TCRA yawapa kibano akina lulu!
Staa wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ Gladness Mallya na Ojuku Abraham, DAR ES SALAAM: Kufuatia tabia ya akina dada wengi kuweka picha za nusu utupu katika akaunti zao kwenye mitandao ya kijamii, wakiwemo mastaa kama Lulu, Masogange na wengineo, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewapa kibano kikali, Risasi Mchanganyiko lina stori kamili. Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka hiyo, Innocent Mungi alisema ingawa jukumu la kuwakamata wote wanaoweka picha zinazokiuka maadili ni la jeshi la polisi kupitia kitengo cha makosa ya mtandao (Cyber Crime), taasisi hiyo inawasiliana na wamiliki wa mitandao ya kijamii ili kutafuta namna nzuri ya kuwadhibiti. Kidoa. “Tunachofanya ni kuzungumza na hawa watu ili kuwafungia wote wanaokiuka maadili, tunajua baadhi yao wanajiunga katika mitandao kwa kutumia majina ya uongo, lakini sisi tutazifungia ‘line’ maana kila moja ina namba zake za siri na hazifanani na zingin