Watu wawili wamekufa katika matukio tofauti wilayani Bunda, mkoani Mara, akiwemo mwanamke mmoja aliyeuawa na mchumba wake na kufukia mwili wake porini na kisha fisi kufukua kaburi hilo na kichwa chake kuonekana mitaani kikiliwa na mbwa. Tukio hilo la kikatili lililothibitishwa na polisi, limetokea Machi 22 mwaka huu, majira ya saa 3:00 asubuhi katika kijiji cha kiroreli wilayani Bunda. Mwanamke aliyeuawa na mchumba wake ametambuliwa kwa jina la Wambura Magonze, mkazi wa kijiji cha Kiroreli. Polisi wamesema kuwa baada ya kupata taarifa ya tukio hilo walikwenda katika eneo la tukio wakiongozana na mkuu wa upelelezi wilayani hapa, Munguwajuna, na kukuta mbwa mitaani wakila kichwa cha marehemu huyo. Imeelezwa kuwa mwaume huyo baada ya kumuua mchumba wake kwa kipigo, wakiwa wanatoka shambani aliuzika mwili wake porini katika kaburi lenye urefu wa futi moja. Aidha, imeelezwa ku