
Kala Jeremiah na Ommy Dimpoz Watisha Kili Awards Wajizolea Tuzo za Kumwaga Mwaka huu umekuwa mwaka mzuri zaidi kimuziki kwa msanii toka rock City Mwanza Kala Jeremiaha ambae maombi yake kwa āDear Godā yamesikika na amepata majibu kwa njia ya kipekee na wimbo wake āDear Godā umeweza kuchukua tuzo tatu katika Kilimanjaro Music Awards 2013. Kala Jeremiah ametumia mkuki mmoja kunasa āswalaā wake watatu muhimu mwaka huu, Dear God imeweza kumpa nafasi kubwa na kushinda tuzo katika kipengele cha wimbo bora wa Hip Hop. Nguvu ya wimbo huo hapana shaka ndiyo imemuwezesha pia kuondoka na tuzo ya msanii bora wa Hip Hop na Mtunzi bora wa mashairi ya Hip Hop. Kala aliweza kuwapenya wasanii wazito kama Fid Q, Joh Makini, Mwana FA, Profesa Jay na mdogo wake katika game Stamina wa Moro Town waliokutana nae katika vipengele vya Hip Hop. Wimbo huu ulitengenezwa na mtayarishaji chipukizi Dee Classic ambae pia alikuwa anawania tuzo katika kipengele cha mtayarisha...