Posts

FANYA HAYA KUZUIA MATITI YA YAKO/MPENZI WAKO YASIWE MALAPA

Image
  Kwanza kabisa hakikisha mtindo wa kulala ni kifudifudi (kulalia tumbo), kwa kufanya hivyo kunasaidia kwa kiasi kikuwa kufanya matiti yako pumzike, kwamba hakutakuwa na kuning'inia kama utakuwa umelala chali(lalia mgongo) au kiubavu.  Zoezi...1 Asimame wima dhidi ya mlango au ukuta kisha aegeshe matiti yake mahali hapo kwa nguvu kisha aachie (ajitoe ukutani), zoezi hili hufanya matiti yaume sana lakini wewe kama dada mpe moyo kuwaavumilie. Afanye hivyo mara 20 kila asubuhi.  Zoezi....2 Simama wima huku mikono yako ikiwa imenyooshwa huku na kule kisha ipeleke mbele nakukutanisha viganja vyako alafu irudishe nyumba kadiri uwezavyo (sio lazima ikutane) ila utahisi maumivu fulani sehemu ya matiti (misuli yafanya kazi hapo)....fanya hivyo mara 10 na ongeza hesabu njinsi unavyokua.  Zoezi...3 Ukiwa umesimama wima na mikono yako imenyooshwa huku na hule inan

HAYA NDO MAJINA 250 YA WAUZA UNGA NA BANGI NCHINI TANZANIA.

Image
Majina ya watanzania 255 wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya   yamejulikana  na  JAMHURI  imeamua kuyachapisha...   Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa kwenye orodha hiyo wapo watu maarufu na baadhi wamekuwa wakitoa misaada ,huku wengine wakijifanya ni wazee  wa kanisa na kushiriki  shughuli mbalimbali za kijamii....   Uchunguzi wetu usio na chembe ya shaka  unaonesha kuwa orodha hii ya watu watakaoandikwa hapo chini kwa sasa wapo chini ya uangalizi wa mahakama na polisi..   "Ni kweli kuna watu tumewapeleka mahakamani, huko wamewekwa chini ya uangalizi na wanatakiwa kuripoti  kwa  muda wanaopangiwa.Tunafanya hivyo baada ya uchunguzi wetu kubaini kwa ni kweli  wanahusika na biashara hii haramu."Alisema  Nzowa Nzowa aligoma kuyataja majina hayo, lakini uchunguzi uliofanywa na JAMHURI  kutoka ndani ya jeshi la polisi na  mahakama  umefanikiwa  kuyapata  majina  hayo... Katika orodha hii, yumo mchungaji aliwekwa chini ya uangalizi

CHID BENZ ASIMULIA JINSI ALIVYOTHIRIWA NA BANGI NA MADAWA YA KULEVYA....ANASEMA HAWEZI KUMALIZA DK 2O BILA KUVUTA

Image
  Rapper Chidi Benz leo kwa mdomo wake mwenyewe amekiri kuwa alikuwa akitumia madawa ya kulevya kwa miaka mingi. Chidi amefunguka leo kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM. Alisema japo hakwenda Nairobi kwaajili ya rehab, mazingira yalimlazimu kutafuta tiba ili aondokane na madhara ya madawa hayo. Alieleza kuwa alipofika jijini Nairobi alikuwa akitakiwa kufanya show nyingi na mwandaaji alimuuliza kama kuna kitu atahitaji ili awezE kufanya show vizuri. “Nikamwambia Yeah kuna vitu ntavihitaji,” alisema Chidi. “Nikamwambia ‘mimi bana kuna vitu ninavyovitumia nikikaa 20 minutes bila hivyo vitu ni noma nachanganyikiwa na akili tena sina, kwahiyo sijui tutafanyaje’.   Akaniambia ‘mimi ntapataje hivyo vitu Chidi na Nairobi ni gharama sana. Nikamwambia ‘mimi pia nina wazo jingine kuna mtu alinitonya kwamba kuna kitu kinaweza kikafanyika na pesa Fulani, pesa nyingi kama milioni 15, 16 hivi za kibongo.  Akaniambia kikifanyika hicho maanake vinavyofolewa kabisa h

KAGERA KWANUKA, CCM YAFUKUZA MADIWANI 8 WA MANISPAA YA BUKOBA

Image
  Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kagera, leo kimewafukuza madiwani 8 wa Manispaa ya Bukoba kupitia chama hicho na kufutwa nyadhifa zao za udiwani kutokana na mgogoro uliokuwa ukiendelea Waliofukuzwa ni: Richard Gaspar (Miembeni ) Murungi Kichwabuta (Viti maalum) Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe) Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa wilaya (Kashai) Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga) Robert Katunzi (Hamugembe) Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na Dauda Kalumuna (Ijuganyondo)

MBOWE AWATAKA WANANCHI KUCHANGIA RASIMU YA KATIBA MPYA

Image
Wananchi wa mkoa wa Mara wametakiwa kuchangia kikamilifu katika rasimu ya Katiba mpya ili wamuenzi Baba wa Taifa Mwl JULIUS KAMBARAGE NYERERE kupitia michango yao itakayoiwezesha Tanzania kupata Katiba mpya. Mwenyekiti wa taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) FREEMAN MBOWE amesema mjini Musoma kuwa  suala la katiba ni jambo linalogusa maisha ya watanzania hivyo ni muhimu kutumia busara kujadili kwa mustakabali wa taifa. Akizungumza katika mikutano na wananchi iliyofanyika kwenye wilaya za Bunda, Serengeti, Tarime na Musoma mjini MBOWE amempongeza Rais wa Tanzania Dk. JAKAYA KIKWETE kwa kukubali kuanzisha mchakato wa katiba mpya. Kwa upande wake mbunge wa Ubungo JOHN MNYIKA aliyeambatana na Mwenyekiti huyo ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Mara kushiriki katika hatua zote zilizosalia katika kupata Katiba mpya ili wawe sehemu ya kuandikwa kwa historia  

KUMBE WAZUNGU KUMWAGIWA TINDIKALI SIRI YAFICHUKA ,SABABU ZAANIKWA SASA HALI INATISHA.

Image
Kate Gee na Kristie Trup baada ya kufikishwa hospitali ya Chelsea and Westminster jijini London. Sakata  la wasichana wawili, Kate Gee (18) na Kristie Trup (18), raia wa Uingereza ambao walimwagiwa tindikali wakiwa katika matembezi Mtaa wa Shangani, visiwani Zanzibar Agosti 8, mwaka huu, limeingia sura nyingine baada ya sababu ya tukio hilo kuanikwa. Kate Gee (18) na Kristie Trup (18) kabla ya kuja Tanzania. Habari za chini kwa chini zinadai kuwa namna ya uvaaji ilichangia wasichana hao kutendewa ukatili huo wa kutisha ambapo ilisemekana waliofanya hivyo walikuwa wanatoa onyo kwa wengine.Na Global Publisher Kristie Trup. MWEZI MTUKUFU WATAJWA “Wale jamaa (waliowamwagia tindikali Wazungu) lengo lao ni kuwapa fundisho na wengine pia ili suala la kukiuka mavazi mwezi mtukufu lisijirudie,” alisema mtoa habari wetu. Shule ya Mtakatifu Monica walipokuwa wakifundisha kwa kujitolea mabinti hao. Habari zaidi zilidai kuwa kundi la wat

WANAOTUHUMIWA KUMPIGA SHEKHE WATINGA KORTINI.

Image
VIJANA sita waumini wa dini ya Kiislamu wilayani Kyela mkoani Mbeya wamefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Kyela kujibu mashtaka manne wanayokabiliana kutokana na vurugu walizozifanya msikitini, ambapo Shekhe Mkuu wa Wilaya Kyela, Nuhu Mwafi lango na waumini wengine walipigwa na kuumizwa.Tukio hilo lilitokea wakati wa Sikukuu ya Idiel- Fitr, wakati shekhe huyo akiongozwa swala. Wakisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kyela, Joseph Luambano, ilidaiwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Nicholaus Tiba kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa manne.  Ilidaiwa kuwa kosa la kwanza ni kula njama za kutenda kosa, kufanya vurugu msikitini, kufanya shambulio la kudhuru mwili na kujeruhi. Alidai kuwa siku ya tukio Shekhe Mkuu wa wilaya alishambuliwa akiwa anaendesha swala ambapo katika tukio hilo watu wengine, akiwemo mtunza hazina wa msikiti, Hamisi Hussein, alijeruhiwa kichwani. Aliwataja watuhum

44 WAUAWA KINYAMA MSIKITINI, NIGERIA

Image
 Maiduguri ni moja ya majimbo yaliyowekewa sheria ya hali ya hatari Takriban waumini 44 wameuawa kwa kupigwa risasi wakiwa msikitini Kaskazini Mashariki mwa Nigeria, kwa mujibu wa maafisa wa jimbo la Borno. Mauaji hayo yalifanyika wakati wa maombi ya asubuhi Jumapili , ingawa taarifa zimejitokeza Jumatatu , kutokana na hitilafu ya mawasiliano kwani jimbo hilo liko chini ya sheria ya hali ya hatari. Shambulizi lilifanyika katika mji wa Konduga, ulio umbali wa kilomita 35 kutoka mji mkuu wa jimbo hilo , Maiduguri. Washambulizi wanasemekana kuwa wanachama wa kundi la wapiganaji la Boko Haram, ambalo liliwaua maelfu ya watu tangu mwaka 2009. Gazeti la Daily Post, liliripoti kuwa watu wengine 26 walikuwa wanatibiwa kwa majeraha waliyopata wakati wa shambulizi hilo hospitalini Maiduguri. Mwanachama wa kikundi cha vijana kinachotoa ulinzi kwa raia, aliambia shirika la habari la Associated Press, kuwa wapiganaji wao wannne waliuawa

MABINTI WAWILI WAKAMATWA AIRPORT NA MADAWA YA KULEVYA YENYE THAMANI YA BILIONI 2.5

Image
Vitendo vya usafirishaji wa madawa ya kulevya vinazidi kuendelea duniani na safari hii wasichana wawili wadogo kabisa, mmoja ana umri wa miaka 19 na mwingine ana umri wa miaka 20 wote wawili wamekamatwa kwenye airport ya Lima nchini Peru wakijaribu kusafirisha mzigo huo.  Passport za mabinti hao zinawatamburisha kama raia wa uingereza na huko ndiko mzigo huo ulikuwa unaelekea. Baada ya kukamatwa na polisi mabinti hawa Mellisa 19 na Michaella 20, walikubali kosa hilo la kujaribu kusafirisha madawa ya kulevya aina ya Cocaine na hadi hivi sasa wapo kwenye mikono ya polis

ANGALIA PICHA ZA MAZISHI YA BILIONEA ERASTO MSUYA

Image
  Wakati unaingia  nyumbani kwa bilionea Erasto Msuya hili ndio  bango lililokua limewekwa.   Hapa utaratibu wa kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Maremu Erasto Msuya.   Hii ndio nyumba ya milele ya bilionea Erasto Msuya ikiandaliwa. MIRERANI zikiwa ni siku takribani sita zimepita tangu mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite aliyefahamika kwa jina la Erasto Msuya kupigwa risasi zaidi ya ishirini na kufariki dunia papo hapo katika eneo la Bomang'ombe karibu na njia panda ya KIA (Kilimanjaro International Airport). Kifo hicho kilichokua na utata mkubwa na kupelekea watu wengi kujiuliza maswali mengi yasiokua na majibu. Leo ilikua ni siku ya mazishi ya mfanyabiashara huyo ambaye kutokana na kuwa alikua akiishi jijini Arusha maeneo ya kwa Iddi ilibidi jana jumatatu wafanye utaratibu wa kuuga mwili wa marehemu nyumbani kwake na leo jumanne kwenda kuzikwa Mirerani katika kijiji cha Kairo.         Msiba wa Erasto ulikua

JE, KUVUNJIKA KWA UCHUMBA NI KOSA KISHERIA?

Image
Re: Kavunja ahadi ya uchumba sheria inasemaje? Sheria ya ndoa ya mwaka 1974 kama ilivofanyiwa marekebisho mwaka 2002 iko wazi katika hilo na kwa kifupi angalia kifungu cha 69-71, kama inavosomeka hapo chini:- 69. Right to damages for breach of promise of marriage (1) A suit may be brought for damages for the breach of a promise of marriage made in Tanzania whether the breach occurred in Tanzania Tanzania or elsewhere, by the aggrieved party or, where that party is below the age of eighteen years, by his or her parent or guardian: Provided that– (a) no suit shall be brought against a party who, at the time of the promise, was below the age of eighteen years; (b) no damages shall be awarded in any such action in excess of loss actually suffered as a result of expenditure incurred as a direct result of the promise. (2) A suit may similarly be brought in respect of the breach of a promise of marriage made in any other country but only if such an action wou

ANGALIA PICHA ZA KILICHOJIRI KATIKA MAZISHI YA ERASTO MSUYA,BILIONEA ALIYEPIGWA RISASI ARUSHA..

Image
Mchungaji Abeli Msuya na mkewe wakitoa sala mbele ya jeneza la marehemu. Familia ya marehemu katika ibada ya kumwaga marehemu Erasto Msuya iliyofanyika  Jumatatu huko  Sakina Arusha. Dada wa marehemu Erasto Msuya  katika ibada ya kumwaga marehemu kaka yake Erasto Msuya nyumbani kwake Sakina Arusha Ndugu jamaa na marafiki wakiwa na majonzi. Mchungaji Mwanga akitoa neno katika ibada hiyo. BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE

DANGURO LA UCHI LAFUMULIWA BUGURUNI DAR..... GHARAMA YA CHUMBA NI 1200/= ....KUMLIPA MALAYA NI 5000 TU.

Image
JUMBA linalodaiwa kutumika kuendesha shughuli za ukahaba limebainika kuwapo katika eneo la Buguruni, jijini Dar es Salaam. Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima, umebaini kuwapo kwa jumba ambalo linatumika kama nyumba ya kulala wageni, ambako idadi kubwa ya makahaba hujazana na kuendesha biashara ya kuuza miili yao bila wasiwasi.  Wasichana wanaofanya biashara hizo hutoza kiasi cha sh 5,000 kama huduma ya ngono na chumba kwa matumizi ya muda mfupi. Biashara hiyo ambayo imeleta usumbufu mkubwa kwa wakazi wengi wanaopakana na nyumba hiyo, imekuwa ikifanikiwa kutokana na kuwapo kwa baadhi ya askari polisi wanaodaiwa kuwalinda wasichana hao pamoja na mmiliki wa nyumba hiyo. Nyumba hiyo inavyo vyumba vingi vinavyotozwa kiasi sha sh 1,200 kwa chumba pamoja na kondomu. Kadhalika wasichana wenye umri wa miaka 15, ni miongoni mwa wanaofanya biashara hiyo. Mjumbe wa serikali ya mtaa wa eneo hilo, Amiri Banza, alikiri kuwapo kwa biashara hiyo, ingawa alisema wam

MAN UTD YAICHAPA WIGAN 2 VAN PERSIE ATISHA

Image
Early blow: Robin van Persie headed Manchester United into the lead in the sixth minute In action: Manchester United's Atonio Valencia takes the ball away from Wigan's Jordi Gomez Ahead: The Dutchman arrived late in the penalty area to head Patrice Evra's cross into the bottom corner Joy: United celebrate Van Persie's early goal at Wembley New signings: United's Wilfried Zaha, (left) competes with Wigan Athletic's James McClean The England winger flitted in and out, rather like United as a whole in a largely mundane affair. Elusive: United's new winger Wilfried Zaha escapes the attention of Ben Watson Vocal: David Moyes and Owen Coyle shout out instructions to their teams Welbeck came close to turning home a near-post chance and Van Persie threatened once more. Advantage doubled: Van Persie net's Manchester

ANGALIA PICHA ZA SHEIKH PONDA BAADA YA KUWASILI MUHIMBILI

Image
Picha ya juu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kiislamu nchini , Shekhe Ponda Issa Ponda,akipata matibabu  jana muda mfupi baada ya kuumizwa na kitu chenye ncha kali kwenye bega lake la kulia wakati akiekelea katika Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja wa Mjini Morogoro baada ya kumalizika kwa kongamano ya Dini ya Kiislamu jana Mkasa huo ulitokea janamajira ya saa 12: 15 za jioni eneo la barabara ya Tumbaku karibu na Fire, mara baada ya kumaliza kwa Kongamano la Kiislamu lililofanyika kwenye uwanja wa Shule ya Msingi Kiwanja Cha Ndege, Kata ya Saba Saba , Manispaa ya Morogoro.Picha ya chini baada ya kwanza juu akiwa hospitali ya taifa ya muhimbili mchana huu kwa ajili ya matibabu  KATIBU wa Jumuiya ya Kiislamu nchini , Shekhe Ponda Issa Ponda akiwa anaingizwa katika chumba cha matibabu hospitali ya taifa ya muhimbili -MOI leo mchana, baada ya kupokelewa katika Hospitali ya muhimbili.

NAY WA MITEGO ATEMANA NA DEMU WAKE.....

Image
 JANA  Nay wa Mitego alikuwa akiandika ujumbe wenye mafumbo kwenye Instagram na baada ya kuusoma ndani ya mistari  ilibainika kuwa  huenda mambo si mazuri kati yake na mpenzi wake ambaye hivi karibuni alikuwa akitarajia kumzalia mtoto lakini mimba ikaharibika. Nay ambaye jina lake halisi ni Emmanuel Munisi, jana alianza  kwa kuandika ujumbe huu: Sasa mapenzi basi# by diamond Platnumz..!! Single boy# Ally Kiba#966 ’ Baada ya muda kidogo aliandika tena: "Niko ivi,,, nikikupenda nakupenda kwa asilimia 100# na kila m2 atajua juu ya upendo wangu kwako..!! Bt ukizingua nakuacha na ninakusahau kwa asilimia 200# na kwa muda mchache 2.   "Nikiamua huwa sirudi nyuma..!!# Mwanamke mjinga ataivunja ndoa yake kwa mikono yake ye mwenyewe# by Linex.#966’

"WASANII WENGI WA BONGO MOVIE NI OMBA OMBA...ACCOUNT ZAO HAZINA KITU"... BATULI

Image
Batulli  ambaye  ni mmoja wa waigizaji wa kike warembo nchini na ambaye jina lake halisi ni Yobnesh Yussuph aka Nesh, amefunguka kwenye Twitter kuwa licha ya soko la movie kupanuka, waigizaji wengi hawana kitu.   “Wasanii wengi wa filamu huwa tunaamka asubuhi hata hatujui tutakula nini. Accounts zetu hazina kitu wakati tuna film nyingi sana sokoni,” ametweet.   “Wenzetu huamka na mipango kamili ya siku iliyopo lakini wasanii wa film huwa tunaamka huku tukiwaza ni nani wa kumpiga kibomu siku iende.   " Jina kubwa umejibana umepata gari yako 1 tena used, siku ikiipeleka garage unashinda na wewe huko huko garage kazi zote unasimamisha #Huruma. ” Batulli ameilalamikia pia mikataba mibovu iliyopo kwenye filamu.   “Mikataba ya kazi za film Tanzania ukiisoma unaweza ukajuta kwanini uliamua kuwa muigizaji, unauza movie yako na haki miliki kwa miaka 50.  "Hakuna anaependa ndio maana tunalia na serikali mikataba ibadilishwe tupewe kipaum

MSANII WA KIKE BONGO MOVIE AMWANDIKIA BARUA RAIS KIKWETE!!

Image
Yobnesh Yusuph(Batuli) ambaye ni actress maarufu Swahiliwood amemuomba Rais Jakaya Kikwete alivunje Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) na kuliunda upya. Leo kupitia akaunti yake ya twitter muigizaji huyo aliyejaaliwa mvuto na kupendwa na mashabiki wengi wa filamu ali-tweet moja kwa moja akimtaja JK kwa kuandika "ujumbe wa sikukuu ya Eid kwako Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzana, vunja baraza la BASATA uliunde upya". Ingawa Batuli hakutaja moja kwa moja kwanini baraza hilo linalosimamia sanaa ikiwemo tasnia ya filamu nchini livunjwe lakini kwa muda mrefu wasanii wakiwemo wa filamu na muziki wamekuwa wakililalamikia baraza hilo kuwa linafanya mambo kienyeji na baadhi ya wasanii kudai kukumbana na urasimu wanapotaka kufanya kazi zao za sanaa. Wengine wanadai hata hatua iliyopigwa sasa katika sanaa nchini ni juhudi za wasanii wenyewe pasipo sapoti ya kutosha kutoka BASATA. Baadhi ya wasanii wa filamu wamekuwa pia wakitaka TAFF ndiyo i