SHIDA YA UMEME KUSINI IMEKWISHA – MAJALIWA
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua Mradi wa Upanuzi wa Kituo cha Kufua Umeme kwa Gesi Asilia Mtwara, Mei 21, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani na kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe wakati alipozindua Mradi wa Upanuzi wa Kituo cha Kufua Umeme kwa Gesi Asilia Mtwara, Mei 21, 2018. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua eneo litakalotumika kupakuwa mafuta kutoka kwenye meli hadi kwenye matangi ya kuhifadhi mafuta katika bandari ya Mtwara, Mei 21, 2018. Majenereta mawili ya kuzalisha umeme yaliyonunuliwa serikali na kufungwa kwenye eneo la TANESCO lenye mitambo ya kuzalisha umeme wa gesi asilia katika Manispaa ya Mtwara ili kupanua uzalishaji umeme wa gesi asilia Mtwara . Majenereta hayo yalizinduliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Mei 21, 2018 . WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema shida ya umeme iliyokuwa inaikabili mikoa ya Lindi na Mtwar