Posts

RAIS KIKWETE ATOA TAMKO RASMI KUHUSU MAUAJI YA ASKARI SABA WA TANZANIA WAKILINDA AMANI DARFUR SUDAN.

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameshtushwa na kuhuzunishwa sana na tukio la kushambuliwa na kuuawa kwa vijana saba hodari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania waliokuwa wanalinda amani katika eneo la Darfur, Sudan. Kwa hakika, Rais amesikitishwa sana na kitendo hicho ambako wanajeshi wengine 14 wa Tanzania wamejeruhiwa na waasi wa Sudan na ametuma salamu za rambirambi za moyoni mwake kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania na kwa familia za wafiwa wote. Aidha, Rais Kikwete anaungana na Watanzania wote na hasa maofisa na wapiganaji wa JWTZ na familia za wafiwa kuomboleza vifo vya vijana hao hodari wa Tanzania. Rais pia anaungana na Watanzania wote kuwaombea wale walioumia katika tukio hilo waweze kupona haraka na kuendelea na majukumu yao ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa. Katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinz

MBATIA AIPONDA RED BRIGADE YA CHADEMA

Image
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR- Mageuzi James Mbatia, amekikosoa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa kitendo cha kutangaza kujihami kwa kuboresha kikosi chao cha ulinzi na usalama cha Red Brigade, kwamba kufanya hivyo ni kushindana na serikali. Wakati Mbatia akisema hayo siku chache zilizopita Rais Jakaya Kikwete alitoa kauli yenye mwelekeo wa  kukiponda chama hicho juu ya mpango wake huo akisema kuwa mpenda amani haundi kikosi cha mgambo. Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, katika kikao cha Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, Mbatia alisema ushindani wa kisiasa unatokana na hoja za msingi na si kushindana kwa vitendo. “Kitendo cha Chadema kuunda kikosi chao ni sawa na kushindana na serikali kwani jeshi linatakiwa kudhibitiwa na serikali na si kila chama wala kabila, kwa sababu kufanya hivyo ni kupoteza amani ya nchi,”alisema Mbatia. Alisema kuwa chama cha NCCR- Mageuzi, kitaendele

MATOKEO YA UCHAGUZI WA UDIWANI KATIKA KATA NNE JIJINI ARUSHA

Image
THEMI CDM -678 CCM-326 CUF-313 KIMANDULU CDM-2665 CCM-1169 KALOLENI CDM-1019 CCM-389 CUF-169 ELERAI CDM-1715 CCM-1239 CUF-213

ANGALIA PICHA YA HALI ILIVYOKUA JANA JIJINI ARUSHA WAKATI WA UCHAGUZI MDOGO WA MADIWANI KATIKA KATA 4

Image
 Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.  Polisi wakimsihi Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari  aondoke nje ya kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu,pamoja na makada wa CCM hawako pichani ambapo walitakiwa kukaa mita 200 badala ya mita 100.  Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu.  Makarani wa uchaguzi wakiingiza masanduku ya kura katika ofisi ya kata ya Kimandolu kutoka  kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi kimandolu.   Polisi wakiimarisha ulinzi katika lango kuu la kuingilia  kituo cha kupigia kura cha Ofisi ya kata ya Kimandolu katika uchaguzi ulifanyika leo mjini Arusha.   Mkazi wa kata ya kima

PICHA ZA AJALI YA FUSO BAADA YA KUGONGANA NA BASI LA METRO COACH LEO MOSHI

Image
  Huu ni upande wa mbele wa fuso iliyopata hitilafu katika breki na kusababisha ajali.  Hii ni fuso iliyokuja kuchukua (kufaulisha) mzigo uliokua kwenye fuso iliyopata ajali. NA  http://kingjofa.blogspot.com Baadhi ya watu wakiwa katika eneo la ajali wakifaulisha mzigo wa ndizi katika fuso nyingine.   Aliyesimama ni team leader wa #team KINGJOFA akiwa anamujulia hali kondakta wa basi la Metro coach katika hospitali ya rufaa ya KCMC iliyopo mjini Moshi.  Kulia ni King jofa akiwa akipata katika eneo la ajali akipata maelezo kutoka kwa kondakta wa fuso aliyejitambulisha kwa jina la Remeni, muda mfupi baada ya kondakta huyo kuruhusiwa kutoka hospitali.  Haya ni mabaki ya fuso iliyogongana na basi la Metro coach maeneo ya kawawa road nje kidogo ya mji wa Moshi.  Haya ni mabaki ya ndizi yaliyotoka kwenye fuso iliyopata ajali.  Huyu ni dereva wa fuso  Godluck maarufu kama Mmasi akiwa amelaz

RAIS KIKWETE AWATUNUKU KAMISHENI MAAFISA WA JWTZ CHUO CHA MAFUNZO YA KIJESHI MONDULI, LEO

Image
   Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiingia katika uwanja wa gwaride wa Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, tayari kwa kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ leo Julai 13. Pamoja naye ni Mkuu wa Chuo hicho Meja Jenerali V.K. Mritaba. Jumla ya wahitimu 205, wakiwemo wanawake 25, wametunukiwa kamisheni na kuwa Luteni Usu, ambapo wahitimu wawili ni wa kutoka Uganda na Visiwa vya Shelisheli.   Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua  gwaride katika  Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  leo. ZAIDI BOFYA HAPO CHINI   Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Rais Jakaya Mrisho Kikwete  akimpa zawadi  Ofisa Kadet  Ngodoke kwa kuibuka mwanafunzi bora wa jumla mwaka huu katika Chuo Cha Mafunzo ya Kijeshi (TMA) Monduli, Arusha, kabla ya kutunuku kamisheni kwa Maafisa wa JWTZ  leo Jul

RAY C AZIDI KUPENDEZA, MASHABIKI WAZIDI KUMSHANGAA..

Image
Mwanamuziki staa wa Bongo Fleva, Rehema Chalamila ‘Ray C’ ambaye amepotea katika anga la muziki kwa kipindi kirefu kutokana na matatizo ya matumizi ya madawa ya kulevya, amejitokeza akiwa amefutuka. Hivi karibuni, Ray C ameibuka na kuanza kutundika picha na vipande vya video zake katika kurasa zake kwenye mitandao ya kijamii, ikiwa ni sehemu ya kujiweka karibu na mashabiki wake. Kufuatia ishu hiyo, kumeibuka mshtuko mkubwa kwa baadhi ya watu kutokana na picha hizo kumuonesha ‘bidada’ akiwa amenenepeana ghafla tofauti na alivyozoeleka. UNENE UNATOKANA NA DOZI? Baadhi ya mashabiki wake katika mtandao wa Instagram walidai kuwa inawezekana unene huo unatokana na dozi ya kuacha ‘unga’. Hata hivyo, wengine walimshukuru Mungu kwa kuwa sasa afya ya mwanadada huyo inaonekana kurudi katika hali yake ya kawaida tofauti na miezi kadhaa aliporipotiwa na gazeti hili akiwa amezimika kutokana na matumizi ya unga. AFUT

PICHA MBALI MBALI ZA KINACHOENDELEA KWENYE MSIBA WA MAMA YAKE PROF J MBEZI YA KIMARA

Image
dolo na nature Juma nature akimpa pole prof j NA  http://phars.blogspot.com/

"RED BRIGED NI LAZIMA IANZISHWE...MBONA CCM NA CUF WANA KUNDI LAO?"...CHADEMA

Image
  SINGO BENSON Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema hakitarudi nyuma katika mpango wa kutoa mafunzo ya ukakamavu kupitia kikundi chake cha red brigade. Chama hicho kimesema, tayari Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF), vyote vikiwa miongoni mwa `vyama vikubwa nchini’, vina vikundi vya aina hiyo.   Mkurugenzi wa Oganizasheni na Mafunzo Chadema, Singo Benson, ametoa msimamo huo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam. Tamko la Chadema kuanzisha mafunzo hayo, limeibua taharuki na kusababisha watu kadhaa akiwamo Rais Jakaya Kikwete, kutaka mpango huo usitishwe. LENGO LA MAFUNZO Benson alisema lengo la kuimarisha kikundi hicho, ni kujikinga dhidi ya mashambulizi yanayoelekezwa kwa viongozi, wanachama na wafuasi wake, ambapo CCM ikitajwa kuwa nyuma ya mashambulizi hayo. Alisema Chadema, imekamilisha maandalizi ya mafunzo yatakayowajumuisha zaidi vijana, ili wapate mbinu za kujikinga na kuwa