Posts

KINANA,NDUGAI WATETA LUMUMBA LEO

Image
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza na Spika wa Bunge Job Ndugai, wakati Spika alipofika kumsalimia, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. Kushoto ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka.  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimwongoza kutoka nje Spika wa Bunge Job Ndugai, baada ya mazungumzo yao, wakati Spika alipofika kumsalimia, Ofisini kwake, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. Nyuma ya Sika ni Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka. Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Msemaji wa CCM Christopher Ole Sendeka, wakisubiri kuondoka Spika wa Bunge Job Ndugai Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam, leo Septemba 24, 2016. (Picha zote na Bashir Nkoromo).

DIAMOND PLATINUMS NA ZARI THE BOSS LADY WATIKISA VISIWANI ZANZIBAR

Image
Leo septemba 23 ni siku ambayo Zarithebosslady anasherehekea siku yake ya kuzaliwakatika kusherehekea siku hii muhimu mpenzi wake Diamond Platnumz, pamoja na mtoto wao Princess Tiffah wameambatana na baadhi ya watu wao wa karibu na kwenda mapumzikoni visiwani Zanzibar. Angalia Picha Jinsi Walivyowasili Visiwani Humo. Diamon Platnumz, Zari, Princess Tiffah na Mwarabau Fighter (Baunsa Wa Mondi) Diamond Platnumz na Mwanae Princess Tiffah.

Zari, Mobeto Kimenuka Tena!

Image
  Mwanamitindo Hamisa Mobeto. DAR ES SALAAM: Kimenuka tena! Ndiyo unavyoweza kusema baada ya mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kutupia picha ya hereni kwenye Mtandao wa Kijamii wa Snapchat huku akitupa dongo kwa kusema aliyesahau vitu vyake aende akavitoe, bifu limeibuka upya mitandaoni.   Mzazi mwenza wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’. Baada ya kutupia picha ya Snapchat hiyo, mashabiki mbalimbali wa mtandao huo walijiongeza na kuoanisha na picha ya Mwanamitindo Hamisa Mobeto kwa kufananisha hereni alizovaa siku za nyuma zikifanana na hizo alizodai Zari zimesahaulika kwenye chumba cha Diamond, nyumbani kwake, Tegeta-Madale jijini Dar. Mbali na mashabiki hao kujiongeza, mjadala mzito uliibuka pia wakidai ugomvi wa Zari na Mobeto si rahisi kumalizika maana kati yao hakuna anayeweza kuwa mpole na kumwachia mwenzake atambe. “Hili

LOWASSA AISIFU SERIKALI URATIBU MAAFA KAGERA

Image
Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa akisalimiana na  Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali Salum Kijuu alipomtembela leo ofisini kwake kumpa pole kutokana na athari ya tetemeko la ardhi katika mkoa wake Na Mwandishi Wetu-KAGERA. Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Edward Lowassa ameipongeza Serikali kwa namna ilivyojipanga kukabiliana na athari za tetemeko la ardhi lililotokea mkoani humo.Bw. Lowassa amesema hayo kupitia salamu zake alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meja Generali Salum Kijuu, ofisini kwake kumpa pole kutokana na athari zilizotokana na tetemeko hilo.“Napenda nikupongenze mkuu wa mkoa kwa namna ulivyokabili tukio hili, wala hatukuwa na mashaka wewe ni mtaalam wa majeshi wa siku nyingi kwa hiyo jambo hili limempata mwenyewe mpiganaji na tunaona kwa pamoja mmelishikilia vizuri,” alisema Lowassa. Adha Mhe. Lowassa alisema kuwa suala hili ni kubwa na halipaswi kuiachia Serikali peke yake katika kulikabili nalo kwani madhara yanaonekana ni makubwa

Shoga: tui la nazi lazima lionjwe!

Image
SHOGA yangu u hali gani? Ni siku nyingine tena tulivu imefika na tumekutana kwenye kona yetu hii inayowaelimisha wengi hususan wanawake wenzangu japo wanaume nao siwaachi nyuma. Natumai na wewe ni mzima wa afya na kama mgonjwa nakuombea kwa Mwenyezi Mungu atakutia nguvu. Baada ya hayo tugeukie basi kwenye hiki kilichonifanya niwaandikie, si mnakumbuka mara ya mwisho nilitoa somo la chakula cha usiku hakifunikiwi! Wengi mlinipigia simu na kunitumia meseji jinsi mnavyowafanyia waume zenu. Inanipa raha sana kuona mada imewaingia kisawasawa na kuyafanyia kazi shoga, mwanamke sharti ujue kukipika chakula bwana! Kiwe kitamu pia usimfunikie mume wako eti kwa kuhofia nzi au kupoa, kifunue ili akila ajihisi ameridhika, upo? Shoga baada ya hayo, nimepata maswali mengine mengi kutoka kwa nyie wasomaji wangu wengi mnaniuliza hivi tui la nazi lina utamu gani? Wengine mnauliza kwani lazima lionjwe? Jamani hata hili kweli la kuuliza au la kujiongeza mwenyewe? Umeshaandaa m

Ufanyeje unapompenda aliyependwa?

Image
KWANZA nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameniwezesha kuandika haya tena wiki hii tukiwa wazima. Lakini pia tumshukuru kwa kutuletea kitu kinachoitwa mapenzi. Mpenzi msomaji wangu, kupenda hakuna macho! Moyo ukishapenda hausikii la kuambiwa. Katika hili ndiyo maana unaweza kumuona mwanaume kazimika kwa demu ambaye hawaendani kabisa lakini moyo wake ndiyo umeshapenda. Ilishawahi kutokea msichana akampenda kijana mmoja ambaye ni fukara kupita maelezo. Yeye akawa ndiyo anamhudumia kwa kila kitu. Akamfanyia mpango wa ajira na mwisho wake wakafunga ndoa. Sasa hivi wanaishi maisha ya furaha na amani. Wamegeuka mfano wa kuigwa kwa jinsi wanavyo-pendana lakini huko nyuma msichana huyo alikuwa akichekwa kwa kutoa penzi kwa mwanaume asiye na mbele wala nyuma. Hayo ndiyo mapenzi jamani! Lakini pia katika kufurukuta kumtafuta mpenzi wa kuwa naye maishani, mwanaume unaweza kujikuta unaangukia kwa demu ambaye tayari ana mpenzi wake yaani ameshapendwa. Moyo w

Wastara, Bond Mapenzi Upyaa!

Image
STAA wa Filamu za Kibongo, Wastara Juma na meneja wake, Bond Suleiman mapenzi yao yamerejea upya baada ya miezi kadhaa nyuma Wastara kumtosa na kwenda kuolewa na Mbunge wa Jimbo la Donge-Zanzibar, Sadifa Juma. Kurejea kwa penzi la wawili hao kulibainika baada ya hivi karibuni waandishi wa habari hii kufika nyumbani kwa Wastara maeneo ya Magereza Relini jijini Dar na kumkuta Bond akiwa amejaa tele huku wakioneshana mahaba ya njiwa.  Wastara afunguka  Licha ya kwamba mwanzo zilipovuja taarifa kuwa wamerudiana walikuwa wakitumia nguvu kubwa kukanusha, safari hii walipobambwa hawakuwa na ujanja zaidi ya kuamua kuanika kila kitu kweupe. Staa wa Filamu za Kibongo, Wastara Juma na meneja wake, Bond Suleiman wakiwa pamoja. “Kweli tumeamua kurudi kwenye penzi letu na sikutaka kufunguka mapema kwa sababu siyo kila uhusiano unaufungukia kwani si kila mtu anayependa, nimepitia matatizo mengi na sababu kubwa ni wanadamu hivyo sikuona haja ya kutangaza tena huu uhusiano.

Irene Uwoya: Mapedeshee Siku Hizi Hawatoi Pesa

Image
Staa wa Bongo movie, Irene Uwoya ‘Mama Krish’. MAMBO vipi mpenzi msomaji wa safu hii uipendayo ya 10 Question? Kama kawa, kama dawa wiki hii tunaye mwanamama ambaye bado ni mrembo, Irene Uwoya ‘Mama Krish’. Naye yuko hapa kujibu maswali mbalimbali ambayo amembana nayo na yeye akaonesha ushirikiano katika kuyajibu. Je, una shauku ya kujua ni maswali gani aliyobananishwa nayo na akajibu vipi? ‘Intaviu’ hii hapa chini inakuhusu… Ijumaa: Hivi ni ipi siri ya wewe kuonekana mrembo siku zote? Uwoya: Cha kwanza mimi najipenda sana, kingine napenda kutumia vitu kwenye ngozi yangu ambavyo havina madhara na nakula matunda sana.  Ijumaa: Ni kweli wewe na Ndikumana bado ni mke na mume au ndo’ vile? Uwoya: Ndoa ya Kikristo haivunjiki bwana, mimi bado hakuna jinsi. Ijumaa: Hamna mpango wa kuishi pamoja na kumlea Krish wenu? Akiwa katika pozi. Uwoya: Ipo siku Mungu atajaalia itakuwa hivyo. Ijumaa: Uliwahi kusema unataka kupata mtoto wa pili kupitia kwa huyohuy

Rais Magufuli Ateua Viongozi Shirika la Ndege La Tanzania (ATCL)

Image

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA URUSI NA JAMHURI YA KOREA HAPA NCHINI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Song Geum-Young mara baada ya kupokea picha hiyo ya mfano wa Daraja jipya la Salenda. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Urusi hapa nchini Yuri Popov aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiaagana na Balozi wa Urusi hapa nchini Yuri Popov mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na kumkaribisha Balozi wa Jamhuri ya Korea hapa nchini Song Geum-Young aliyefika Ikulu kwa ajili ya mazungumzo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea picha ya mfano wa Daraja jipya la Salenda litakojengwa kuanzia maeneo ya Hospitali ya Agha Khan na kupita baharini hadi eneo la Coco

KWETU FASHION ILIVYOWAKILISHA MAVAZI YA KIMASAI KATIKA SHUKHULI YA East Africa cultural festival 2016 U.S.A.

Image
 Vivazi vya Missy Temeke wa Kwetu Fashions vikiwa tayari kwenye onesho la mavazi la Utamaduni wa Afrika Mashariki lililofanyika Onley, Maryland siku ya Jumamosi Septemba 17, 2016.  Missy T (kati) akiwa katika picha ya pamoja na models wake wakiwa na vivazi vya kimasai.

RAIS Uhuru Kenyatta wa Kenya aenda gengeni kula ugali na nyama choma.Tazama Picha

Image
Rais Uhuru Kenyatta amekichoka chakula cha ikulu ndio maana aliamua kujichanganya na Senator Mike Sonko kwenda gengeni kula ugali na nyama choma. Sonko alimpeleka rais huyo kupata chakula cha usiku kwenye soko la Kenyatta. Aliongoza na waheshimiwa wengine, Sakaja, Madam Shebesh na Kariuki walianza kwa kutembelea soko hilo kuzungumza na wafanyabiashara. Baadaye Sonko aliweka picha akiwa na waheshimiwa hao na kuandika: Together with President Uhuru Kenyatta, Hon Sakaja, Hon Madam Shebesh, Hon Kariuki we made a surprise stop at Kenyatta Market interacted with traders and later on my bestfriend and our President akasema anahisi njaa so I decided to buy lunch at one of the kiosks. Lazima tuinue biashara za watu.”

Ndege mpya ya serikali yatua Dar

Image
Ndege mpya ya serikali, Bombardier Q400 ikiwa katika Uwanja wa Julius Nyerere, Dar es Salaam baada ya kuwasili nchini mchana wa leo kutoka Canada. Ndege hiyo ikimwagiwa maji mara baada ya kutua. Rubani aliyeileta ndege hiyo akiwa katika pozi baada ya kutua. Baadhi ya watu walioipokea ndege hiyo wakiwa ndani wakifurahia mandhari yake. Baadhi ya Viongozi wa Shirika la Ndege la ATCL wakikagua ndege hiyo. Marubani waliyeileta ndege hiyo na kiongozi mmoja wa ATCL wakiwa katika picha ya pamoja. Ndege ya kwanza kati ya mbili zilizoagizwa na serikali, aina ya Bombadier Q400 kutoka nchini Canada tayari imewasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere uliopo jijini Dar es Salaam. Ndege hizi mbili zimenunuliwaili  kulifufua Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) ambalo kwa sasa lina ndege mbili, ambayo moja ni ya kukodi. Ujio wa ndege hizi mbili umeelezwa kuwa umelenga kusaidia katika soko la ndani na kurahisisha usafiri wa anga kwenda m