Posts

WAZIRI MKUU: RUSHWA YAPOTEZA DOLA BILIONI 150 AFRIKA

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akihutubia Mkutano wa  Tano wa Bunge la Afrika ya Mashariki kwenye ukumbi wa Benki Kuu jijini Dar es salaam Machi 8,2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema tatizo la rushwa barani Afrika limesababisha bara hilo lipoteze dola za Marekani bilioni 150 kila mwaka. Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumanne, Machi 8, 2016) wakati akihutubia wajumbe wa mkutano wa tano wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) linaloendesha vikao vyake jijini Dar es Salaam. Mkutano huo ulioanza Machi 6, utamalizika Machi 18, mwaka huu. Akizungumza kwa niaba ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu alisema rushwa imechangia kwa kiasi kikubwa kurudisha nyuma maendeleo ya Jumuiya hiyo. “Rushwa yaweza kuwa kwa njia kuhonga fedha, kupata fedha kwa kula njama, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, ama kwa njia za vitisho,” alisema. “Kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Afrika (AU), rushwa na urasimu vimeainishwa kuwa ni vikwa

MAJALIWA AHUTUBIA MKUTANO WA TANO WA BUNGE LA AFRIKA YA MASHARIKI

Image
Spika wa Bunge la  Afrika Mashariki  ( EALA ),  Mhe .  Daniel  Kidega (katikati) akiongoza ufunguzi wa Mkutano wa tano wa Bunge hilo jana jijini Dar es Salaam. Kulia Kwake ni Spika wa Bunge la Tanzania Mhe Job Ndugai na Kushoto ni Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa. Spika wa Bunge la  Afrika Mashariki  ( EALA ),  Mhe .  Daniel  Kidega (katikati) akiongoza ufunguzi wa Mkutano wa tano wa Bunge hilo jana jijini Dar es Salaam. Kulia Kwake ni Spika wa Bunge la Tanzania Mhe Job Ndugai na Kushoto ni Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa. Spika wa Bunge la  Afrika Mashariki  ( EALA ),  Mhe .  Daniel  Kidega (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa Bunge la Tanzania Mhe Job Ndugai pamoja na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa tano wa Bunge hilo jana jijini Dar es Salaam. Spika wa Bunge akihutubia ufunguzi wa Mkutano wa tano wa   Bunge la  Afrika Mashariki ( EALA) jana jijini Dar es Salaam. Spika wa Bunge la  Afrika Mashariki  ( EALA

Tuzo Ya Lulu yamliza mama Kanumba

Image
Lulu. Na Imelda Mtema, RISASI mchanganyiko DAR ES SALAAM! Tuzo ya Mtayarishaji Bora wa Filamu Afrika Mashariki, iliyotwaliwa na Mbongo, chozi mama wa aliyekuwa nyota wa filamu Bongo, marehemu Steven Kanumba, Flora Mtegoa, tambaa na Risasi Mchanganyiko liujaze moyo wako. Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na mama Kanumba, muda mchache baada ya Lulu kutangazwa na waandaaji wa tuzo ambao ni African Magic Viewers Choice ‘AVCA’ kwamba yeye ni mshindi, aliwasiliana na mama yake mzazi, Lucresia Karugila, ambaye naye alimtwangia simu mama Kanumba ili kumfahamisha ushindi huo ambapo mama huyo alitoa chozi. WEWE SIKIA HII “Sasa sijajua, yule mama alilia kwa sababu ya furaha au vipi! Maana si unajua siku za karibuni hawakuwa vizuri? Lakini inawezekana akalia kwa chuki kweli?,” kilihoji chanzo hicho. NJIA PANDA Pamoja na maneno yote, bado chanzo hicho kilishindwa kuweka wazi kilio cha mama Kanumba kilitokana na nini lakini kilisema kuwa, mwanamke huyo, baada ya kupokea salamu

Sakata la Makamba na Muitaliano lachukua sura mpya

Image
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), January Makamba. Sakata la Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira na Muungano), January Makamba na Mdogo wake Mwamvita kudaiwa kupokea rushwa kutoka kwa raia wa Italia, Vincenzo Cozzolino ili wamsaidie kupata zabuni ya ujenzi limechukua sura mpya. Sauti na jumbe mbalimbali zilizosambazwa na kuwekwa kwenye mtandao na mmiliki wa tovuti ya U-Turn, Mange Kimambi, raia wa Tanzania aishie Marekani, zinaonesha mazungumzo kati ya watatu hao, mwaka 2011. Jana, Mwamvita na Makamba walikiri kuwa sauti hizo ni za kweli. Msikilize Mhe. January Makamba akifunguka kuhusu sakata hilo hapa chini: Muitaliano huyo ambaye anadaiwa kumpa Mange Kimambe ushahidi wote wa mawasiliano kati yake na Ndugu hao, amejitokeza na kuwasafisha akidai kuwa hakuwahi kuwapa rushwa wala kuhusiana na January kibiashara. Cozzolino ameandika ujumbe akidai kuwa ingawa yeye na Mwamvita walikuwa na uhusiano wa mapenzi mwaka 2011 na b

Wauguzi wasitisha huduma Butimba

Image
Wauguzi, na madaktari wa Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana Butimba mkoani Mwanza wakiendelea na mgomo jana. Wagonjwa wakiwa katika hali ya mshangao baada ya wauguzi, na madaktari kugoma. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Konisaga (katikati) akiongea na wagonjwa. …Akiendelea kuongea.   …Wagonjwa kabla ya mkuu wa wilaya kufika. Na Idd Mumba, Mwanza Hali ya usalama katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana Butimba mkoani Mwanza kwa wauguzi, na madaktari sio nzuri na kusababisha wananchi kutopata huduma zaidi ya saa sita jana, jambo ambalo lilizua taharuki kubwa kwa wagonjwa na wananchi hospitalini hapo. Mgojwa aliyejitambulisha kwa jina Janet John alisema wakifika katika hospitali hiyo ya saa moja asubuhi kwa ajili ya kupatiwa matibabu lakini hadi ilipofika saa tatu asubuhi hakukuwepo na daktari ama nesi aliyeingia katika vyumba vyao kwa ajili ya kupatiwa matibabu. ‘’Sisi tumefika hapa hospitali mapema sana tukawa tumekaa kusubiri wauguzi na madakta

BREAKING NEWS: AJALI MBAYA YATOKEA ASUBUHI HII BARABARA YA MANDELA DALADALA YAGONGANA NA LORI LILILOBEBA NG'OMBE YASABABISHA VIFO NA MAJERUHI

Image
Ajali Mbaya imetokea eneo la Tabata Matumbi, Ajali iliyohusisha Lori la Ng'ombe na Daladala iliyo kuwa ikitokea Gongo la Mboto kuelekea Ubungo  Abiria kadhaa Wamepoteza Maisha na wengine wengi Wamejeruhiwa Vibaya sana  

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu Ataka Makahaba wanaojiuza Pamoja na Wanaume Wanaowanunua Wakamatwe

Image
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza kuiunga mkono Polisi nchini katika operesheni ya kukamata wateja wa makahaba kuhakikisha biashara hiyo inakoma nchini. Waziri wa wizara hiyo, Ummy Mwalimu alisema takwimu zinaonesha wanawake ndio waathirika wakubwa wa ugonjwa wa Ukimwi, ambapo kati ya Watanzania 100 wanaopimwa, sita ni wanawake na wanaume ni wanne pekee. Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Dar es Salaam jana, Ummy alisema si haki kuwakamata wanawake wanaojiuza na kuwaacha wateja wao ambao ni wanaume. “Ninalipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua hiyo kwa sababu imeonesha kutoegemea upande mmoja kwa kuwakamata wanawake makahaba. Wote wanaojiuza na wanaonunua huduma hiyo ni wakosaji wanaostahili kuchukuliwa hatua za kisheria.Tunaungana na Polisi kushiriki operesheni hiyo,” alisema. Alieleza kuwa, biashara ya ukahaba inayofanywa na wanawake isingekuwepo endapo wateja wasingekuwepo, hivyo, wateja wanastahili

JAMII YATAKIWA KURIPOTI UHALIFU UNAOFANYWA KWA NJIA YA LAINI ZA SIMU NA MITANDAO.

Image
Na. Benedict Liwenga-Maelezo JESHI la Polisi limewataka wananchi kuwa makini ili kuepukana kutapeliwa fedha na watu wasio waaminifu wanaojipatia fedha hizo kwa njia ya simu na mitandao. Kauli hiyo imetolewa leo na Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Mrakibu Mwandamizi (SSP), Advera Bulimba wakati akiongea na Mwandishi wa Idara ya Habari kwa njia ya simu ambapo amesema kuwa jamii hainabudi kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuwaibua watu wanaojihusisha na uhalifu kwa njia ya laini za simu pamoja na njia ya mtandao kwa kutoa taarifa mapema katika vituo vya Polisi. Ameongeza kuwa, watu wanatakiwa kuwa makini kabla ya kutuma pesa kwa watu wanaodaiwa kuhitaji kutumiwa pesa ili kujiridhisha nao na kuepuka kutapeliwa. ‘’Jeshi la Polisi limekuwa likifanyia kazi taarifa zinazotolewa na walalamikaji kwa kuwakamata watuhumiwa na kuwafikisha mahakamani ambapo mpaka hivi sasa tayari kuna baadhi tumewafikisha mahakamani na baadhi wanatumikia vifungo vyao,’’alise

KIVUKO CHA MV DAR ES SALAAM KUANZA KAZI HIVI KARIBUNI

Image
Rais Dk. John Pombe  Magufuli akikagua kivuko cha MV Dar es salaam.  Na Raymond Mushumbusi MAELEZO Kivuko cha Mv Dar es Salaam maarufu kama kivuko cha Rais Magufuli kipo katika matengenezo ya kawaida na kinatarajiwa kuanza kutoa huduma kama kawaida siku za hivi karibuni. Akitoa ufafanuzi juu ya madai ya kutelekezwa kwa kivuko cha Mv Dar es Salaam katika maegesho yaliyopo kigamboni Jijini Dar es Salaam ,Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Mhandisi Manase Le-Kujan amesema sio kweli kwamba kivuko hicho cha Mv Dar es Salaam kimetelekezwa bali kimepumzishwa kutokana na matengenezo yaliyohitajika kufanywa katika kivuko hicho ili kuongeza ufanisi katika kutoa huduma kwa wasafiri. “Sio kweli kwamba Kivuko cha Mv Dar es Salaam kimetelekezwa katika maegesho ya Kigamboni bali kimepumzishwa kwa muda kwa ajili ya matengenezo yake ya kawaida, hii ikiwa ni juhud i ya kukiwezesha Kivuko hiki kuwa katika ubora unaotakiwa katika kutoa hudumazake” “

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA KOREA NA INDIA LEO

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Profesa Choi Oe Chool Rais wa GLOBAL SAEMAUL DEVOLOPMENT NETWORK ya Jamhuri ya Korea, Wakati Rais huyo na Ujumbe wake alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es Salaam Leo March 08,2016, kwenye mazungumzo yao Viongozi hao wamezungumzia juu ya kukuza na kuendeleza ushirikiano wa kimaendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya p