Mtwara na ameiagiza serikali kuwa kesho wawasilishe taarifa bungeni kuhusiana na hali hiyo. Makinda ameitisha kamati ya uongozi ili kuona kama wanaweza kutuma kamati ya Bunge kesho kwenda huko.

PROFESA J. AJIUNGA NA CHADEMA

Image
PROFESA JAY AJIUNGA NA CHADEMA TAYARI KWA KUENDELEZA MAPAMBANO YA KISIASA KAMA MKONGWE SUGU Rapper mkongwe nchini, Joseph Haule aka Profesa Jay amejiunga rasmi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA. Profesa amekabidhiwa kadi ya uanachama wa CHADEMA na mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi aka Sugu.  Kujiunga rasmi kwa Profesa kwenye chama hicho kunaashiria kuwa huenda akawa na nia ya kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho mwaka 2015. Profesa ameamua kuweka wazi uamuzi wake baada ya watu wengi kuanza kumuuliza maswali. “Mmeniuliza sana kwamba mimi ni CHAMA gani jibu litapatikana Muda sio mrefu!! Still in Dodoma STAY TUNED,” alitweet.   Rapper huyo anayejulikana kama mchawi wa rhymes yupo Dodoma pamoja na wasanii wengine akiwemo Lady Jaydee kwa mwaliko wa Sugu

SHEHA WA TOMONDO-ZANZIBAR ALIYEMWAGIWA TINDIKALI

Image
PICHA ZA SHEHA WA TOMONDO- ZANZIBAR ALIYEMWAGIWA TINDIKALI JANA USIKU \ Sheha Mohammed Omary Said aliyemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana akiwa katika hospitali ya Mnazi Mmoja Unguja akipatiwa matibabu, Sheikh Mohammed amepata maumivu makali sehemu za kifuwa na jicho kuumia Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole. Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na kwamba hakuweza kumtambua. Sheha Mohammed Kidevu akiwa katika wodi ya Hospitali kuu ya Rufaa Mnazi Mmoja akipata matibabu ya majaraha ya kitu kinachosadikiwa kwa Tindi Kali,akipata matibabu hayo katika hospitali hiyo.
Image
Why Obama is coming to Tanzania Share Bookmark Print Email Rating President Barack Obama meets his Tanzanian counterpart Jakaya Kikwete in the Oval office at the Whie House. In his second tour of Africa next month Mr Obama will visit three African countries, which include Tanzania, Senegal and South Africa. PHOTO | FILE  By Elisha Magolanga  ( email the author ) Posted  Tuesday, May 21  2013 at  22:32 In Summary President Barack Obama will come with a delegation of more than 1200 people, including 500 businessmen and investors. He becomes the third US President to, consecutively, visit Tanzania after Bill Clinton in 2000, and George Bush in 2008. The US President’s tour of Africa will start on June 26 and end on July 3. In addition to Tanzania he will also visit Senegal and South Africa SHARE THIS STORY
Image
MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA DODOMA AFARIKI DUNIA BAADA YA KUGONGWA NA TRENI Mwanafunzi  wa chuo kikuu cha Dodoma  anayejulikana  kwa jina  la Boid Mwakitalima  amefariki dunia  baada  kugongwa na treni....Mwanafunzi huyo  alikuwa  mwaka  wa  tatu. Taarifa zinaeleza  kuwa, mwanafunzi  huyo  alikuwa   anatembea pembezoni  mwa  reli huku  akiwa ameweka  "headphone"  sikioni, hali  iliyomfanya  ashindwe  kusikia ama  kuhisi  chochote  juu  ya  muungurumo  wa  treni  hilo  mpaka  lilipomsogelea  karibu  na  kumsukuma  pembeni  ambapo  aliangukia  chuma  na  kuaga  dunia  pale  pale...  Makamu Mkuu wa Chuo kikuu  cha Dodoma Prof.Idrisa Kikula  akiwasili Collage ya Informatics  Mbele  ni Mshauri wa wanafunzi ( dean of student ) chuo kikuu cha dodoma, Nyuma ni mshauri wa wanafunzi, Pro.Anatory  ( dean of students )  collage ya informatics na Katikati ni Makamu mkuu wa chuo cha Dodoma... ------ Baada  ya  ajali  hiyo, mwanafunzi  hu