Posts

RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA JAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI PAMOJA NA JAJI KIONGOZI, PIA AAGANA NA BALOZI WA OMAN ANAYEMALIZA MUDA WAKE HAPA NCHINI.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali kuwa Jaji Kiongozi, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Jaji Shaaban Ali Lila kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Jaji Shaaban Ali Lila mara baada ya kumuapisha kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Jaji Ferdinand Leons Katipwa Wambali mara baada ya kumuapisha kuwa Jaji Kiongozi, Ikulu Jijini Dar es Salaam. Read more »  

Kesi ya Bosi wa TRA na Wenzake Yarudishwa Tena Mahakama Kuu

Image
                 Mahakama ya Rufani Tanzania, imeamuru jalada la kesi inayomkabili Kamishna Mkuu wa zamani wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya na wenzake kurudishwa Mahakama Kuu kwa ajili ya kusikilizwa rufani ya Jamhuri. Pia, imeagiza jalada hilo lipangiwe kusikilizwa kwa jaji mwingine dhidi ya rufaa ya kupinga kuondolewa shtaka la utakatishaji fedha katika kesi ya kujipatia Dola za Marekani milioni 6. Hukumu hiyo ilisomwa jana na Msajili wa Mahakakama ya Rufani, Zahra Maruma baada ya kusikilizwa na jopo la majaji watatu, likiongozwa na Mwenyekiti Salum Masati akisaidiana na Kipenka Musa na Augustine Mwarija. Msajili Maruma alisema mahakama hiyo imeona kwamba Jaji Mfawidhi Moses Mzuna alikosea kukubali pingamizi la utetezi na kutupilia mbali kusikiliza rufani ya kupinga uamuzi uliotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wa kuliondoa shtaka la kutakatisha fedha dhidi ya Kitilya na wenzake. “Mahakama hii imebatilisha uamuzi uliotolewa na Jaji Mzu

Pichaz: Muhammad Ali Alivyoagwa Kiislamu

Image
                  Maombi ya Kiislamu ya kuswaliwa kwa jeneza la marehemu bondia mashuhuri duniani Mohammed Ali yamefanyika katika jimbo la Kentucky, Marekani. Ali alifariki wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 74.  Maelfu ya watu, wakiwemo Waislamu kutoka maeneo mengi duniani, wamehudhuria swala hiyo katika ukumbi wa Freedom Hall, mjini Louisville.  Swala hiyo inapeperushwa moja kwa moja kupitia runinga na Waislamu wengi duniani wanatumai kwamba itaashiria mchango mzuri kwa dini ya Kiislamu nchini Marekani. Muhammad Ali alisilimu akiwa kijana. Alikuwa kwanza mwanachama wa madhehebu ya Nation of Islam, kundi lililotetea haki za watu weusi, lakini baadaye akakumbatia imani ya kawaida ya Kiislamu. Mazishi yake yatafanyika leo Ijumaa <a href='http://kwanza.co.tz/login/www/delivery/ck.php?n=a397efbc&cb=INSERT_RANDOM_NUMBER_HERE' target='_blank'><img src='http://kwanza.co.tz/login/www/delivery/avw.php?zone

Aliyemtukana Rais Magufuli Achangiwa Pesa

Image
VIJANA, wadau na wanaharakati wamefungua vikundi vya mtandao wa kijamii kwa ajili ya kuchanga fedha za kumsaidia kijana wa Arusha aliyepatikana na hatia ya kumtukana Rais na kuhukumiwa faini ya Sh7 milioni au kifungo. Kijana huyo, Isaack Habakuki wa Arusha alipatikana na hatia ya kumtukana Rais kwa kutumia ukurasa wake wa facebook na ametakiwa kulipa fedha hizo kwa awamu mbili na kuzikamilisha ifikapo Julai 7 au kwenda jela miaka mitatu. Diwani wa Kata ya Levolosi jijini Arusha (Chadema), Ephata Nanyaro ambaye anaratibu michango hiyo kwa mkoa wa Arusha, alisema mpaka sasa wameshakusanya Sh 800,000/- ambazo walizipata kwa njia ya kutuma kwa simu. Alisema wanatarajia kupata Sh1.7 milioni kutoka mikoa yote. “Tumesikia familia yake imeweza kutoa 3.5 millioni pekee, sisi tumejitolea kumsaidia ili afikishe 7 millioni kabla ya tarehe 7 mwezi julai,” alisema. 27

Chadema Wajifungia Kujadili hatua za kuchukua Dhidi ya Jeshi la Polisi Lililopiga Marufuku Maandamano na Mikutano

Image
Viongozi wa Chadema, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Vincent Mashinji jana walijifungia kutwa nzima kujadili hatua za kuchukua dhidi ya kitendo cha Jeshi la Polisi kuzuia maandamano na mikutano ya chama hicho ya kisiasa. Tangu asubuhi jana, viongozi hao walikuwa na kikao katika ukumbi wa Mandela, hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza na wakati wa mapumziko mafupi saa kumi jioni, Mbowe alisema chama hicho kitatoa kauli rasmi leo baada ya kikao kingine kilichotarajiwa kufanyika jana usiku. “Tutatoa kauli rasmi kesho (leo), baada ya vikao. Ninachoweza kuthibitisha ni kwamba tunaendelea kushauriana njia sahihi ya kuchukua,” alisema Mbowe. Juni 7, mwaka huu polisi ilitangaza kupiga marufuku kwa muda usiojulikana maandamano na mikutano yote ya kisiasa kwa kile kilichodaiwa ni taarifa za kiintelijensia za kuwapo tishio la kiusalama na kuwa wanakwenda kushawishi wananchi kuipinga Serikali. Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Salum Mwalimu alis

Wasichana 500 wa Tanzania wanatumika Asia

Image
 Wasichana 500 wa Tanzania wanatumika Asia Serikali ya Tanzania imesema zaidi ya wasichana 500 raia wa nchi hiyo wanatumikishwa katika kazi hatari zikiwemo za ukahaba katika nchi za Asia na Uarabuni. Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Tanzania imesema imepata taarifa kuwa kuna mtandao unaowasafirisha wasichana katika nchi hizo kwa madai ya kufanya kazi za ndani lakini baadae hutumikishwa kwenye biashara ya ngono. Taarifa zinasema baadhi ya wasichana hao wemekimbilia kwenye ubalozi wa nchi hiyo ili kuomba kurudishwa nyumbani Mindi Kasiga ni Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Tanzania ambaye anasema '' Mtandao huo unachofanya ni pamoja na kuwatafuta wasichana wenye umri kati ya miaka 18 na 24 na hata chini ya umri huo na kuwalaghai kuwa kuna fursa za ajira katika mahoteli, migahawa, maduka makubwa au kazi za nyumbani nchi za nje na kwamba watawasaidia wasichana hao kupata kazi hizo pamoja na kuwawezesha kupata vyeti vya kusafiria VISA na tiketi za ndege kwa

Muhammad Ali Kuzikwa Kishujaa Leo

Image
Muhammad Ali LOUISVILLE, Marekani GWIJI wa ndondi duniani, Muhammad Ali, anatarajiwa kuingizwa kwenye nyumba yake ya milele kwa heshima kubwa leo Ijumaa baada ya sara maalum ya Kiislam huko Louisville, Kentucky, Marekani. Ratiba ya sara za mazishi, ilianza juzi Jumatano na jana zaidi ya watu 14,000 kuzikwa kishujaa leo waliungana kuomboleza kwa sala katika ibada iliyorushwa moja kwa moja kwenye televisheni. Ali, alifariki dunia Ijumaa iliyopita akiwa na umri wa miaka 74 baada ya kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa Parkinson ambao unashambulia mfumo wa seli. Mazishi yake leo yanatarajiwa kushirikisha wawakilishi kutoka dini mbalimbali wakiwemo Wayahudi na Wakristo. Ali, alianza kupanga jinsi mazishi yake yatakavyokuwa mwaka mmoja uliopita na akasisitiza yawe huru kwa kila mmoja anayetaka kuhudhuria, afanye hivyo bure, familia imethibitisha. Ali ameacha mke na watoto tisa.

Wasiotumia EFDs Marufuku Kufanya Biashara na Serikali

Image
KUANZIA Julai mosi mwaka huu, serikali imepiga marufuku kwa Wizara, Taasisi, Wakala za Serikali, Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kufanya biashara na wazabuni na wafanyabiashara wengine ambao hawatumii mashine za kielektroniki - EFDs. Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango alisema hayo jana bungeni wakati akiwasilisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017 bungeni mjini Dodoma jana. Aidha, Dk Mpango aliwapongeza wafanyabiashara walioitikia matakwa ya Sheria ya Usimamizi wa Kodi ambayo inamtaka kila mfanyabiashara isipokuwa wale ambao wametangazwa rasmi na Kamishna wa Mamlaka ya Mapato kutotumia mashine za EFD kutoa risiti kila anapouza bidhaa au huduma. Alisema ili kuwa na usimamizi mzuri wa fedha za serikali na kuhakikisha kwamba zinatumika kama ilivyokusudiwa, kwa mamlaka aliyopewa chini ya Sheria ya Fedha za Umma na kanuni zake, alitangaza kuwa malipo yote lazima yaambatanishwe na ankara za madai au stakabadhi (tax invoice) zilizotolewa na mashin

Huu Hapa Mchanganuo wa Bajeti ya Serikali 2016/ 2017

Image
SERIKALI imewasilisha Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/2017 ya Sh trilioni 29.53, ambayo nguvu kubwa imewekwa katika kukusanya mapato kwa kulinda viwanda vya ndani na kubana matumizi ya serikali ili kuelekeza sehemu kubwa ya matumizi katika maeneo ya vipaumbele. Katika bajeti hiyo, bidhaa za lazima zinazogusa maisha ya wananchi ikiwemo mafuta ya petroli na dizeli pamoja na ushuru wa barabara na maji ya kunywa, havijaguswa huku bidhaa za starehe kama bia, sigara, soda, juisi na nyingine kama nguo za mitumba, huduma za kupanga nyumba na uhamishaji fedha kwa simu, vikipandishwa kodi, huku kiinua mgongo cha wabunge, kufutiwa msamaha wa kodi. Aidha, makusanyo ya mapato yasiyo ya kodi, ikiwemo mapato ya taasisi za udhibiti kama Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Mafuta (EWURA), Shirika la Viwango (TBS), Jeshi la Polisi (Trafiki) na mamlaka nyingine za udhibiti, sasa yatapelekwa moja kwa moja katika Mfuko Mkuu wa Serikali ambapo mahitaji yao ya fedha yatatolewa na Wizara ya

KARIBU UJUMUIKE NA WAZAZI WENZAKO KWENYE JUKWA LA KUJADILI MALEZI YENYE MALENGO

Image
Ni ukweli usiopingika kuwa waazazi wote hupenda kuona watoto wao wakikua katika maadaili yanayopendeza na ikiwemo kufaulu vizuri katika masomo yao na hata wafikiapo umri wa kujitegemea wawe vijana wenye maono bora. Hapo nyuma hakukuwa na mitaala ya kuweza kuwasaidia wazazi kukuza watoto vile inavyotakikana, hivyo ilipelekea watoto wengi kushindwa kufikia malengo yao na lawama walitupiwa wazazi wao. Njoo ujiunge sasa na wazazi wenzako kwa mara ya kwanza Tanzania inakuletea (Malezi yenye malengo) ni jukwaa la majadiliano,maoni,na njia mbadala za kuwalea watoto wetu. Nafasi ni chache jisajili mapema Karibuni sana. Wazungumzaji watakuwa Mrs Grace Makani Tarimo kutoka  Grace Inc Ltd na Dr. Elie Waminian (PHD) Kutoka Marekani Namba ya simu 0754-46174 11/06/2016. Hyatt Regency Hotel

TIMU YA ENGLAND YAWASILI PARIS UFARANSA KWAJILI YA EURO

Image
Kikosi cha wachezaji 23 wa timu ya taifa ya England kimewasili Paris Ufaransa mchana wa leo June 6 2016 kwa ajili ya michuano ya Euro 2016, England imeondoka Lutonasubuhi na kuwasili Paris Airport-Le Bourget mchana wa leo June 6 2016, Englanditacheza mchezo wake wa ufunguzi wa Euro 2016 Jumamosi hidi ya Urusi.

RAIS DKT MAGUFULI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA RAIS WA SAHARAWI, AKUTANA NA NAIBU WAZIRI MKUU WA UBELGIJI, BALOZI WA MAREKANI NA KUAGANA NA BALOZI WA ITALY

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana  na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa mambo ya Nje wa Ubelgiji Mhe. Didier Reynders aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana  na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa mambo ya Nje wa Ubelgiji Mhe. Didier Reynders aliyemtembelea Ikulu Dar es salaam leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akisalimiana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italy nchini Mhe. Luigi Scotto  aliyemtembelea na kumuaga baada ya kumaliza muda wale wa kazi Ikulu Dar es salaam leo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akisalimiana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Italy nchini Mhe. Luigi Scotto  aliyemtembelea na kumuaga baada ya kumaliza muda wale wa kazi Ikulu Dar es salaam leo. Rais

TAARIFA YA UTEUZI WA MWENYEKITI WA BODI YA WAKALA WA UAGIZAJI WA MAFUTA KWA PAMOJA (PBPA)

Image
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Profesa Sospeter M. Muhongo (Mb), amemteua Dk. Steve Mdachikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), kuanzia tarehe 03 Juni, 2016. Kufuatia uteuzi huo, amewateua pia wafuatao kuwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya PBPA kuanzia tarehe 03 Juni, 2016. 1. Dkt. Daniel Sabai 2. Dkt. Henry Chalu 3. Dkt. Siasa Mzenzi 4. Mr. Salum Mnuna Imetolewa na; KATIBU MKUU 6 Juni, 2016

TRA YAVUKA LENGO LA MAKUSANYO YA KODI KWA MWEZI MEI 2016

Image
MKamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata akitilia mkazo jambo wakati wa kikao na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya makusanyo ya mapato kwa mwezi Mei 2016,kilichofanyika katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo na kushoto ni Meneja wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Abdul Mapembe. MAMLAKA ya Mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.032 katika mwezi Mei ambayo ni sawa na asilimia 100.7 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.025 katika mwezi huo. Makusanyo ya kipindi cha miezi kumi na moja (Julai 2015 hadi Mei 2016) ni jumla ya shilingi trilioni 11.956 sawa na asilimia 99.2 ya lengo la shilingi trilioni 12.054 katika lengo la kipindi hicho kwa Tanzania Bara na Zanzibar. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi leo kuhusu mwenendo wa makusanyo ya mapato, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata amesema TRA inaendelea na jitihada mbalimbali kuhakiki

MSANII DIAMOND ATOA MSAADA WA MADAWATI 600 KWA MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM MHE. MAKONDA

Image
  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akimpongeza Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' mara baada ya kumtembelea ofisini kwake na kutoa mchango wake wa madawati yapatayo 600 kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya Mkoa wetu. Akiongea katika makabidhiano hayo msanii huyo alisema ni jambo jema kwao kuweza kujitolea mchango huo ili kuweza kumuunga mkono Mhe. Makonda katika kukabilana na changamoto za elimu. Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' akiongea mara baada ya kukabidhi msaada wa madawati yapatayo 600 kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda ili kuweza kupunguza tatizo la wanafunzi kukaa chini. Makabidhiano hayo yalifanyika leo Juni 6, 2016 ofisini kwa mkuu wa mkoa jijini Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda akitoa shukrani zake za pekee kwa Mkurugenzi wa WCB, msanii Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' kwa kuweza kutoa madawati 600 ikiwa ni mchango wake k

Polisi Jijini Mwanza Wapambana na Majambazi kwa Saa 16, Wakamata Silaha Nzito, Watatu Wauawa

Image
Watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi,wameuawa katika majibizano ya risasi na askari polisi mkoani Mwanza,alfajiri ya kuamkia jana jumapili katika mapango ya mlima wa Utemini yaliyopo kata ya Mkolani jijini Mwanza. Kamanda wa polisi mkoani Mwanza Ahmed Msangi,amewataja majambazi waliouwa katika majibizano ya risasi usiku kucha kuwa ni Omar Francis Kitaleti mkazi wa Nyegezi Kona,said Khamis Mbuli maarufu kama fundi bomba mkazi wa bugarika na jambazi mwingine ambaye jina lake bado halijafahamika. Amesema majambazi hayo yalikuwa yamejificha kwenye mapango ya mlima wa Utemini kabla ya askari polisi kufanikiwa kuyaua. Jambazi mmoja aliyeuawa ambaye hajafahamika jina lake mwenye umri kati ya miaka 20 hadi 25 alikuwa akiwashambulia polisi kwa kutumia bastola ambapo baada ya polisi kumpiga risasi walimpekua na kumkuta akiwa na bastola aina ya Chinese,iliyokuwa na risasi tatu ndani ya magazine,huku majambazi wengine waliokuwepo kwenye mapango hayo wakiendelea kujibishana kwa