Posts

NAIBU KAMISHNA WA POLISI (DCP) ANG’OLEWA KWA TUHUMA YA KUMILIKI NYUMBA 40

Image
Mkuu  wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu   Mkuu  wa Jeshi la Polisi, IGP Ernest Mangu, amemwondoa kwenye nafasi yake, Mnunuzi wa Vifaa na Boharia Mkuu wa jeshi hilo, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Adriano Magayane ili kupisha uchunguzi wa tuhuma dhidi yake. Kuondolewa kwa DCP Magayane katika nafasi hiyo kunatokana na taarifa zilizochapishwa na vyombo vya habari hivi karibuni, kuwa anamiliki nyumba zaidi ya 40 na kumbi kadhaa za starehe ndani na nje ya Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Gazeti la Mtanzania,  IGP Mangu amefikia uamuzi huo kwa kile kinachodaiwa kuwa tuhuma hizo ni nzito na zinalenga si kumfedhehesha yeye kama ofisa mkuu wa Jeshi la Polisi, lakini kwa jeshi zima. “IGP Mangu amemwondoa mara moja DCP Magayane kutokana na tuhuma zinazomkabili, kwa kweli ni nzito, nadhani hatua zilizochukuliwa ni sahihi… unajua sisi askari tuna miiko ya utendaji kazi, sasa inapotokea tuhuma kama hizi kwa ofisa kama huyu, lazima uchunguzi wa ki

TAZAMA PICHA ZA MELI KUBWA KULIKO ZOTE DUNIANI

Image
Longer than The Shard and wider than a Boeing 747 wingspan: The world's largest cruise ship arrived in the UK today for the first time.

BINTI MWENYE ULEMAVU AFUNGIWA NDANI MIAKA 16

Image
Vitendo vya kuwafungia ndani watoto wenye ulemavu limeendelea kushamiri kwenye maeneo mengi nchini tukio la sasa likitokea katika kijiji cha njani wilayani Arumeru ambapo mtoto wa kike mweye ulemavu wa viungo amebainika kufungiwa ndani kwa kipindi cha umri wake wote wa miaka kumi na sita. Mtoto huyo Wine Ruth anayelelewa na bibi yake baada ya kutelekezwa na mama yake mzazi mara baada tu ya kugundua kuwa ana ulemavu amegundulika wakati wa zoezi la kuwaorodhesha watoto wenye ulemavu wilayani Arumeru ambapo bibi yake Veraelly Ndetaulo anakiri kumfungia kwa ajili ya usalama wake anapokwenda kuwatafutia rizi wajukuu zake. Akizungumzia tukio hilo Mbunge wa Viti Maalum Walemavu Dk.Elly Macha aliyeongoza zoezi la kumtoa ndani mtoto huyo anasema imefika wakati sasa jamii ikatambua kuwa malezi ya watoto wa kundi hilo ni la kushirikishana hasa ikizingatiwa kuwa wengi wamekua wakitokea kwenye familia zenye kipato duni. Maisha ya Bibi Ndetaulo anayemlea mtoto huyo mwenye ulemavu,pa

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AMUWAKILISHA RAIS MAGUFULI KWENYE KUMBUKUMBU YA KARUME ZANZIBAR

Image
  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein akiweka Shada la Maua kwenye Kaburi la Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Muasisi wa ASP Hayati Sheikh Abeid Amani Karume wakati wa Dua maalum ya kumbukumbu ya kifo cha Muasisi huyo    inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo April 07, Kisiwandui Zanzibar.   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akijiandaa kuweka Shada la Maua kwenye Kaburi la Rais wa kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Muasisi ASP Hayati Sheikh Abeid Amani Karume wakati wa Dua maalum ya kumbukumbu ya kifo cha Muasisi huyo    inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo April 07, Kisiwandui Zanzibar, ambapo  Makamu wa Rais amemuwakilisha Rais John Magufuli ambaye yuko nje ya nchi kikazi.   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wa pili kulia, Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein kulia na Viongozi mbalimbali