Posts

Wassira Ateuliwa Mwenyekiti Bodi Kumbukumbu ya Nyerere

Image
Stephen Wassira. RAIS John Magufuli amemteua Stephen Wassira kuwa Mweyekiti wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere,  nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Prof. Mark Mwandosya. You May Like

Manji kuisuka Yanga upya

Image
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Matawi ya Yanga Dar es Salaam, Boas Ikupilika, Mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji amewaahidi kuisuka Yanga mpya kwenye dirisha dogo la Novemba. Manji pia ameahidi kumpa sapoti kubwa Kocha Mwinyi Za­hera kuhakikisha sifa ya Yanga inarejea kwani amewakubali wachezaji baada ya kuwaona kwenye Uwanja wa Taifa hivi ka­ribuni alipokwenda kuwaangalia. Usajili wa dirisha dogo umepangwa kuanzia Novemba 15 hadi Desemba 15, mwaka huu ambapo timu hupata nafasi ya kuongeza wachezaji wach­ache kulingana na upungufu wao. Ikupilika amethibitisha kuwa Manji amekuwa akihusika katika mambo mbalimbali ndani ya klabu, amemuahidi Zahera kuwa, atamsaidia kutimiza ma­hitaji yake kwa kufanya usajili wa wachezaji ambao atahitaji kwenye dirisha dogo. “Manji aliomba muda kidogo kabla ya kurejea rasmi wakati wowote, lakini kuna baadhi ya majukumu ambayo amekuwa ak­itekeleza kama kiongozi wetu. Amekuwa akishauri mambo mengi kuhusu timu yetu,” alidokeza kion­go

Utapeli mkubwa waibuka 40 ya Mzee Majuto

Image
AMA KWELI kufa kufaana! Hayo ndiyo maneno unayoweza kusema endapo yatakufikia madai ya utapeli mzito unaofanywa na baadhi ya watu wakiwemo wasanii wa kuchangisha pesa kinyume na taratibu wakidai eti ni kwa ajili ya kufanikisha 40 ya marehemu Amri Athumani ‘Mzee Majuto’ inayotarajiwa kufanyika hivi karibuni. Taarifa hiyo ya kushtua ilipenyezwa na mmoja wa wasanii wa komedi Bongo, Jabir Ally ‘Wajajo’ ambaye alidai kuwa, akiwa katika mishemishe zake Mitaa ya Kariakoo jijini Dar alikumbana na baadhi ya wafanyabiashara waliohoji juu ya uhalali wa watu hao kuchangisha michango ya 40 hiyo. Alisema: “Kuna jambo la kushangaza sana nimekutana nalo huku Kariakoo, kuna watu wanapita kwenye maduka na kuomba michango ya kufanikisha 40 ya Mzee Majuto, mimi sikuwa na taarifa ya utaratibu huo, nikahisi kuna utapeli unafanyika. “Lakini katika kufuatilia nikagundua yupo pia msanii aliyewahi kufanya kazi kwa karibu na Majuto, Bi Rehema, naye anapita kuomba michango, nilipomuuliz

Rais Magufuli - Huyu ndiye Mkuu wa Mkoa kinara anayepiga kazi hana mfano

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtaja mkuu wa mkoa wa Simiyu Mh. Anthony Mtaka, kuwa ndiye mkuu wa mkoa kinara anayepiga kazi na kwamba hana mfano licha ya kupuuzwa kabla  hajamteua. Hayo ameyasema leo mkoani Simiyu wakati akihutubia wananchi wa mkoa huo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jioni hii ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 7 katika mikoa ya kanda ya ziwa. Rais Magufuli ameeleza kuwa, wakati anajaribu kutafuta wakuu wa Wilaya na wakuu wa mikoa aliambiwa na vyombo vyake kuwa Mtaka hafai hata U-DC lakini yeye akaamua kumteua kuwa mkuu wa mkoa kwasababu anajua watu wazuri huwa wanapigwa vita sana. ''Nilipotaka kumteua niliuliza vyombo vyangu nikaambiwa hafai kabisa lakini nimeuliza ripoti ya Wakuu wa Mikoa wanaofanya kazi vizuri, wakaniletea Mtaka ndio namba moja na namba mbili ni yeye kwa kifupi hana mfano'', amesema. Aidha Rais Magufuli ambaye atakamilisha ziara yake katika mikoa hiyo siku ya

BAD NEWS: AJALI YA MAGARI MATANO MBEYA, WALIOFARIKI WAFIKA 15

Image
IDADI ya watu waliokufa katika Ajali ya lori iliyogonga Magari mengine manne kabla ya kupinduka na kuwaka moto kwenye mteremko mkali wa Iwalanje, eneo la Igawilo jijini Mbeya imefikia 15, baada ya majeruhi wengine wawili kufariki dunia wakati wakipewa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya. Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Dk. Petro Seme amesema kuwa majeruhi wengine 13 wanaendelea na matibabu hospitalini hapo na kati yao wawili hali zao ni mbaya. Ajali hiyo imetokea jana tarehe 07 Septemba, 2018 majira ya saa 10 jioni katika mteremko wa mlima wa Igawilo Jijini Mbeya baada ya Lori lililokuwa na shehena ya viazi, likitokea Tukuyu kwenda Mbeya Mjini kuyagonga magari matano likiwemo basi dogo lililokuwa na abiria.

Ugomvi wa DC na Mkuu wa Mkoa wamkera Rais Magufuli

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amekemea tabia ya wakuu wa wilaya na mikoa kugombana wakati wanapotumikia wananchi. Ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa wilaya ya Tarime mkoani Mara wakati wa ziara yake ya kikazi, ambapo kuna mgogoro mkubwa kati ya DC wa wilaya Glorius Luoga na mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Daud Ngicho na mkuu wa mkoa huo Adam Malima. Rais Dkt. Magufuli ameonyesha kukerwa na misiguano ya viongozi wa mkoa wa Mara unaofanya hata miradi mbalimbali ya maendeleo kukwama kufuatia DC Luoga na RC Malima kutofautiana. “Kwanini mnagombana, wewe DC uko chini ya RC Malima, umheshimu na si kugombana kila wakati mpaka shughuli za maendeleo zinakwama,”amesema JPM Hivi karibuni  Rais pia alikemea mgogoro kati ya mkuu wa wilaya ya Chemba na Naibu waziri wa Fedha, Dkt. Ashatu Kijaji na viongozi wa wilaya hiyo wakati wa kuzindua barabara inayounganisha Afrika.

Chozi la Mkurugenzi wilaya ya Serengeti lamuokoa kutumbuliwa na Mh. rais

Image
Mkurugenzi wilaya ya Serengeti bwana Juma Hamsini ameepuka rungu la Mh. rais Magufuli la kutumbuliwa baada ya mbunge wa wilaya hiyo kupitia chama cha Chadema bwana Marwa Ryoba kumtaka Rais kuchukua uamuzi wa kumuondoa mkurugenzi huyo. Bwana Marwa amedai kuwa mkurugenzi huyo ni mwizi sana ndio tatizo la wilaya hiyo kutoendelea mbunge huyo alisema:-“Mimi nakupenda Mh rais lakini kwa mkurugenzi huyu tuna mkurugenzi mwizi, naomba niseme ameenda WMA akawalaghai wakampa milioni ishirini akaenda akakutana na aliyekuwa rasi wa mkoa akampa rasi wa mkoa milioni tatu akarudi milioni kumi na sana akaweka mfukoni eti anaenda kumugawia mkuu wa wilaya hakuwagawia akaweka mfukoni mpaka leo,Takukuru mkoa wanajua wilaya wanajua” mbunge huyo aliongeza ” Mh. rais sio hilo tu juzi kwenye kamati ya bunge mkurugenzi huyu wamefukuzwa na kamati ya bunge kutokana na fedha za miradi ya maendelea ambazo hazionekani kwa mujibu wa taarifa za CAG kwenye vikao pia haji,kwahiyo mh;rais mimi sio kw

Mwanakwaya Aliyeuawa Gesti, Familia Yasimulia Mazito

Image
D AR ES SALAAM: Tukio la mwanakwaya wa Kwaya ya Vijana ya Kanisa la AICT-Chang’ombe (CVC) Mariam Charles, 25, (pichani) mkazi wa Keko Furniture, wilayani Temeke jijini Dar aliyekutwa ameuawa kwenye Gesti ya East London, Mtaa wa Kwa Hamad Bonge, Temeke limeendelea kutikisa mjini na Risasi Jumamosi linakupa undani wake. Tukio hilo linadaiwa kutokea Septemba 5, mwaka huu katika nyumba ya wageni aliyokuwa amefikia mchumba wake aliyetajwa kwa jina la Frank ambaye amehusishwa na mauaji hayo. TUMSIKILIZE KAKA WA MAREHEMU Akizungumza  kaka wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Enock Charles, alisema kwamba alipata taarifa za kifo cha mdogo wake siku ya Jumatano (Septemba 5) asubuhi baada ya kutumiwa ujumbe na mama yao mzazi. “Mimi ninaishi Kigamboni, Jumatano asubuhi nikiwa kwenye mishemishe zangu, mama alinitumia SMS kwamba kuna matatizo nyumbani. “Nilimuuliza ni kuhusu nini akaniambia ni kumhusu Mariam. Nilishangaa kwa maana siku ya Ijumaa (jana) tulikuwa t

Breaking News: Baba Mzazi wa Profesa Jay Afariki Dunia

Image
       Profesa J. MBUNGE wa Mikumi kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),  Joseph Haule (Profesa Jay), amefiwa na baba yake mzazi leo akiwa katika Hospitali ya  St. Kizito,  Mikumi, ambapo alikuwa asafirishwe kwenda kupata matibabu zaidi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Prof. Jay amethibitisha kifo hicho katika mawasiliano aliyoyafanya kwa njia ya simu akiwa Dodoma.

Mashabiki watoa ya moyoni baada ya Diamond kumpost Irene Uwoya

Image
 Wiki hii wakati muimbaji Diamond Platnumz anahojiwa na Wasafi TV alifunguka mambo mbalimbali kuhusu maisha yake pamoja na kueleza kuwa kwa sasa hayupo kwenye mahusiano na mwanamke yeyote. Hatua hiyo ilikuja baada ya muimbaji huyo kumtuhumu Hamisa Mobetto ambaye ni mzazi mwenzake kwamba alienda kwa mganga ili airoge familia yake. Ijumaa hii muimbaji huyo ameibua hisia tofauti mtandaoni kwa mashibiki wake na wadau wa burudani baada ya kupost picha ya mke wa rapa Dogo Janja, Irene Uwoya bila kuandika ujumbe wowote. Kama unavyojua picha inazungumza zaidi ya maneno 1000 ambapo wadau wengi katika mitandao ya kijamii wamekuwa na maoni tofauti huku wengi wakihisi msanii huyo anatafuta kiki kupitia mrembo huyo. Angalia maoni ya mashabiki hao. masikini_jr Kuwa Star ili uwe na amani oa mwanamke mwenye sura ya babake kwasababu Mdogo wake dullysykes anapenda ku review mafile mazuri kama yote duh!!! Sasa janjaro kama nakuona 😂 😂 😂 saidsabin70 @evansmbesigwe hii n

Linah afunguka kuhusu unene wake.

Image
Mwanadada Linah Sanga amefunguka na kusema kuwa swala la kuongezeka kwa mwili wake baada ya yeye kujifungua hakuathiri kazi zake kwa sababu anaweza kufanya kitu chochote jukwaani kuwafurahisha mashabiki wake, Hii inakuja baada ya moja ya picha yake ya wikiendi hii kusambaaa sana katika mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiwa kama amenenepa sana na kuwa anaweza kushindwa kufanya show nzuri kama zamani, Akiongea na  Clouds fm Linah anasema; "Mazoezi nafanya ya kawaida tu, naupenda sana mwili wangu, mimi naona kawaida tu kuongezeka kwangu hakujaniathiri chochote nafanya kazi zangu kama kawaida, napiga shoo jukwaani na najiona ni mwepesi kama kawaida, unajua kuwa watu wembaba lakini wazito, lakini mimi unene nilionao haunipi changamoto zozote ninapokuwa jukwaani nawaburudisha mashabiki wangu kama kawaida, halafu ujue kwamba mimi sio dansa mimi ni mwanamuziki naimba nitakavyo sio lazima niruke ruke"

Zari aandika waraka mzito

Image
 Mashabiki wengi wameupokea kwa furaha ujumbe wa Zari the Bosslady kwa kile wanachoamini ujumbe huo unamlenga Hamisa Mobetto. Zari The Bosslady ametumia ukurasa wake wa Instagram kueleza kuwa; 'Usimpe mtu yeyote nguvu ya kuchagua kati yako na mtu mwingine... kama hukubaliki, ondoka na usiangalie nyuma na wala usimweleze mtu. Situmi chochote zaidi ya upendo kwako , Sasa futa machozi na urekebishe,'. "Never give anyone the power to 'choose' between you and someone else. If they can't decide, decide for them. Walk it away and never look back. Go where your celebrated. Don't even explain i to anyone, your journey is yours. NOBODY has to understand it but YOU. Sending nothing but love you sis in TZ, Now wipe those tears and fix that. Ujumbe huo wa Zari unakuja ikiwa ni hivi karibuni Hamisa Mobetto ameingia kwenye shutuma nzito kwa kile kinachodaiwa kuwa alikuwa akipanga njama za kumloga Diamond Platnumz na familia yake. Zari the Bosslady

Hiki ndio Kilichomkuta Mchina baada ya kumuita Rais Kenyatta nyani

Image
Mfanyabiashara raia wa China anaeishi nchini Kenya, Liu Jiaqi amekamatwa kufuatia kusambaa kwa video yake katika mitandao ya kijamii inayomuonesha akiwakashifu raia pamoja na Rais wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta. Taarifa ya uhamiaji nchini Kenya imesema “Kibali chake cha kazi kimefutwa na atafukuzwa nchini kutokana na ubaguzi”. Video hiyo iliyosambaa katika katika mitandao ya kijamii inamuonesha mfanyabiashara huyo akirekodiwa na mfanyakazi wake huku akisema, “Kila mmoja, kila mkenya ni kama nyani, akiwamo Uhuru Kenyatta, hao wote”. Aliposhauriwa na mfanyakazi huyo kuwa arejee kwao China endapo hapendi kuendelea kuishi Kenya, alijibu, “Mimi si mkazi wa hapa, sipapendi hapa, watu wake ni kama nyani na sipendi kuongea nao, pananuka harufu mbaya, masikini na watu ni weusi, siwapendi. Kwanini hawako kama watu weupe, kama wamarekani ?”. Kwa mujibu wa msemaji wa ubalozi wa China nchini Kenya, Zhang Gang, video hiyo ilirekodiwa mwezi Juni na tayari alishachukuliwa hat

Tambua faida ya matumizi ya Choya (rosela) kiafya

Image
Rosela ni ni maua yanayo julikana kabisa  pia  huoeshwa au kupandwa mazingira ya kawaida haswa nyumbani, maua haya yanapatikana kirahisi katika nyumba za ndugu, jamaa na marafiki na sehemu zinginezo japo kuwa baadhi ya watu huyaita maua damu. Zifuatazo ni faida za kutumia rozela. Maua ya rosella utengenezwa juisi inayo ongeza damu mwilini kwa haraka Hutumiwa kama mboga na mbegu zake hutoa mafuta yanayo tumika kama dawa ya vidonda. Dawa ya magonjwa mbalimbali kama kushusha presha, sukari, uric acid mwilini, inatibu kikohozi na mafua, ina punguza mwili pia hutengeneza ngozi na kuifanya iwe laini. Maua ya rosela hutumika kutengenezea juisi , chai ,jam, pia hutumiwa kama rangi ya chakula. Faida zinginezo; Maua ya rosella yana vitamin C,A,D B1,B2,calcium,magnesium,iron, nk Muhimu. Kulingana na matumizi na faida za maua ya rosella ni vyema kupanda kwa wingi maua haya katika mazingira ya nyumbani kama ya navyo pandwa maua mengine ili iwe rahisi kuyapata pindi yanap

BREAKING NEWS: Rais Magufuli amteua Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU

Image
 Rais John Magufuli amemteua Kamishna wa Polisi, Diwani Athumani kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU) kuchukua nafasi ya Kamishna wa Polisi Valentino Mlowola ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Mabasi Mawili ya Wanafunzi Yagongana, Dereva Afariki

Image
Muonekano wa basi la shule ya Kivulini baada ya ajali. Basi la shule ya Nyamunge likionekana baada ya ajali. Mabasi mawili ya wanafunzi ya Shule za Kivulini na  Nyamunge yamengana uso kwa uso katika Barabara ya Mwanza–Simiyu katika eneo la Nane Nane mkoani Mwanza na kusababisha kifo cha dereva na wanafunzi wanane wa shule hizo kujeruhiwa.

Wakili wa kesi ya Mbowe na wenzake ajitoa

Image
WAKILI Jeremiah Mtobesya aliyekuwa akiwawakilisha Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na viongozi wenzake nane wa chama hicho, amejitoa kwenye kesi hiyo leo Agosti 23 mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri. Mtobesya amejitoa katika kesi hiyo baada ya Mahakama ya Hakimu Kisutu kutupilia mbali maombi yao ya kutaka kesi hiyo ya jinai namba 112 ya mwaka 2018 iahirishwe katika Mahakama ya Kisutu ili kusubiri  maombi yao na rufaa yaliyowasilishwa kwenye Mahakama ya Rufani yasikilizwe kwanza na kutolewa maamuzi. Kwa upande wake, hakimu Mashauri alitupilia mbali maombi hayo kwa maelezo kwamba, kifungu cha sheria walichotumia cha 225 (1) (2) cha Mwenendo wa Mashauri ya Jinai Sura ya 20 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 hakiipi mamlaka hayo. Ikumbukwe kwamba, Mbowe na wenzake wanakabiliwa na mashtaka 13 ikiwamo  kuhamasisha maandamano Februari 16 mwaka huu siku moja ya uchaguzi mdogo wa ubunge jimbo la Kinondoni yaliyosababisha

NAFASI ZA KAZI 45 HOSPITALI YA BUGANDO

Image
OFISI ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora imetangaza nafasi 45 za kazi Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza za Medical Attendant daraja la II, mwisho wa kutuma maombi ni 2018-08-29 MEDICAL ATTENDANT II.. – 45 POST Employer: Bugando Medical Centre Date Published: 2018-08-15 Application Deadline: FASI DUTIES AND RESPONSIBILITIES: i. Providing basic health education to in patients and relative ii. Ensuring that all utensils are clean. iii. Inspecting the Institute clinical areas. iv. Advising matron on all matters relating to cleaning duties. QUALIFICATION AND EXPERIENCE: Holder of an Ordinary Secondary School Certificate. Must have a Pre-Nursing Certificate OR Certificate in Community Health from recognized institution REMUNERATION: Salary Scale PMOSS.2.1. Login to Apply

Irene Uwoya ampa za uso shabiki Instagram

Image
 Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na akanti nyingi ‘fake’ za Instagram ambazo zinatumia majina ya mastaa na viongozi wa serikali na usipokuwa makini unaweza kugombana na kila mtu mtandaoni. Kwani akaunti hizo zimekuwa zikitumiwa na watu hao kwaajili ya kuwachonganisha mastaa kwa mastaa ili wapate followers. Hayo yamemkuta malkia wa filamu, Irene Uwoya baada ya kuingia kwenye majibizano na akaunti ‘fake’ ambayo inatumia jina la Jokatemwegeelo akidhani anabishana na Mhe DC Jokate, ambae kupitia mtandao huo anatumia jana Jokate Mwegelo. Kaunti hiyo ‘fake’ ilionekana ikidai muigizaji huyo wa filamu amekuwa akitumia muda mwingi kwenye kujiremba na sio kufanya kazi.

RC Mongella ashiriki mazishi ya Bibi yake Paul Makonda

Image
Na James Timber, Mwanza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella leo Agosti 23, ameungana na waombolezaji mbalimbali kushiriki mazishi ya Bi. Anna Makwega Manasse (81) ambaye ni Bibi wa Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Paul Makonda. Mazishi ya Bi. Manasse ambaye alifariki dunia juzi Agosti 21, Mwaka huu akiwa katika hospitali ya Rufaa Bugando Jijini Mwanza alikokuwa amelazwa kwa ajili ya matibabu, yamefanyika katika makaburi ya nyumbani yaliyopo Kahangala wilayani Magu. Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa serikali mkoani Mwanza, Mkuu wa Mkoa Mongella amewaombea kuwa na uvumilivu kwa  ndugu, jamaa na marafiki kutokana na msiba huo na kuwahimiza kumuombea kwa Mola ili apumzike kwa Amani.