Ostaz Juma: Muziki karibu univunjie ndoa
Meneja wa muziki hapa Bongo, Ostaz Juma Namusoma. Musa mateja UKIANZA kutaja majina ya mameneja mbalimbali wa muziki hapa Bongo, baadhi ya majina makubwa yasiyoisha miongoni mwao huwezi kulikosa jina la Ostaz Juma Namusoma. Kwa mujibu wa kinywa chake mwenyewe Ostaz Juma Namusoma, juzikati nilipata nafasi ya kumbana na kunieleza kiunagaubaga namna alivyoweza kujipenyeza hadi kupata jina kupitia muziki wa Bongo. Kwa kinywa chake aliniambia kwamba, muziki kwake ni sehemu ya maisha ambayo ameishi kwa kipindi kirefu sana, kwani tangu alipokuwa mdogo alipenda muziki kushinda kitu chochote, msikie mwenyewe. OSTAZ JUMA: Mimi ni miongoni mwa vijana wa kipindi hicho ninayetokea Musoma mkoani Mara. Nilianza kupenda muziki tangu nasoma shule ya msingi tena mapema kabisa nikiwa darasa la tatu. Nikiwa shuleni nilikuwa napenda sana kuimba nyimbo mbalimbali za wasanii wa Kongo hadi nikafikia hatua ya kununua redio na kuwarekodi watoto wenzangu wakiimba kisha nazitunza nyim