Posts

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI LAAPISHWA MISRI

Image
Rais wa mpito wa Misri ameliapisha baraza lake jipya la mawaziri huku akiwapa nafasi viongozi wenye msimamo wa kati na pia akiwajumuisha wanawake wawili kwenye Serikali mpya. Serikali mpya inaongozwa na waziri mkuu, Hazem el-Beblawi ambaye kwa taaluma ni mchumi, Abdel-Fattah al-Asisi ambaye ataendelea kushikilia nafasi yake ya waziri wa ulinzi na pia Kama naibu waziri mkuu wa kwanza. Waziri wa masuala ya ndani ambaye aliteuliwa na rais aliyepinduliwa, Mohamed Ibrahim ataendelea kushikilia wadhifa wake, huku Nabil Fahmy ambaye aliwahi kuwa balozi wa Misri nchin Marekani, sasa atakuwa Kama waziri wa mambo ya nje. Akisisitiza kwanini baraza lake limejumuisha viongozi wenye msimamo wa Kati, rais wa mpito, Adly Mansour amesema amazingatia mahitaji ya nchi huku akitangaza nafasi tatu za wanawake kwenye baraza lake. Wizara walizopewa wanawake hao ni pamoja na wizara ya habari, wizara ya afya na wizara ya mazingira, uteuzi ambao unaonekana haukutar

Ujangili Tanzania! Tembo 475 wauwawa majangili 1215 wanaswa

Image
Na Suleiman Msuya WIZARA ya Maliasili  na Utalii kupitia Idara ya Wanyamapori imesema zaidi ya tembo 475 wameuwawa na majangili kwa kipindi cha mwaka 2012/13 ambapo watuhumiwa 1215 walikamatwa kwa makosa mbalimbali. Mkurugenzi wa Wanyamapori, Profesa Alexander Songoro pamoja na watuhumiwa hao pia jumla ya bunduki 85 na risasi 215 za aina mbalimbali zilikamwata na kesi 670 zilifunguliwa katika mahakama za hapa nchini, ambapo kesi 272 zimekamilika kwa washitakiwa 247 kulipa faini ya jumla ya  Sh175,002,420 na washitakiwa 71 kupewa adhabu ya vifungo vya jumla ya miaka 99. Alisema kesi 398 zenye jumla ya washitakiwa 897 bado zinaendelea katika mahakama mbalimbali nchini ambapo wanaamini kuwa zitakamilika hivi karibuni. "Kimsingi ndugu zangu wanahabari hali ya ujangili ni kubwa sana kwani kwa kipindi cha mwaka jana zaidi ya tembo 475 waliuuwawa hali ambayo inahitaji juhudi zaidi ziongezeke ili kukabiliana na hali hiyo," alis

MAMA BAGHDAD AMUOMBEA MSAMAHA MWANAE KWA CHID BENZ...AOMBA WAKUTANE PAMOJA NA NA WA MITEGO

Image
Baada ya jana Chidi Benz kuweka wazi kuwa hategemei kumsamehe Baghdad kwa ‘blunder’ aliyoifanya ya kuwashirikisha yeye na Nay wa Mitego bila kuwaambia, mama mzazi wa Baghdad amekuja hadharani na kumuombea msamaha mwanae. Mama huyo ameongea leo kwenye segment ya 255 kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM kuhusu nia yake ya kutaka kumaliza tofauti zilizopo kati ya mwanae na Chidi. Mama Baghdad amekiri kuwa mwanae hakutumia akili kuchukua uamuzi huo wa kuwashirikisha wasanii wanaofahamika kuwa na uadui mkubwa kimuziki bila kufikiria madhara yake. Amesema mwanae hakufanya jambo la busara na ndio maana ameamua kumpigia magoti Chidi ili ampe ‘second chance’ mwanae ambaye amejaribu kuomba msamaha bila mafanikio. 255 pia imezungumza na Chidi Benz aliyepo nchini Kenya kwa sasa ambaye amesema hawezi kukataa wito wa mama yake na Baghdad kwakuwa ni kama mama yake pia na amekubali kuja kukutana naye akirejea nchini. Jana wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Mambo Mseto

MZEE MAGALI WA BONGO MOVIE AKIMBILIA BONGO FLAVA

Image
Mwaka 2013 utakuwa na surprise nyingi sana... So far tumeshapata surprise kibao ikiwemo ile ya jana ya promoter na Mkurugenzi wa Watanashati Entertainment, Ostaz Juma na Musoma kuingia kwenye hip hop na kurekodi wimbo mmoja aliomshirikisha Young Killa. Surprise zinaendelea na sasa inakuja bombshell nyingine. Kwa mujibu wa mtangazaji wa Take One ya Clouds TV, Zamaradi Mketema, muigizaji wa filamu nchini maarufu kama Mzee Magali ametupa karata yake kwenye muziki. “Mzee magali augeukia mziki wa bongo fleva now.. sikiliza movie Leo siku ya KESHO on CLOUDS FM Radio ili usikie wimbo wake mpya kabisa wa kwanza ambao ameufanya SAA NNE na Dk 45 asubuhi,” ameandika Zamaradi kwenye Instagram.

PICHA ZA BEVERLY AKIWA BAFUNI KATIKA JUMBA LA BIG BROTHER

Image

MWENYEKITI WA HALMASHAURI AFARIKI DUNIA BAADA YA KUANGUKA CHOONI

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Laurent Hoya, amefariki dunia ghafla jana alfajiri baada ya kuanguka chooni . Kifo hicho kimetokea nyumbani kwa marehemu Nkuhungu katika Manispaa ya Dodoma. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana, Mkuu wa Wilaya ya Chamwino, Fatma Ally alisema Hoya ambaye alikuwa na tatizo la ugonjwa wa moyo, alianguka chooni jana alfajiri na kukutwa na mauti. “Tuliachana juzi saa 7.30 mara baada ya kikao, taarifa ya kifo chake nilizipata saa 11 alfajiri jana, ni kifo cha ghafla sana na halmashauri imempoteza mtu ambaye alikuwa mfano kwa jamii,” alisema. Hoya ambaye alikuwa Diwani wa Kata ya Mpwayungu, anatarajiwa kuzikwa kijijini kwake Mpwayungu kesho. Mkuu huyo wa Wilaya alisema alikuwa akishirikiana kwa karibu na Mwenyekiti huyo, kwani alikuwa kiongozi mwenye ushirikiano mkubwa na hakuwa mtu wa kukwepa kuitikia mwito. Alisema alikuwa akilima mazao yanayohimizwa katika mkoa wa Dodoma na shamba la

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA KATIKA ZIARA WIALAYANI TUNDURU

Image
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda  na mkewe Tunu (kushoto) wakisalimiana na Mkurugenzi wa  Kanisa la  Upendo wa Kristo Masihi  (KIUMA), Dr. Matomola Matola  (wapili kuli) baada ya kuwasili katika misheni hiyo kuweka jiwe la msingi la Chuo cha Elimu cha Misheni hiyo, Julai 15, 2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Waziri Mkuu,Mizengo Pinda  akizungumza  kabla ya kuweka jiwe la msingi la Chuo cha Elimu cha Kanisa la Upendo wa Kristo Masi (KIUMA) wilayani Tunduru akiwa katika ziara ya mkoa wa Ruvuma Julai 15, 2013. Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiweka jiwe la Msingi la Chuo cha Elimu cha Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi (KIUMA) wilayani Tunduru akiwa katika iara ya mkoa wa Ruvuma Julai 15,2013. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)   Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akizungumza na Mkrugenzi wa Kanisa la Upendo wa Kristo Masihi , Dr. Matomola Matomola kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Chuocha Elimu cha Kanisa hilo wilayni Tunduru akiwa katika ziara ya mkoa wa

CHEKA AONYWA KUCHEZA MECHI YA 'NDONDO'

Image
Bondia Francis Cheka OGANAIZESHENI ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO-Limited), imetahadharisha na kusisitiza kuwa bondia Francis Cheka 'SMG' hawezi kucheza pambano jingine lolote kabla ya kuvaana na Mmarekani Derrick Findley. Cheka na Mmarekani huyo wanatarajiwa kuvaana Agosti 30 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee kuwania mkanda wa WBF katika mchezo wa raundi 12 uzito wa Super Middle (kilo 75). Hata hivyo, kuna taarifa kwamba Cheka anayeshikilia taji la Mabara la IBF atapanda ulingoni mwanzoni mwa Agosti dhidi ya Mmalawi Chimwemwe Chiotcha katika pambano lisilo la ubingwa. Hata hivyo, Rais wa TPBO, Yasin Abdallah 'Ustaadh', alisema kwa mujibu wa mkataba na taratibu za ngumi, Cheka hawezi kucheza mapambano mawili ndani ya mwezi mmoja na hivyo kutoa tahadhari mapema. Ustaadh alisema Cheka alishasaini mkataba wa pambano hilo dhidi ya Mmarekani tangu Mei mwaka huu na kwa taratibu ndani ya mwezi mmoja hawezi kupigana

Kauli ya Ban K-Moon juu ya mauaji ya askari wa JWTZ Darfur

Image
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UNO), Ban K-Moon(pichani chini), amesema amesikitishwa na kuhuzunishwa na mauaji ya askari saba wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), lililofanywa na waa si wa Sudan Julai 13, mwaka huu. Askari hao wa JWTZ waliokuwa Darfur, Sudan ya Kusini kulinda amani kwa mujibu wa UNO, walishambuliwa na waasi hao karibu na kambi ya Manawashi eneo la Khor Abeche, mji wa Darfur Jimbo la Nyala ambapo pia askari wengine 17 walijeruhiwa baadhi yao vibaya. Katika salamu zake hizo kupitia kwa Msemaji wake, Katibu Mkuu huyo wa Uno, ameelezea masikitiko yake kuhusiana na vifo hivyo na kutoa pole kwa familia za marehemu waliokuwa wakilinda amani, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Vikosi vya Umoja wa Afrika kwa Umoja wa Mataifa vya Kulinda Amani (Unamid). Ban K-Moon amelaani shambulio hilo dhidi ya Unamid na kuelezea matumaini yake kwamba Serikali ya Sudan itachukua hatua zinazofaa kuhakikisha kwamba wahusika

DK MALASUSA: NCHI HAITAKUWA NA AMANI KWA KUONGEZA IDADI YA POLISI

Image
Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ), Askofu Dk.Alex Malasusa amesema nchi haitakuwa na amani kwa kuongeza idadi ya polisi bali amani itapatikan a kutokana na Watanzania kuheshimiana. Askofu Malasusa aliyasema hayo jana alipokuwa akiweka jiwe la msingi kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Faragha na maombi katika Kijiji cha Chasimba wilayani Bagamoyo kitakachojengwa kwa ushirikiano wa Usharika wa Dayosisi ya Kariakoo. “Nchi haiwezi kuwa na amani kwa kuongeza idadi ya polisi njia pekee ni kuheshimiana na kuheshimu madhehebu mengine ili kuendeleza amani,” alisema Dk.Malasusa. Aidha, alisema kituo hicho kitajengwa kumbi za kisasa za mikutano, zahanati, chuo cha ufundi, maktaba na nyumba ya faragha kwa ajili ya maombi na viwanja mbalimbali vya michezo. Katika ibada hiyo mgeni rasmi alikuwa ni Makamu wa Rais Dk.Gharib Bilal, lakini aliwakilishwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya

ANGALIA PICHA KILICHOJILI KWENYE MAZISHI YA BABA YAKE JOYCE KIRIA

Image
My Late Dad Michael Francis Iwambo Kiria, R.I.P Huyu ndo baba yangu aliyefariki dunia 10/7/2013 huko mkoani Tanga ambako alikuwa anaishi na familia yake. Katika kizazi cha Babu yangu mzaa Baba, anaanza Baba yangu mzazi kisha anafata huyu ambae ni Baba yangu mdogo (kwangu binafsi hana tofauti na baba mzazi kwa namna tulivyoishi nae enzi za uhai wake) HISTORIA Kwa miaka mingi sana kumekuwa na MGOGORO WA ARDHI kwenye familia yetu, na kila malumbano yakitokea yanayohatarisha AMANI ya Familia, Baba Michael Kiria pichani alisimama kidete kuhakikisha Amani inakuwepo. TAARIFA ZA MSIBA Siku ya Jumatano nilipokea kwa mshtuko mkubwa taarifa za msiba wa Baba aliyefia katika hospitali ya Mkoa Bombo, Kwa taarifa nilizopewa na mdogo wangu anaeitwa KIRI (Mwanae wa kwanza wa kiume) ni kuwa Baba alipata matatizo ya kupumua na katika harakati za kumkimbiza Hospitali alifia mapokezi mara baada ya kufikishwa katika Hospi