Posts

MAMA SALMA KIKWETE AKUTANA NA MAMA CHERRIE BLAIR NA AFUTURISHA VIONGOZI NA WANAKIJIJI CHA HOYOYO. IMG_7126

Image
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete na mgeni wake Mama Cherrie Blair wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA, mara baada ya kufanya mazungumzo yao. Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akifanya mazungumzo na Mama Cherrie Blair, Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu wa Uingereza walipokutana kwenye ofisi za WAMA tarehe 23.7.2013 Mama Blair yupo nchini akifuatana na mumewe Tonny Blair katika ziara ya kikazi. ke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa nasaha zake baada kuwafuturisha viongozi wa serikali, madhehebu ya dini wa wilaya ya Mkuranga na wananchi wa kijiji cha Hoyoyo kilichoko karibu na Mkuranga katika Mkoa wa Pwani tarehe 23.7.2013.  NA FULLSHANGWE BLOG ke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa nasaha zake baada kuwafuturisha viongozi wa serikali, madhehebu ya dini wa wilaya ya Mkuranga na wananchi wa kijiji cha Hoyoyo kilichoko karibu na Mkuranga katika Mkoa wa Pwan

IRENE UWOYA NA LUCY KOMBA WASHIKANA UGONI

Image
NYOTA wa filamu za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krrish’ ametoa kali ya mwaka baada ya kudai kwamba amemshika ugoni msanii mwenzake, Lucy Komba mara baada ya kuziona picha za msanii huyo akiwa na mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ wakiigiza filamu. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu kutokea nchini Swaziland, Uwoya amepinga vikali utetezi unaosemwa kwamba Lucy na Kataut walikuwa wakishuti filamu na anaamini kuwa msanii huyo ameamua kumzunguka na kutaka kuibomoa ndoa yake. “Lazima kuna kitu kinaendelea kwani katika dunia hii sijawahi kuona filamu inayochezwa na watu wawili tu mwanzo mpaka mwisho, ninachotaka kusema  ni kwamba Lucy ana mpango wa kuiharibu ndoa yangu,” alisema Uwoya kwa hasira. Uwoya amehoji usiri wa filamu hiyo na kila alipokuwa akimpigia simu mumewe alikuwa akimjibu kwamba yuko Rwanda kumbe alikuwa Bongo akiigiza filamu na Lucy.   “Kwanza Lucy ashukuru niko mbali, laiti ningekuwa karibu angenieleza vizuri kwa sababu

KAHABA LANASWA LIKIFANYA NGONO KATIKA MAKABURI YA MALAPA BUGURUNI

Image
LICHA ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani watu wengi kuogopa kufanya maovu, jimama anayekwenda kwa jina la Joyce Benson (34), amefumwa akifanya ngono katika makaburi ya Malapa, Buguruni jijini Dar. Joyce amekamatwa usiku wa kuamkia Alhamisi iliyopita saa nane katika maeneo hayo akifanya biashara haramu ya kuuza mwili wake katika makaburi hayo kwa njia ya kujipatia fedha.   Joyce mwenye umbile la miraba minne alipatwa na fedheha kubwa baada ya majirani zake kusikia habari hizo na kuanza kumlaani. Mbali na Joyce pia siku hiyo machangudoa wengine 14, waliokuwa wakifanyia vitendo vya ukahaba kwenye makaburi hayo walikamatwa. Joyce na wenzake hao walifikishwa katika Mahakama ya Jiji (Sokoine Drive) ili sheria ifuate mkondo wake. Wakiwa mahakamani hapo, mwendesha mashitaka wa mahakama hiyo, Richard Magodi aliwasomea tuhuma za kufanya ukahaba na kumfanya hakimu wa mahakama hiyo, Timoth Lyon kupigwa na butwaa. Hata hivyo, Joyce na wenzake walikana kufanya kosa hilo ambapo

RAIS KIKWETE AINGILIA KATI KODI ZA LINE.....

Image
HATMAYE RAIS KIKWETE AMEZITAKA MAMLAKA HUSIKA ZIKUTANE HARAKA ILI TATIZO LIISHE Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameagiza Wizara za Serikali zinahusika na kodi na mawasiliano pamoja na makampuni ya simu za mikononi nchini kukutana mara moja kutafuta jinsi gani ya kumaliza mvutano wa kodi mpya ya kadi za simu hizo za mikononi. Rais kikwete ametoa maelekezo hayo jioni ya leo, Jumanne, Julai 23, 2013 wakati alipokutana na viongozi wa Wizara ya Fedha, Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia na wawakilishi wa makampuni ya simu ya TTCL, Airtel, Vodacom, Tigo na Zantel katika kikao cha pamoja kilichofanyika Ikulu, Dar es Salaam. Rais Kikwete amesema kuwa lengo kuu la mkutano huo wa pamoja kati ya Wizara hizo za Serikali na makampuni ya simu yawe ya kupendekeza jinsi gani ya kuziba pengo la Sh. Bilioni 178 ambazo zitapotea katika Bajeti iwapo kodi hiyo kwa kadi za kuongelea za simu za mikononi italazimika

VAZI LA NUSU UCHI LAZUIA NDOA KUFUNGWA JIJINI DAR....PADRI AGEUKA MBOGO NA KUWATIMUA WAPAMBE

Image
KIVAZI cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri. “Ninatoa dakika 10 kwa aliyeingia na mavazi ambayo hayatakiwi kanisani humu kutoka mara moja akavae vizuri, la sivyo ndoa yao haitafungwa,” alisema Padri Haule wa Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam. Awali vurugu hizo zilizotokea Jumamosi iliyopita, zilianzia nje, wakati Katekista wa Parokia hiyo, Yohane Maboko, alipotangazia wanandoa na ndugu zao waliokuwa mabega wazi au kuvaa nguo fupi, kutafuta nguo za kujifunika au wasiingie kabisa kanisani. Maharusi walikubali kutekeleza ombi hilo, wakavishwa vitambaa mabegani vya rangi tofauti na gauni jeupe la harusi, wakaruhusiwa kuingia kanisani, tayari kufunga pingu zao za maisha. Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa maharusi hao ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alipotaka kulazimis

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar lakamata silaha 7 na majambazi 8 na pia lakanusha Mh. Mnyika kukoswa na bomu.

Image
  Baadhi ya askari polisi wakionyesha kwa waandishi wa habari silaha zilizokamatwa kutoka kwa watuhumiwa wa matukio ya ujambazi. DCP Mlege akitoa taarifa ya mafanikio ya Jeshi hilo kwa waandishi wa habari ambapo akizungumzia suala la Mh. Mnyika amesema askari No. E. 5340 D/CPL Julius aliyekuwa ndani ya gari la polisi PT. 1902 alikuwa anasogeza boksi lenye mabomu ya kutoa machozi ya kurusha kwa mkono, kwa bahati mbaya bomu hilo lililipuka ndani ya gari hilo na halikuleta madhara yeyote kwa askari polisi wala raia waliokuwa eneo la uwanja wa Sahara uliopo Mabibo ambako chama cha CHADEMA kilikuwa kifanye mkutano wa hadhara tarehe 21 Jula 2013 kinyume na utaratibu. Jeshi la Polisi Kanda maalum Dar es Salaam limefanikiwa kukamata sila 5 ikiwemo SMG moja, Shortgun mbili, Riffle Mark 3 tatu, Pisto moja, Risasi 56, Maganda ya Risasi 17 na Majambazi 8. Akizungumza na vyombo vya habari jijini Dar es Salaam kwa niaba

RAIS KIKWETE LEO AKUATANA NA VIONGOZI MBALIMBALI IKULU

Image
RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA RAIS WA MPITO WA WA MADAGASCAR IKULU   Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais wa serikali ya mpito ya Madagascar Mhe Andy Rajoelina Ikulu jijini Dar es salaam leo Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza  Rais wa serikali ya mpito ya Madagascar Mhe Andy Rajoelina baada ya mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es salaam leo . RAIS JAKAYA KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA UINGEREZA LEO IKULU Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Mhe. Tony Blair Ikulu jijini Dar es salaam leo  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Mhe. Tony Blair Ikulu jijini Dar es salaam leo Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimwonesha mandhari mbalimbali Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Mhe. Tony Blair Ikulu jijini Dar es salaam leo  Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiagana na Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Mhe.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA MAKAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Image
 Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitambulishwa kwa wajumbe wa Chama cha  Makampuni ya Simu za mkononi na Bw. Manoj Kohli wa Airtel ambaye pia ni Mkurugenzi wa Pamoja wa chama hicho alipokutana nao kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 23, 2013   Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Bi Beatrice Singano, mmoja wa wajumbe wa Chama cha  Makampuni ya Simu za mkononi alipokutana nao kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 23, 2013 Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na maofisa waandamizi wa Wizara ya pamoja na  wajumbe wa Chama cha  Makampuni ya Simu za mkononi alipokutana nao kwa mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 23, 2013.PICHA NA IKULU

KASI YA MAAMBUKIZI YA VVU/UKIMWI YAPUNGUA HALMASHAURI YA MOSHI

Image
Kasi ya maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi imepungua katika Halmashauri ya Moshi baada ya kuanzisha kampeni za kuhamasisha jamii kupima afya zao kwa hiari kwa kutumia vikundi mbalimbali vya sanaa za maonyesho . Mratibu wa UKIMWI wa Halmashauri ya Moshi Benedicto Rwamuruku amesema ,kampeni hiyo wamaeanzisha baada ya kuona mafanikio ya elimu iliyotolewa awali  kwa njia ya sinema imewafikia jamii na maambukizi yamepungua. Aidha ameongeza kuwa maambukizi hayo yamepugua kutoka wastani wa asilimia 1,6 hadi kufikia asilimia 1.3 miaka mitaano iliyopita na lengo likiwa ni kuhakikisha kuwa maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi  hayaogzeki kwani Tanzania bila ukimwi inawezekana.

YUSUF MLELA AFUNGUKA KUMRITHI SAJUKI KWA WASTARA

Image
Jul 23 2013 BAADA ya wiki iliyopita kumleta kwenu staa wa filamu za Kibongo, Yusuf Mlela ili mumuulize maswali, leo tunawaletea majibu na ufafanuzi wa maswali mliyomuuliza. SHUKA NAYO… HUYU ANAMKUBALI Mimi ninakukubali kinoma kwa sababu huna majivuno wala skendo kwa hiyo kaka endelea hivyohivyo. Calvin Mabula, 0719371176 MLELA: Asante. ONGEZA UBUNIFU Nakupa hongera kwa uigizaji wako lakini pia ongeza ubunifu, skendo usizipe nafasi hazitakujenga bali zitakubomoa. Kelvin Mwaibula, 0713644447 MLELA: Asante kwa ushauri wako nitaufanyia kazi. YEYE NA WASTARA Mlela umeanzia mbali enzi zile ukiwa bado chalii, nakuombea heri uendelee kuwa nyota, fafanua kuhusu uhusiano wako na Wastara (Juma) maana tayari watu wanasema unataka kumrithi (Juma Kilowoko (Sajuki). Rocky, Moshi, 0715289337 MLELA: Wastara ni mtu wangu wa karibu sana tangu Sajuki akiwepo, tunafanya kazi

WALIOWAUA WANAJESHI WA TANZANIA WATAJWA.....NI KUNDI LA "JANJAWEED" LINALOUNGWA MKONO NA SERIKALI YA SUDAN

Image
WAKATI miili ya wanajeshi saba ikiwa imeagwa jana katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, imeelezwa kuwa kundi la Janjaweed linaloungwa mkono na serikali ya Sudan ndilo lililowavamia na kuwaua askari hao nchini humo  na kuwajeruhi wengine 17 . Wanajeshi hao wa Tanzania ambao walikuwa ni sehemu ya Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), walifanyiwa unyama huo Julai 13, mwaka huu katika eneo la kusini mwa Darfur, nchini Sudan. Kiongozi wa moja ya makundi ya wapiganaji la Sudan Liberation Movement (SLM), Minni Mannawi ameibuka na kuwatuhumu wanamgambo wa Janjaweed wanaoungwa mkono na serikali ya nchi hiyo na ametaka ufanyike uchunguzi wa kimataifa. Katika mahojiano yake na Gazeti la Sudan Tribune alipokuwa anahudhuria mkutano wa majadiliano kuhusu namna ya kupata amani ya kudumu nchini Sudan uliofanyika jijini Geneva Uswisi wiki iliyopita, alikanusha kuwa kundi lake linahusika na shambulio hilo.   “Tuna uhakika shambu

VIJANA WAUANA JIJINI MBEYA WAKIGOMBANIA PENZI LA MSICHANA

Image
Mnamo tarehe 21/07/2012 majira ya saa 23:30hrs huko kijiji cha Nkwangu wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, Seni s/o Sandu, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu aliuawa kwa kupigwa fimbo kichwani na Tolo s/o Seko, miaka 20, Msukuma, mkulima na mkazi wa Nkwangu. Chanzo ni ugomvi wa kumgombania msichana aitwaye Holo d/o Kulwa, miaka 16, Msukuma mkulima na mkazi wa Nkwangu. Mtuhumiwa amekamatwa na taratibu za kumfikisha mahakamani zinaandaliwa. Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya kamishna msaidizi wa polisi diwani athumani anatoa wito kwa jamii kutojichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na kudhibiti hasira zao kwa kuyatatua matatizo ya kimapenzi kwa njia ya mazungumzo ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza. Signed by, [Diwani Athumani – ACP] kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya.  Source: Watemi

WANAOPINGA KODI YA LINE ZA SIMU NI WANAFIKI WASIOPENDA MAENDELEO.

Image
  Wakati Serikali ikiahidi kutazama upya tozo ya Sh 1,000 kwa laini za simu ili kupunguza mzigo kwa wananchi, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini. Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma, baada ya kuutembelea mkoa mpya wa Njombe. “Ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petroli, ambayo imetupa fedha nyingi kwenye Mfuko wa Barabara, za kuunganisha miji na mikoa na nyingi zimejengwa na zinaendelea kujengwa. “Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vid ogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema,” alisema Pinda. Bunge la bajeti lililomalizika mwezi uliopita, lilipitisha tozo ya

POLISI WAFANIKIWA KUMKAMATA MVUTA BANGI ANALIYEMUUA MDOGO WAKE KWA KUMKATA MAPANGA HUKO SINGIDA

Image
 Jeshi la polisi mkoa wa Singida limefanikiwa kumkamata Elibariki Alphoce (21) mkazi wa kijiji cha Kizega wilaya ya Iramba, anayetuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam (9) mwanafunzi wa darasa la pili katika shule ya msingi Kizega. Elibariki anatuhumiwa kumuua mdogo wake Mariam Julai 16 mwaka huu katika kijiji cha Kizega kwa kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili na kisha kuteganisha kichwa na kiwiliwili. Ilielezwa kuwa Elibariki ni mtumiaji sugu wa madawa ya kulevya aina ya bangi. Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida ACP Geofrey Kamwela, amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa Julai 18 mwaka huu akiwa amejificha kando kando ya mto Ruruma wa kijiji cha Ruruma tarafa ya Kiomboi. 

DIAMOND PLATNUM AZUNGUMZIA KIFOCHAKE SOMA HAPA

Image
Msanii anayefanya vizuri sana kwa sasa Afrika mashariki Nasib Abdul aka Diamond Platnumz amezungumza maneno mazito aliyokiri huwa yanamtoa machozi, ni mambo yanayohusiana na ‘kifo chake’!. Dakika chache zilizopita hit maker huyo wa ‘Kesho’ ame post picha Instagram yenye sura yake na maswali yanayouliza nini kitatokea baada ya kifo chake. Tazama picha hiyo inazungumza yenyewe Picha hiyo ilisindikizwa na caption hii “One of my songs,always gets me crying whenever I listen to it, how I wish u would hear it, but then again I have no clue as to when I will release it… #WCB” Platnumz amekaa kimya bila kutoa wimbo mpya kwa muda sasa, je unahisi kuna uwezekano ‘KAMA NIKIFA KESHO’ ukawa ndio ndio wimbo mpya anaotegemea kuachia hivi karibuni? Tusubiri tuone!

HUU NDO MWONEKANO MPYA WA JOKATE MWEGELO

Image
TUPE MAONI YAKO KWA KUJIUNGA NASI KATIKA UKURA WA FACEBOOK

LWAKATARE KWENDA INDIA KUTIBIWA

Image
Mahakama yaridhia Lwakatare kwenda India kwa matibabu Mkurugenzi wa Usalama wa Chadema, Willifred Lwakatare akizungumza kuhusu hali ya ugonjwa wake akiwa katika Tasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) jijini Dar es Salaam jana.Picha na Fidelis Felix  Na James Magai,Aziza Masoud  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imempa kibali Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare, akatibiwe nje ya nchi. Lwakatare ambaye anasumbuliwa na maumivu ya shingo, kwa sasa amelazwa katika Taasisi ya Mifupa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) kwa uangalizi maalumu na kufanya mazoezi, alipata kibali hicho kwa kuwa anakabiliwa na kesi ya kula njama za kumdhuru Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky. Wakili wake, Nyaronyo Kicheere alililiambia gazeti hili nje ya mahakama kuwa Lwakatare anatarajiwa kupelekwa India, lakini akasema tarehe ya kusafi