Posts

HUWEZI AMINI,HUU NDIO UTAJIRI WA MAJUMBA YA KIFAHARI YA MCHEZAJI MRISHO NGASA ,JIONEE MWENYEWE HAPA

Image
SASA ni miaka nane tangu aanze kucheza soka ya ushindani mwaka 2005 katika klabu ya Kagera Sugar ya Bukoba, lakini kwa namna alivyopanga vyema karata zake, Mrisho Khalfan Ngasasa anafurahiamaisha ya mpira.  Huwezi kumuita tajiri, lakini huwezi kuacha kumpa heshima miongoni mwa wachezaji wakizazi chake, kwamba amewaacha mbali. Amecheza klabu nne katika Ligi Kuu tu, baada ya Kagera Sugar ni Yanga SC mwaka 2007 hadi 2010, Azam 2010 hadi 2012,Simba SC 2013 na sasa amerejea Jangwani. Hakuna maslahi makubwa aliyopata Bukoba, zaidi alikuwa anatafuta njia ya kutokea katika soka ya Tanzania na tangu Yanga SC hadi sasa unaweza kusema Mrisho ametumia kipindi hicho kuchanga vyema karata zake.  Anamiliki nyumba tano, tatu zipo Mwanza na mbili Dar es Salaam- na ana gari nane, wakati huo huo akaunti yake wakati wote ikiwa ‘imefulia sana’ ina Sh. Milioni 20. Akiwa bado anategemea soka kama ajira yake, Ngassa amekwishaanza kujipanga kwa maisha ya baada ya soka na

ANGALIA PICHA ZA MAANDALIZI YA SWALA YA EID MOROGORO ASUBUHII HII

Image
 Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislamu wakijipatia mahitaji muhimu kabla ya swala ya Eid Mkoani morogoro asubuhi  Baadhi ya waumini wa Dini ya Kiislamu wakiwa wamekusanyika tayari kuswali swala ya Eid katika viwanja vya Islamic Foundation Mjini Morogoro asubuhii hii at Thursday, August 08, 2013 Email This BlogThis! Share to Twitter Share to Facebook No comments: Post a Comment PATA MATUKIO YOTE HAPA:NAKUOMBA LIKE PAGE YETU YA FACEBOOK HAPA KUPATA ZAIDI

SAKATA LA MFANYABIASHARA WA MADINI ALIYEPIGWA RISASI 6 JIJINI ARUSHA

Image
  Habari zilizopatikana majira ya saa kumi kasoro robo alasiri ya leo zinafahamisha kuwa, Mfanyabiashara maarufu wa madini mkoani Arusha na mmiliki wa hoteli amepigwa risasi na watu wasiojulikana katika eneo la Mijohoroni upande wa kulia (punde tu baada ya Boma Ng’ombe ukitokea Moshi kuelekea Arusha), mchana wa leo, alipokuwa ameitikia wito alioitiwa wa mazungumzo ya kibiashara ya madini. Taarifa zinasema marehemu amepigwa risasi kati ya 6 - 12 katika paji la uso na maeneo mengine ya mwilini.   Mtu mmoja aliyewahi kufika kwenye eno la tukio baada ya kusikia milio ya risasi anasema alimkuta mtu mmoja wa fanani ya Kimasai ambaye alishuhudia tukio zima na kumsimulia kuwa aliona watu wanapiga risasi na kisha wakaondoka kwa pikipiki kuelekea porini huku akielekeza mkono kuonesha walikokimbilia. Polisi wanaendelea na uchunguzi baada ya kuuchukua mwili wa marehemu kutoka kwenye eneo la tukio na kuupeleka hospitalini. Mwili wa marehemu upo katika chumba cha kuhifadhia m

SKENDO YA KUMPIGA RIHANNA YAMKERA CHRISS BROWN...ANADAI KACHOKA KUANDIKWA VIBAYA NA ANAFIKIRIA KUACHA MUZIKI

Image
  Chris Brown anafikiria kuachana kabisa na muziki siku za usoni na amesema huenda X ikawa albam yake ya mwisho.  Breezy ametumia akaunti yake ya Twitter kuelezea kuchoshwa na kuandikwa vibaya kila kukicha kutokana na kosa alilolifanya akiwa na miaka 18 la kumpiga aliyekuwa mpenzi wake Rihanna.   Wataalamu wa mambo wanasema Chris Brown ameandika hivyo kutokana na msongo wa mawazo alionao hivi sasa kwasababu anahusishwa sana na mambo ya mahakamani.  Mtandao mmoja wa huko Marekani umeandika kwamba Chris Brown alikaa jela kwa muda wa dakika 45 kabla ya mambo kukaa sawa na baadae kutolewa. Hizi ni tweet nyingine ambazo aliandika akiwa katika wakati huo mgumu.

SABABU MBILI ZILIZOMFANYA MADAM RITA AIHAMISHIE BONGO STAR SEARCH TBC1

Image
  Epiq Bongo Star Search ya mwaka 2013 haitaoneshwa tena kupitia ITV. Mwaka huu shindano hilo la kusaka vipaji vya kuimba litakuwa likioneshwa kupitia TBC1.  Kupitia Facebook, Rita Paulsen aka Madam Rita ambaye ni mwanzilishi na jaji mkuu wa shindano hilo ametoa sababu mbili za kuhamisha matangazo hayo kutoka ITV hadi TBC1. “Baada ya kusoma maoni yenu, ningependa kufafanua sababu mbili za kurusha Epiq Bongo Star Search 2013 kupitia kituo cha Televisheni cha TBC1.  Kwanza kabisa ni sababu za kibiashara ndio zimepelekea kipindi cha EBSS kurushwa kupitia TBC1 na sababu ya pili ni kwamba baada ya kwenda kidigitali, TBC1 sasa inapatikana kwenye ving’amuzi karibia vyote vikiwemo Star Times, DSTV na Zuku.”

DUDU BAYA ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUCHOMA MOTO NYUMBA YA MSANII MWENZAKE

Image
MSANII wa Bongo Fleva, Godfrey Tumaini ‘Dudu Baya’ ameswekwa rumande kwa kudaiwa kuchoma nyumba ya baba wa msanii mwenzake ‘Geez Mabovu’, Mashaka Mrisho. Tukio hilo lilitokea Agosti 1, mwaka huu ambapo mwenye nyumba sambamba na polisi walimkamata Dudu Baya na mkewe Mariam kwa madai ya kuchoma moto nyumba kwa makusudi na kuwapeleka katika Kituo cha Polisi Oysterbay.   “Mkewe alitupia mkaa wa moto katika sofa, likashika moto kabla majirani hawajanisaidia kuuzima. Baada ya kuwauliza kulikoni wakanitishia maisha ndipo nikawapeleka polisi na kupewa RB namba OB/RB/13485/2013 na kuja kumkamata,” alisema Mashaka.   Dudu Baya alipotafutwa na mwandishi wetu, alikiri kukamatwa na kuwekwa sero kwa saa sita kabla ya kuwekewa dhamana na shemeji yake aliyemtaja kwa jina la Vero. “Vyumba vyake na vyangu haviingiliani kabisa, tumetenganishwa na ukuta hivyo shutuma zake hazina ukweli dhidi yetu ila naamini uchunguzi wa polisi ndiyo utatoa majibu,” alisema Dudu baya.  ...

PICHA ZA NUSU UCHI ZA RIHANNA KATIKA TAMASHA LA CROP OVER 2013

Image
  Taswira juu na chini zinamuonesha Mwanamuziki Robyn Rihanna Fenty 'Rihanna' akijiachia na ndugu, jamaa na marafiki katika tamasha la kila mwaka la 'Crop Over Carnival' lililofanyika nyumbani kwao Barbados.

CCM BADO INA IMANI KUBWA NA TUME YA KATIBA

Image
Nape Nnauye NA MWANDISHI WETU CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) kimesema bado kina imani na Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini, katika mchakato unaoendelea wa kupata katiba mpya. Imesema licha ya CCM kutofautiana kimawazo katika baadhi ya maeneo katika rasimu ya kwanza ya  katiba iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, lakini haina ugomvi na tume hiyo. Hayo yamesemwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Sekretarieti, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.  "Tunawaheshimu sana wajumbe wa tume hii, na kwa kweli tunamatumaini nao sana kuwa watatimiza wajibu wao kwa weledi mkubwa", alisema Nape. Nape alibainisha kwamba  pamoja na maeneo mengine ya rasimu ya kwanza ya katiba ,  CCM ina mawazo tofauti kwenye suala la Muundo wa Muungano ambapo wakati rasimu inapendekeza muundo wa serikali tatu, CCM yenyewe inapende

MTOTO WA USHER RAYMOND ALAZWA ICU MAUTUTI KWA AJALI

Image
Usher 's son  Usher Raymond V  is in the ICU at an Atlanta hospital after a serious accident in the singer's pool Monday, source has learned. Sources tell source, the accident occurred around 6 PM yesterday. Usher was not home at the time. Here's what we know.   The child was playing in the pool with his aunt and saw a toy in the drain.  He dove down to get the toy and his arm got stuck in the drain.  The aunt immediately dove in to rescue him but couldn't get his hand out.  The maid then dove in and tried but was also unsuccessful. The maid screamed for help.  Two men working in the house came out, dove in and freed the boy.  He was given CPR immediately and rushed to the hospital.  Usher arrived and drove in the ambulance with his son. 5-year-old Usher Raymond V is the oldest of Usher's two sons with ex-wife Tameka Raymond. We're told Usher and Tameka are cu

BILIONEA AMTWANGA RISASI MFANYABIASHARA WA MADINI ARUSHA

Image
JIJI la Arusha na Mkoa wa Manyara, hali ya hewa ilishachafuka, wingu zito limefunika kufuatia kuuawa kwa kupigwa risasi, mfanyakazi wa Kampuni ya Tanzanite One, Onesmo William Mushi (pichani). Mtuhumiwa wa mauaji hayo ni bilionea wa madini, mkazi wa Arusha, Joseph Mwakipesile ‘Chusa’ ambaye ni mfanyabiashara anayemiliki migodi, Mererani wilayani Simanjiro, Manyara.NA GLOBAL PUBLISHER ONESMO ALIVYOUAWA Habari zimedai kwamba Onesmo akiwa eneo lake la kazi, mgodini chini, alipigwa risasi mbili kifuani ambazo ziliondoa uhai wake. Tukio hilo lilitokea saa 8 usiku, Julai 20, mwaka huu, chanzo kikitajwa kwamba ni mgogoro wa kugombea madini. Imedaiwa kuwa Onesmo, akiwa na wafanyakazi wenzake wa Tanzanite One ambao wamefahamika kwa jina mojamoja, Kennedy na Leonard, walikutana na wachimbaji wadogowadogo hivyo kutokea mvutano wa kimaslahi. Habari zimedai kwamba miongoni mwa wachimbaji hao wadogo, alikuwepo Chusa ambaye ndiye a

TEKNOLOJIA MPYA KUOKOA MAZAO YANAYOPOTEA

Image
  Na Mahmoud Ahmad,Arusha. Uhifadhi duni na mbovu wa mazao husababisha wakulima kupoteza aslimia 5%ya mazao yao  kuanzia shambani kabla ya kuvunwa na kusafirishwa hadi kwenye masoko Hayo yameelezwa na Msimamizi wa kituo cha kueneza teknolojia ya kilimo kanda ya kaskazini (ATTC)  Ernest Elias alipokuwa akizungumzia teknolojia mpya ya mavuno  ambayo wanayoonyesha katika maonyesho ya nane nane mwaka huu yanayofanyika katika viwanja vya Taso vilivyoko kata ya themi jijini hapa Ernest Elias amesema kuwa teknolojia hiyo mpya ambayo wameionyesha kwa mara ya kwanza katika maonyesho hayo itawasaidia wakulima kuvuna kwa urahisi na kufungasha wakiwa huko huko shambani kwa namna ambayo haitaruhusu upotevu wa mazao hata wakati wa usafirishaji na masokoni pia. Elias alisema kwa wastani  Mkulima akivuna gunia 10 anapoteza gunia 1 kutokana na  ubovu wa uhifadhi  wa mazao na mfumo mzima hadi kumfikia mhitaji sokoni.