Posts

MFALME WA BLUES, BB KING AFARIKI DUNIA

Image
 Riley B. King 'BB King'. MFALME wa Blues, mpiga gitaa na mwimbaji, Riley B. King 'BB King' wa nchini Marekani amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 89 akiwa usingizini huko Las Vegas jana. King alifahamika kwa baadhi ya nyimbo zake kali kama My Lucille, Sweet Little Angel na Rock Me Baby. Marehemu alizaliwa Mississippi na kuanza kutumbuiza miaka ya 1940. Miezi ya nyuma marehemu alikuwa na matatizo ya kiafya na hivi karibuni alipelekwa hospitali akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari.

Baada ya Kupotea kwa Muda: Wema Sepetu Arudi tena Kuigiza Akiwa na JB- VIDEO

Image
Staa mrembo wa Bongo Movies, Wema Sepetu ameshare nasi video ya kazi mpya  inayokwenda kwa jina la  Chungu Cha Tatuakiwa na Staa mwnzake, Jacob Stephen  'JB'. Kwa muda mrefu sasa Wema Sepetu amekuwa afanyi filamu, Bila shaka mashabiki wake wana hamu kubwa sana ya kumuona tena kwenye filamu.

MAIMATHA APEWA MAKAVU LIVE BAADA YA KUINGILIA UGOMVI WA WEMA SEPETU NA AUNT EZEKIEL

Image
     

MAJAMBAZI SUGU WAKAMATWA MCHANA HUU JIJINI DAR WAKITAKA KUIBA BENKI YA NMB

Image
Majambazi hao wakiwa wametiwa pingu baada ya kukamatwa na jeshi laPolisi jijini Dar.  Wananchi wakiwa eneo la Benki ya NMB Sinza-Mori, Dar wakifuatilia tukio hilo.  Polisi jijini Dar wamewakamata watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakiwa katika jaribio la kuiba pesa katika benki ya NMB iliyopo Sinza-Mori, Dar es Salaam.Tukio hilo limetokea mchana wa leo katika Benki ya NMB tawi la Sinza-Mori jijini Dar ambapo majambazi hao walikamatwa wakiwa katika harakati za kutekeleza tukio hilo.Majambazi hao baada ya kukamatwa wamepelekwa katika kituo cha Polisi Mabatini kilichopo Kijitonyama jijini Dar.

RAIS WA MSUMBIJI FILIPE JACINTO NYUSSI AWASILI NCHINI KWA ZIARA RASMI YA SIKU TATU

Image
Rais Kikwete akimpokea Rais Filipe Jacinto Nyusi uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo. Rais huyo anayefanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi kama rais wa Msumbiji yuko katika ziara rasmi ya siku tatu. Rais Kikwete akimpokea Rais Filipe Jacinto Nyusi uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo. Rais huyo anayefanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi kama rais wa Msumbiji yuko katika ziara rasmi ya siku tatu. Rais Filipe Jacinto Nyusi akipokea shada la maua baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo. Rais huyo anayefanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi kama rais wa Msumbiji yuko katika ziara rasmi ya siku tatu. Rais Filipe Jacinto Nyusi akikagua gwaride la heshima baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam leo. Rais huyo anayefanya ziara yake ya kwanza nje ya nchi kama rais wa Msumbiji

KUTOKA BUNGENI DODOMA

Image
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na wabunge kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Mei 18, 20154, Victor Mwambalaswa wa Lupa, Sylvester Mabumba wa Dole na Dkt. Hamisi Kigwangalla wa Nzega. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na mbunge wa Viti Maalum, Riziki Lulida kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Mei 18, 2015. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Uratibu na Bunge Mhe.Jenista Mhagama akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Simanjiro Mhe.Christopher Ole-Sendeka nje ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya kupitishwa kwa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu Mei, 16 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

FINALY MAJIZO HAVE DECIDED TO SHOW OF HER EXPECTED WIFE HAMISA MOBETO

Image
their.relationship started as jokes, peole and social medias started to talk about this wonderful relationship as gossip without any prouf, another thing which it have suprised people is after hamisa mobeto run away from his social networks for six months, people without knowing any reason but people and social networks have come to realise that in the ninth months of the pregnancy of hamisa mobeto, and she deleiver her child well without any problem, the website of makubwa haya website gave a big congratulations of this two super stars what they have done is wonderfull and very different from other african

MAKUBWA ZAIDI YAIBUKA PATI 2 YA PADRI ALIYENASWA NA MREMBO KICHAKANI JIJINI DAR!

Image
Stori: Waandishi Wetu KISA cha Padri Anatoly Salawa (pichani) ambaye pia ana cheo cha Katibu Mtendaji wa Idara ya Mawasiliano wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (Tanzania Episcopal Conference, Tec), kunaswa hivi karibuni kichakani akiwa na mrembo, kimechukua sura mpya, Gazeti la Kufichua Maovu, Uwazi linakokotoa.  Padri Anatoly Salawa akitaharuki baada ya fumanizi hilo. TUJIKUMBUSHE Tukio hilo la kushangaza lilijiri hivi karibuni majira ya saa 8: 02 usiku ambapo padri huyo na mrembo walinaswa ndani ya gari aina ya Toyota RAV 4 lenye namba ya usajili T 674 ADA kwenye kichaka kilichopo maeneo ya viwanda na gereji za magari makubwa, Kurasini jijini Dar. Gazeti ndugu na hili, Ijumaa la Mei 15, mwaka huu liliandika kwa kina habari hiyo ikiwa na kichwa kisemacho; PADRI WA KATOLIKI ANASWA KICHAKANI! YALIYOJIRI SASA Kabla ya tukio hilo halijapachikwa kwenye Gazeti la Ijumaa, Padri Salawa alipigiwa simu mara kadhaa ili kupewa nafasi ya kujitetea lakini hakupokea na hata pale a

RECHO WA THT ALIA NA BABU TALE BAADA YA KUZUIWA KUMTUNZA DIAMOND.

Image
MREMBO mwenye sauti nyororo kutoka Jumba la Kukuza Vipaji Tanzania (THT), Winifrida Josephat ‘Recho Mapenzi,’ hivi karibuni alijikuta akiangua kilio baada ya kuzuiwa kupanda kwenye jukwaa kwa ajili ya kumtunza Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz.’ Mrembo mwenye sauti nyororo kutoka Jumba la Kukuza Vipaji Tanzania (THT), Winifrida Josephat ‘Recho Mapenzi. Tukio hilo lilitokea ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar kwenye shoo ya Zari All White Party ambapo bidada huyo akiwa katika hali ya mzuka alijikuta akiishia kuangua kilio baada ya kuzuiwa na Meneja wa Diamond, Babu Tale kupanda jukwaani. Akilalama kwa machungu baada ya kukwamishwa kumfikia Diamond, Recho alisema kuwa hakufurahishwa hata kidogo na uamuzi wa Babu Tale kwani anamjua wazi ni msanii hivyo hakuwa na haja ya kuwaamuru mabaunsa kumzuia kwenda kumtuza staa mwenzake. “Kweli Tale hajanitendea haki hata kidogo, kwani nilimuahidi mapema Diamond ningemtuza na pale nilitaka kutimiza ahadi

YULE BI HARUSI ALIYETOROKA SIKU MOJA BAADA YA KUFUNGA NDOA ANASWA LIVE.

Image
YULE mwanamke Tatu Ally, mkazi wa Kongowe, Mbagala jijini Dar aliyefunga ndoa na kutoroka kwa mumewe aliyetajwa kwa jina moja la Ramadhan, mkazi wa Mbezi-Kimara, amenaswa baada ya msako mkali uliofanywa na polisi kwa kushirikiana na ndugu zake. Stori ya Tatu kutoroka kwa mumewe siku moja baada ya kufunga ndoa iliripotiwa na gazeti hili wiki iliyopita, ukurasa wa nyuma, ikiwa na kichwa cha habari kilichosomeka:BI HARUSI AFUNGA NDOA, ATOROKA. Habari kutoka kwa chanzo cha kuaminika kilieleza kuwa, Tatu alikutwa na mwanaume mwingine maeneo ya Toangoma, Kigamboni, Dar na kujitetea kuwa aliamua kutorokea kwa mwanaume huyo kwa kuwa ndiye mchumba’ke wa siku nyingi na alikuwa amesafiri kwa muda tu. “Kweli Tatu amepatikana na alipelekwa moja kwa moja kwenye Kituo cha Polisi cha Kongowe-Mwisho, huku akiwa na huyo anayedai ni mchumba’ke wa siku nyingi (jina halikupatikana).Ilisemekana kwamba, Tatu akiwa mikononi mwa polisi alinena kuwa mwanaume huyo alikuwa amesafiri kwa muda na

MADEREVA WAPEWA KIPAUMBELE KWENYE KAMATI YA KUSIMAMIA USAFIRISHAJI.

Image
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akizungumza na wandishi wa habari hawapo pichani ofisini kwake leo jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wandishi wa habari waliohudhulia katika mkutano wa wandhi wa habari na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda jijini Dar es Salaam leo.(Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.) Na Avila Kakingo,Globu ya Jamii. Madereva wamepewa kipaumbele kwenye tume itakayokuwaikisimamia usafirishaji,kwani tume hiyo itakuwa na wajumbe watano kutoka Umoja wa madereva tuu na kutoka sekta nyingine watakuwa wajumbe watatu . Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo. Makonda amesema kuwa kamati hiyo haitaundwa na serikali, wajumbe watatokana na uchaguzi wa madereva wenyewe pia na wajumbe wengine watatoka Mamlaka ya usafirishaji (SUMATRA), TABOA , TATOA, Wizara ya Ajira, wizara ya na mambo ya ndani. Makonda ameongezea kuwa Mg

MREMBO ABABULIWA ‘RECEPTION’ NA MTALAKA WA BOSI WAKE JIJINI DAR

Image
INASIKITISHA sana! Muuza baa mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Halima, anajiuguza vidonda vikubwa mwilini vilivyotokana na kumwagiwa maji ya moto na mwanamke ambaye ni mtalaka wa bosi wake ambaye ndiye mmiliki wa baa anayofanyia kazi, Amani linakupa zaidi. Halima anayedaiwa kumwagiwa maji ya moto. Kwa mujibu wa chanzo ambacho ni ndugu wa majeruhi huyo, tukio hilo lilijiri mwezi uliopita ndani ya baa moja maarufu iliyopo maeneo ya Ubungo, Dar es Salaam ambapo majeruhi huyo anafanyia kazi baada ya mwanamke huyo kuamini Halima anatembea na mtalaka wake. Inadaiwa kuwa, mwanamke huyo ambaye ni mtuhumiwa na mwanaume mmiliki wa baa aliyejulikana kwa jina moja la Mushi waliachana miaka mingi iliyopita.“Lakini mwanamke akawa anamfuatilia mumewe kila siku na kwa kila kitu. Ilifika mahali akaambiwa kuwa, mwanaume huyo aliyetengana naye ana uhusiano wa kamapenzi na baamedi wake mmoja.” “Ndipo siku ya tukio, mwanamke huyo alifika kwenye baa hiyo akitoka kusikojulikana. Wakati h

ANGALIA MVUA ZINAVYOKWAMISHA SHUGHULI ZA WATU JIJINI DAR

Image
Wananchi wakijaribu kuvuka barabara eneo la Sinza, Afrika sana leo asubuhi. Mwanafunzi akionekana akipita katika barabara iliyojaa maji eneo la Afrika Sana. Baadhi ya wananchi wakionekana kutafakari namna ya kupita eneo la Sinza Afrika Sana. Kijana aliyeko upande wa kushoto ambaye hakufahamika jina lake haraka, akivusha wananchi kwa kiasi cha shilingi mia mbili (200) eneo la Afrika Sana. Magari pamoja na Bajaji zikionekana kupita kwa tabu katika barabara iliyojaa maji. Vijana wakiendelea kuvusha raia kwa kiasi cha shilingi mia mbili (200) eneo la Afrika Sana.MVUA zinazoendelea kunyesha jijini Dar es Salaam, zimeleta mafuriko katika baadhi ya maeneo ya jiji hilo na kusababisha adha kwa wakazi wake huku barabara zikiwa zinapitika kwa tabu na zingine kutopitika kabisa.

LULU AFUNGUKA NA KUDAI ''MIMI SINA JINI MAUTI JAMANI''

Image
MSANII nyota wa filamu, Elizabeth Michael `Lulu’ amekanusha uvumi kuwa matatizo yanayowatokea wanaume aliowahi kuwa nao yanatokana na yeye kuwa na Jini Mauti anayesababisha hali hiyo kutokea, Amani linakujuza.   Msanii nyota wa filamu, Elizabeth Michael `Lulu’.Akizungumza na gazeti hili juu ya madai ya wadau mbalimbali kuhusiana na matukio mengi yanayomtokea, muigizaji huyo wa filamu ya Foolish Age, alisema maisha yake ya siku hizi ni ya kusali sana, hivyo anaamini kutokana na maombi yake, hali yake iko vizuri kutokana na Mungu kumpa anachokihitaji. “Ninasali sana kwa sasa aisee, mara nyingi nafanya hivyo mara tatu kwa siku, ninao uwezo wa kukemea mapepo na yakaondoka, hayawezi kukaa mwilini mwangu,” alisema muigizaji huyo ambaye miaka michache iliyopita, aliondokewa na mpenzi wake, Steven Kanumba aliyeanguka na kufariki mbele yake. Mtabiri mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, Maalim Hassan Yahya Hussein, alisema tatizo kubwa linalomsumbua binti huyo ni jini mauti am

ADEBAYOR AVIANIKA VISA VYA FAMILIA YAKE NA INAVYOMCHUMA FEDHA, BARUA YAKE YASIKITISHA WENGI, IMETAFSIRIWA KISWAHILI HAPA

Image
Mshambuliaji wa Tottenham, Emmanuel Adebayor ameandika maelezo marefu kwenye akaunti yake ya Facebook kuelezea visa anavyofanyiwa na familia yake wakiwemo mama, kaka na dada zake. Adebayor anawashutumu ndugu zake kwa tamaa ya mali zake. Licha ya kuwafanyia mambo mengi ikiwemo kuwajenga nyumba, kuwanunulia magari na kuwapa mitaji ya biashara, wameendelea kumtupia shutuma nyingi. Tumeitafsiri post hiyo kwaajili yako. Sehemu ya maelezo hayo marefu inasema: SEA, nimezihifadhi habari hizi kwa muda mrefu lakini nadhani leo ni muhimu kuziweka wazi baadhi yake kwenu. Ni kweli masuala ya kifamilia yanapaswa kusuluhishwa ndani kwa ndani na sio hadharani lakini nafanya hivi ili pengine familia zote zinaweza kujifunza kutokana na kile kilichotokea kwangu. Pia weka akilini kuwa hakuna chochote kati ya haya kinahusiana na pesa. Nikiwa na miaka 17, kwa mishahara yangu kama mcheza soka, nilijenga nyumba kwaajili ya familia yangu na kuhakikisha kuwa wapo salama. Kama nyote mn

WEMA, AUNT KIMENUKA KISA ZARI

Image
KIMENUKA! Mashosti wa kufa na kuzikana, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson wanadaiwa kugombana baada ya Aunt ‘kuposti’ kwenye ukurasa wake wa Instagram tangazo lililohusiana na pati ya mwandani wa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ iliyofanyika Mlimani City jijini Dar wikiendi iliyopita. Mashosti wa kufa na kuzikana, Wema Isaac Sepetu na Aunt Ezekiel Grayson. Kwa mujibu wa mtu wa karibu wa mastaa hao wa sinema za Kibongo, baada ya Aunt kuposti tangazo hilo akiwalaumu watu wa mtandao wa huduma za simu waliomtumia ndipo Wema akaona na kuja juu. Ilielezwa kwamba baada ya Aunt kutupia picha ya tangazo hilo, Wema alichukizwa na kitendo hicho huku akimuona Aunt kuwa amemsaliti. Aunt Ezekiel Grayson. Ilisemekana kwamba katika utetezi wake, Aunt hakupendezwa na tangazo hilo alilotumiwa na mtandao huo wa simu. “Wema alivyoona alichukia na kusema Aunt alikuwa akimsaliti na

SALMAN KHAN WA BOLLYWOOD AHUKUMIWA JELA MIAKA 5 KWA MAUAJI

Image
Mwigizaji maarufu wa filamu za Bollywood nchini India Salman Khan. Mwigizaji maarufu wa filamu za Bollywood nchini India Salman Khan amekuhumiwa kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia ya kumuua mtu mmoja asiye na makazi alipokuwa akiendesha gari huku akiwa amelewa mjini Mumbai. Khan alikuwa ameshtakiwa kwa kuua bila kukusudia baada ya kuelekeza gari lake kwenye kundi la watu waliokuwa wamelala kwenye njia kando ya barabara mwaka 2002. Mmoja kati ya watu hao Noor Ullah Khan alikufa katika ajali hiyo. Khan amedai kuwa dereva wake ndiye anayepaswa kulaumiwa lakini mashuhuda wanasema mwigizaji huo ndiye aliyekuwa kwenye usukani na alikimbia baada ya kutokea kwa ajali hiyo. Kwa mujibu wa Jaji wa mahakama hiyo, Khan anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo. NA BBC