GOMO WA MADEREVA WAINGIA SIKU YA PILI LEO

Taswira nzima ya mabasi yaendayo mikoani katika Stendi ya Ubungo.MGOMO wa madereva umeingia siku ya pili leo baada ya kuanza jana asubuhi huku wakazi mbalimbali wakiwemo wa jijini Dar wakilazimika kutembea kwa mguu kwenda kwenye maeneo yao ya kufanyia shughuli za kila siku.
Wananchi wakiwa wametaharuki katika eneo la Ubungo kutokana na mgomo unaoendelea.Mitaa mbalimbali ya Jiji la Dar asubuhi hii imeonekana kujaa magari binafsi huku bajaji na bodaboda zikionekana kuwa nyingi kuliko siku nyingine.
Katika Kituo cha mabasi yaendayo mikoani Ubungo, mabasi matatu ya Kampuni ya Shabiby Line yameripotiwa kuondoka kituoni hapo kuelekea Morogoro na Dodoma yakiwa chini ya ulinzi mkali wa eskoti ya askari polisi.

Comments

Popular posts from this blog